Swali la 4: Katika Enzi ya Sheria, Mungu alimtumia Musa kutenda kazi Yake, hivyo kwa nini Mungu hamtumi mtu kutekeleza kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, lakini Mungu mwenye mwili Mwenyewe lazima aifanye?

Jibu:

Ni kwa nini lazima Mungu apate mwili ili kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho? ni swali ambalo wengi walio na kiu ya ukweli na wanatafuta kuonekana kwa Mungu wanalijali sana. Pia ni swali linalohusiana na kama tunaweza kunyakuliwa kwenda katika ufalme wa mbinguni. Kwa hiyo, ni muhimu sana kuelewa kipengele hiki cha ukweli. Ni kwa nini lazima Mungu ajipatie mwili ili kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho badala ya kumtumia mwanadamu kuifanya kazi Yake? Hili linaamuliwa na hali ya kazi ya hukumu. Kwa sababu kazi ya hukumu ni onyesho la Mungu la ukweli na onyesho la tabia Yake yenye haki ili kuwashinda, kuwatakasa, na kuwaokoa wanadamu.

…………

Kutoka kwa maneno ya Mwenyezi Mungu tunaona kwamba Kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho inajumuisha kuonyesha vipengele vingi vya ukweli, kuonyesha tabia ya Mungu, chote ambacho Mungu anacho na Alicho, kufichua siri zote, kuhukumu asili ya kishetani ya mwanadamu ya kumpinga Mungu na kumsaliti Mungu, kufichua na kuchangua maneno na mwenendo wa mwanadamu, na kufichua kiini kitakatifu na chenye haki cha Mungu na tabia isiyokosewa kwa wanadamu wote. Wakati wateule wa Mungu wanapitia hukumu kwa maneno ya Mungu, ni kana kwamba wako uso kwa uso na Mungu, wakifichuliwa na kuhukumiwa naye. Wakati Mungu anamhukumu mwanadamu, lazima amruhusu kuona dhihirisho la tabia Yake yenye haki, kana kwamba kuona kiini kitakatifu cha Mungu, kana kwamba kuona nuru kuu inayorushwa kutoka mbinguni, na kuona neno la Mungu ni kama upanga mkali ukatao kuwili unaoingia ndani ya moyo na roho ya mtu, ukimsababisha kuvumilia maumivu yasiyoelezeka. Ni kwa njia hii tu ndio mwanadamu anaweza kupata kutambua kiini chake potovu na ukweli wa upotovu wake, ahisi fedheha nzito, aone aibu, na asujudu mbele za Mungu kwa toba ya kweli, na kisha ataweza kukubali ukweli na kuishi kulingana na neno la Mungu, aachane kabisa na ushawishi wa Shetani, na aokolewe na kukamilishwa na Mungu. Kazi kama hii ya hukumu, utakaso, na wokovu wa mwanadamu inaweza tu kufanywa na Mungu mwenye Mwenyewe.

Baada ya kupitia hukumu kwa neno la Mwenyezi Mungu, sote tumehisi jinsi utakatifu na tabia yenye haki ya Mungu ni visivyokosewa na wanadamu. Kila herufi ya neno la Mungu ina uadhama na ghadhabu, kila neno hugonga hadi kiini cha mioyo yetu, likifichua kabisa asili yetu ya kishetani ya kumpinga Mungu na kumsaliti Mungu, pamoja na vitu vya tabia ya upotovu vilivyozikwa ndani kabisa mwa mioyo yetu ambavyo hata sisi wenyewe hatuwezi kuviona, likituruhusu kutambua vile asili yetu na kina chetu vimejaa kiburi, kujidai, ubinafsi, na udanganyifu, jinsi tunavyoishi kulingana na vitu hivi, kama pepo walio hai wakizurura duniani, wasiokuwa na hata kiasi kidogo cha ubinadamu. Mungu analiona hili kuwa la kuchukiza sana na la karaha. Tunahisi kufedheheshwa na kunyanyaswa na majuto. Tunaona ubaya na uovu wetu wenyewe na tunajua hatustahili kuishi mbele za Mungu, kwa hiyo tunasujudu sakafuni, tukiwa radhi kupokea wokovu wa Mungu. Katika kupitia hukumu kwa neno la Mwenyezi Mungu, tunashuhudia kweli kuonekana kwa Mungu. Tunaona kwamba utakatifu wa Mungu hauwezi kuchafuliwa na haki Yake ni isiyokosewa. Tunatambua makusudi yenye ari na upendo halisi ambao Mungu anajitahidi nao kumwokoa mwanadamu na tunaona ukweli na kiini cha upotovu wetu mikononi mwa Shetani. Hivyo, ndani ya mioyo yetu, tunaanza kuhisi kumcha Mungu na tunakubali kwa furaha ukweli na kutii mpango wa Mungu kwa ajili yetu. Kwa namna hii, tabia yetu potovu inatakaswa polepole. Mabadiliko tuliyofikia leo ni matokeo ya kupata mwili kwa Mungu kufanya kazi ya hukumu. Kwa hiyo mwaona, ni wakati ambao kupata mwili kwa Mungu anaonyesha ukweli tu, Anaonyesha tabia yenye haki ya Mungu na chote ambacho Anacho na Alicho kutekeleza kazi ya hukumu, wakati huo tu ndipo mwanadamu anaona kuonekana kwa nuru ya kweli, kuonekana kwa Mungu, na anaanza kuwa na ufahamu wa kweli kuhusu Mungu. Ni namna hii pekee ndipo tunaweza kuona kwamba ni Mungu tu anaweza kututakasa na kutuokoa. Isipokuwa Kristo, hakuna mwanadamu anayeweza kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho.

…………

Kutoka kwa neno la Mwenyezi Mungu tunaona waziwazi kwamba kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho lazima ifanywe kwa njia ya kuonyesha ukweli, tabia ya Mungu, na uweza na hekima ya Mungu kumshinda, kumtakasa, na kumkamilisha mwanadamu. Mungu anaonekana Mwenyewe kuifanya kazi hii ya hukumu katika siku za mwisho. Kazi hii inaashiria mwanzo wa enzi moja na mwisho wa enzi nyingine. Kazi hii lazima ifanywe na kupata mwili kwa Mungu, hakuna mwanadamu anayeweza kuifanya kazi hii badala Yake. Ni kwa nini watu wengi wanaamini kwamba Mungu anapaswa kuwatumia wanadamu kuifanya kazi Yake yote, badala ya kupata mwili ili kuifanya kazi hiyo Mwenyewe? Hili haliaminiki! Je, wanadamu wanakaribisha ujio wa Mungu kweli? Kwa nini kila mara kuna watu wengi sana wanaotumaini kwamba Mungu atawatumia wanadamu kuifanya kazi Yake? Hili ni kwa sababu wanadamu hufanya kazi kwa mujibu wa dhana zao, wao hufanya mambo tu jinsi watu wanavyofikiri yanapaswa kufanywa, kwa hiyo wanadamu huwaabudu wanadamu wengine kwa urahisi, huwakweza na kuwafuata, Lakini njia ya Mungu ya kufanya kazi huwa haipatani kamwe na dhana za mwanadamu, Hafanyi mambo jinsi mwanadamu anavyofikiri yanapaswa kufanywa. Kwa hivyo mwanadamu huona ugumu kulingana na Mungu. Kiini cha Mungu ni ukweli, njia, na uzima. Tabia ya Mungu ni takatifu, yenye haki na isiyokosewa. Mwanadamu mpotovu, hata hivyo, amepotoshwa kabisa na Shetani, na amejaa tabia ya kishetani, na yeye huona ugumu kulingana na Mungu. Kwa hiyo, mwanadamu huona ugumu kukubali kazi ya kupata mwili kwa Mungu na hataki kusoma na kuchunguza, badala yake anamwabudu mwanadamu na kuweka imani isiyoweza kutambua katika kazi yake, akiikubali na kuifuata kana kwamba ni kazi ya Mungu. Tatizo ni lipi hapa? Ungesema, wanadamu hawana habari hata kidogo kuhusu nini maana ya kumwamini Mungu na kupitia kazi Yake, kwa hiyo, kazi ya Mungu katika siku za mwisho lazima iwe na maonyesho ya ukweli na kupata mwili ili kutatua matatizo yote ya wanadamu wapotovu. Kuhusu swali lenu la kwa nini Mungu hamtumii mwanadamu kuifanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, bado linahitaji jibu? Kiini cha mwanadamu ni mwanadamu, mwanadamu hamiliki kiini cha uungu, kwa hiyo mwanadamu hawezi kuonyesha ukweli, kuonyesha tabia ya Mungu, chote ambacho Mungu anacho na Alicho, na hawezi kuifanya kazi ya kuwaokoa wanadamu. Licha ya kuwa, wanadamu wote wamepotoshwa na Shetani na wana asili ya dhambi, hivyo wana sifa gani za kustahili kuwahukumu wanadamu wengine? Kwa kuwa mwanadamu mchafu na mpotovu hana uwezo wa kujitakasa na kujiokoa, anatarajia vipi kuwatakasa na kuwaokoa wengine? Wanadamu kama hao wangekabiliana na fedheha tu wakati watu wengine wangekataa kukubali hukumu yao. Mungu pekee ndiye mwenye haki na mtakatifu, na Mungu pekee ndiye ukweli, njia, na uzima. Kwa hiyo, kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho lazima itekelezwe na kupata mwili Kwake. Hakuna mtu anayeweza kuifanya kazi kama hii, huu ni ukweli.

Sasa kwa nini Mungu alimtumia mwanadamu kuifanya kazi Yake katika Enzi ya Sheria? Hii ni kwa sababu kazi ya Enzi ya Sheria na ile ya hukumu ya siku za mwisho zina hali tofauti. Katika Enzi ya Sheria, wanadamu walikuwa jamii ya binadamu iliyokuwa imezaliwa upya, walikuwa wamepotoshwa na Shetani kwa kiwango kidogo tu. Kazi ya Yehova Mungu ilijumuisha hasa kutangaza rasmi sheria na amri kutoa mwongozo kwa mwanadamu wa mwanzo kuhusu namna ya kuishi duniani. Hatua hii ya kazi haikulenga kuibadilisha tabia ya mwanadamu, haikuhitaji kuonyesha ukweli mwingi zaidi. Mungu alihitaji tu kumtumia mwanadamu kuwasilisha kwa Waisraeli sheria Alizokuwa Ameunda, ili Waisraeli wangejua namna ya kuzitii sheria, kumwabudu Yehova, na kuishi maisha ya kawaida duniani. Baada ya kufanya hivyo, hatua hiyo ya kazi ilikamilishwa hivyo. Kwa hiyo, Mungu angemtumia Musa kuikamilisha kazi ya Enzi ya Sheria, Hakuhitaji kupata mwili ili kuitekeleza kazi hiyo Mwenyewe. Kinyume chake, kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho inalenga kuwaokoa wanadamu, ambao wamepotoshwa na Shetani kwa hali kubwa. Kutoa vifungu vichache vya neno la Mungu na kutangaza rasmi sheria chache hakutatosha kamwe katika hali hii. Kiasi kikubwa cha ukweli lazima kionyeshwe. Tabia ya Mungu ya asili, chote ambacho Mungu anacho na Alicho lazima vionyeshwe kabisa, ukweli, njia, na uzima lazima vifunguliwe kwa ajili ya wanadamu wote, kana kwamba Mungu angejifichua Mwenyewe uso kwa uso na wanadamu, Akimruhusu mwanadamu kuelewa ukweli na kumjua Mungu, na kwa kufanya hivyo, Anawatakasa, Anawaokoa na kuwakamilisha wanadamu kabisa. Mungu lazima afanye hili Mwenyewe binafsi kwa njia ya kupata mwili, hakuna mwanadamu anayeweza kuifanya kazi hii badala Yake. Mungu anaweza kuwatumia manabii kutoa vifungu vichache vya neno Lake, lakini Mungu hawaruhusu manabii kuonyesha tabia ya Mungu ya asili, chote ambacho Mungu anacho na Alicho, au kuonyesha ukweli wote, kwa sababu mwanadamu hastahili kufanya hivyo. Kama Mungu angemtumia mwanadamu kuonyesha tabia na ukweli Wake wote, kuna uwezekano wa kumwaibisha Mungu, kwa sababu mwanadamu ana tabia potovu, ana uwezekano wa kuzisaliti dhana na njozi zake mwenyewe, lazima kuwe na uchafu katika kazi yake, ambalo lingemfedhehesha Mungu na kuathiri matokeo ya jumla ya kazi ya Mungu. Pia, mwanadamu anafaa kuchukua chote ambacho anacho na alicho kwa ajili ya chote ambacho Mungu anacho na Alicho, akichukua uchafu wa mwanadamu katika kazi yake ya ukweli. Hili husababisha kumwelewa Mungu visivyo na kumfedhehesha. Pia, kama Mungu angemtumia mwanadamu kuonyesha tabia na ukweli Wake wote, watu hawangetaka kukubali na hata wangepinga, kwa sababu ya uchafu wa mwanadamu. Kisha Shetani angewalaumu na kuwatafutia makosa. akichochea mwanadamu kutoridhika na Mungu, akichochea uasi, na kuwachochea waanzishe ufalme wao wenyewe ulio huru. Hili ni tokeo la mwanadamu kuifanya kazi ya Mungu. Hasa, katika hali ya Mungu kumwokoa mwanadamu aliyepotoshwa kabisa katika siku za mwisho, wanadamu hawakubali na kutii kwa urahisi kazi ya kupata mwili kwa Mungu. Kwa hiyo kama Mungu angewatumia wanadamu kuifanya kazi hii, wanadamu huenda hawangekubali zaidi na kutii kiasi hicho. Je, huu si ukweli mtupu? Watazame wazee wa kanisa na wachungaji wa ulimwengu wa kidini, je, upinzani na shutuma yao ya kazi ya kupata mwili kwa Mungu ni tofauti kwa hali yoyote na vile makuhani wakuu na Mafarisayo wa Kiyahudi walimpinga Bwana Yesu awali? Mungu kuwaokoa wanadamu wapotovu si kazi rahisi. Lazima tuelewe vile Mungu anafikiria!

…………

Kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho kwa njia ya kupata mwili ni ya maana kweli. Mungu amepata mwili duniani katika siku za mwisho, Akiishi miongoni mwa wanadamu na kulitangaza neno Lake kwa wanadamu, Akionyesha tabia ya Mungu Mwenyewe na chote ambacho Mungu anacho na Alicho kwa umati. Yule ambaye Mungu anampenda na yule ambaye Mungu anamchukia, yule ambaye ghadhabu ya Mungu inaelekezwa, yule Anayemwadhibu, hali Yake ya hisia, matakwa Yake kwa wanadamu, kusudi Lake kwa wanadamu, mtazamo wa njozi wa mwanadamu kuhusu maisha, maadili, n.k., Anawaarifu wanadamu kuhusu mambo haya yote, Akimruhusu mwanadamu kuwa na malengo wazi katika maisha ili wasihitaji kutafutatafuta bila malengo katika ufuatiliaji wa dini usio dhahiri. Kuonekana kwa kupata mwili kwa Mungu “anahitimisha enzi ambapo Yehova alionekana mgongo tu, na pia anahitimisha enzi ya mwanadamu kuamini katika Mungu asiye dhahiri.” Wale wote ambao wamepitia neno na kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho wana utambuzi wa pamoja: Hata ingawa tumepitia hukumu na kuadibu kwa Mungu, tumevumilia kila aina ya majaribio na usafishaji, na tumeteswa sana na ukimbizaji wa kinyama, katili na mateso ya serikali ya Kikomunisti ya Uchina, tumeiona tabia yenye haki ya Mungu ikija kwetu, tumeona uadhama na ghadhabu ya Mungu na uweza na hekima Yake, tumeona dhihirisho la chote ambacho Mungu anacho na Alicho, kama vile tu tungemwona Mungu Mwenyewe. Ingawa hatujauona mwili wa kiroho wa Mungu, tabia ya asili ya Mungu, uweza na hekima Yake, na chote ambacho Anacho na Alicho, vimefichuliwa kwetu kwa ukamilifu, kana kwamba Mungu alikuwa Amekuja mbele yetu, uso kwa uso, Akituruhusu tumjue Mungu kweli na tuwe na moyo unaomcha Mungu ili tuweze kutii mpango wowote ambao Mungu anao kutuhusu hadi kifo. Sote tunahisi kwamba katika neno na kazi ya Mungu tunamwona na kumjua Mungu kwa njia halisi na kweli, na tumeacha kabisa dhana na njozi zote na tumekuwa wale wanaomjua Mungu kweli. Awali, tulifikiria tabia ya Mungu ni yenye upendo na huruma, kumwamini Mungu kungesamehe dhambi za mwanadamu siku zote. Lakini baada ya kupitia hukumu ya neno la Mwenyezi Mungu, tumekuja kuelewa kweli kwamba tabia ya Mungu si yenye huruma na ya upendo tu, pia ni, yenye haki, adhimu, na yenye ghadhabu. Yeyote anayeikosea tabia Yake ataadhibiwa. Hivyo, tunaweza kumcha Mungu, kuukubali ukweli na kuishi kulingana na neno la Mungu. Kwa kupitia kazi ya Mwenyezi Mungu ya hukumu katika siku za mwisho, sote tumekuja kuelewa kweli na kwa uhalisi kwamba tabia ya Mungu ni takatifu, yenye haki, na isiyokosewa, tumepitia huruma na upendo wa Mungu, tumekuja kukubali kweli uweza na hekima ya Mungu, tumetambua jinsi Mungu amejishusha katika siri, tumekuja kujua makusudi Yake yenye ari, sifa nyingi za kupendeza, hali Yake ya hisia, uaminifu Wake, uzuri na wema Wake, mamlaka Yake, ukuu, na uchunguzi Wake makini wa kila kitu, n.k. chote ambacho Mungu anacho na Alicho kimeonekana mbele yetu, kana kwamba tunamwona Mungu Mwenyewe, kikituruhusu kumjua Mungu uso kwa uso. Hatumwamini na kumfuata Mungu tena kwa kutegemea dhana na njozi zetu, bali tunahisi uchaji na ibada ya kweli kwa Mungu, na kumwabudu na kumtegemea Mungu kweli. Tumetambua kwa kweli kwamba kama Mungu hangekuwa Amepata mwili mwenyewe kuonyesha ukweli na kumhukumu mwanadamu, hatungemjua Mungu kamwe, na hatungeweza kujiondolea dhambi na kufikia utakaso. Kwa hiyo haijalishi unavyoiona, kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho lazima ifanywe na Mungu mwenye mwili Mwenyewe, hakuna anayeweza kuchukua nafasi Yake. Kwa ajili ya dhana na njozi za mwanadamu, kama Mungu angemtumia mwanadamu kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho, Hangeweza kutimiza matokeo yanayotakikana.

Kimetoholewa kutoka katika Maswali na Majibu Bora zaidi Kuhusu Injili ya Ufalme

Iliyotangulia: Swali la 3: Mbona Mungu amepata mwili katika siku za mwisho, akiwa Mwana wa Adamu ili kufanya kazi ya hukumu? Ni nini tofauti ya kweli kati ya mwili wa roho wa Bwana Yesu kufufuliwa kutoka kwa kifo na Mwana wa Adamu mwenye mwili? Hili ni suala ambalo hatulielewi—tafadhali shiriki ushirika kuhusu hili.

Inayofuata: Swali la 5: Kwa nini inasemwa kwamba wanadamu potovu lazima waokolewe na Mungu mwenye mwili? Hili ni jambo ambalo watu wengi sana hawalielewi—tafadhali shiriki ushirika kuhusu hili.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp