Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 231

27/09/2020

Inaweza kusemwa kwamba matamko yote ya leo yanatabiri masuala ya siku za baadaye, yanahusu Mungu kufanya mpango kwa ajili ya hatua inayofuata ya kazi Yake. Mungu karibu amemaliza kazi Yake ndani ya watu wa kanisa, baadaye Atatumia ghadhabu kuonekana mbele ya watu wote. Kama asemavyo Mungu, “Nitawafanya watu walio duniani wakubali mambo Yangu, na mbele ya ‘kiti cha hukumu,’ matendo Yangu yatathibitishwa, ili yakubalike miongoni mwa watu walio kote duniani, ambao watasalimu amri.” Je, uliona chochote ndani ya maneno haya? Humu mna muhtasari wa sehemu inayofuata ya kazi ya Mungu. Kwanza, Mungu atawafanya walinzi wote wanaotawala kwa nguvu za kisiasa waridhike kabisa na wajiondoe katika jukwaa la historia, kutowahi kupigania hadhi tena au kufanya hila na kula njama. Kazi hii lazima itekelezwe kwa njia ya Mungu kusababisha mabaa mbalimbali duniani. Lakini Mungu hataonekana; kwa sababu, wakati huu, nchi ya joka kubwa jekundu bado itakuwa ni nchi ya uchafu, Mungu hataonekana, lakini ataibuka tu kwa njia ya kuadibu. Hiyo ndiyo tabia ya Mungu yenye haki, na hakuna anayeweza kuiepuka. Katika wakati huu, vyote vinavyoishi katika taifa la joka kubwa jekundu vitapitia maafa, ambavyo kwa kawaida ni pamoja na ufalme ulio duniani (kanisa). Huu ndio hasa wakati ambao ukweli hujitokeza, na kwa hiyo unapitiwa na watu wote, na hakuna anayeweza kuepuka. Hili limejaaliwa na Mungu. Ni kwa sababu ya hatua hii ya kazi hasa ndio Mungu asema, “Huu ndio wakati wa kutekeleza mipango mikuu.” Kwa sababu, katika siku za baadaye, hakutakuwa na kanisa duniani, na kwa ajili ya majilio ya machafuko, watu wataweza tu kufikiria kuhusu kile kilicho mbele yao na watapuuza kila kitu kingine, na ni vigumu kwao kumfurahia Mungu katikati ya machafuko, hivyo, watu wanatakiwa kumpenda Mungu kwa moyo wao wote katika wakati huu wa ajabu, ili wasikose nafasi. Ukweli huu unapopita, Mungu amelishinda kabisa joka kubwa jekundu, na hivyo kazi ya ushuhuda wa watu wa Mungu imefika mwisho; baadaye Mungu ataanza hatua inayofuata ya kazi, Akifanya uharibifu kwa nchi ya joka kubwa jekundu, na hatimaye kuwagongomelea watu juu chini msalabani kotekote katika ulimwengu, baadaye Atawaangamiza wanadamu wote—hizi ni hatua za siku za baadaye za kazi ya Mungu. Hivyo, mnapaswa kutaka kufanya lote muwezalo kumpenda Mungu katika mazingira haya ya amani. Katika siku za baadaye hamtakuwa na nafasi zaidi za kumpenda Mungu, kwani watu huwa tu na nafasi ya kumpenda Mungu katika mwili; wanapoishi katika ulimwengu mwingine, hakuna atakayenena kuhusu kumpenda Mungu. Je, hili si jukumu la kiumbe aliyeumbwa? Kwa hiyo unapaswa kumpenda Mungu vipi katika siku zako za uhai? Umeshawahi kufikiri juu ya hili? Je, unangoja mpaka ufe ili umpende Mungu? Je, haya si maneno matupu? Leo, kwa nini hufuatilii kumpenda Mungu? Je, kumpenda Mungu huku ukiwa na shughuli nyingi kunaweza kuwa upendo halisi wa Mungu? Madhumuni ya kusema kwamba hatua hii ya kazi ya Mungu itafika mwisho hivi punde ni kwa sababu Mungu tayari ana ushuhuda mbele ya Shetani; hivyo, hakuna haja ya mwanadamu kufanya lolote, mwanadamu anatakiwa tu kufuatilia kumpenda Mungu katika miaka ambayo yuko hai—hili ndilo jambo muhimu. Kwa sababu masharti ya Mungu si mengi, na, zaidi ya hayo, kwa kuwa kuna hamu kuu ndani ya moyo Wake, Amefichua muhtasari wa hatua inayofuata ya kazi kabla ya hatua hii ya kazi kumalizika, ambalo linaonyesha kwa dhahiri kuna kiasi gani cha muda: kama Mungu hangekuwa na hamu ndani ya moyo Wake, je, Angeyanena maneno haya mapema hivyo? Ni kwa sababu muda ni mfupi ndio maana Mungu anafanya kazi kwa njia hii. Inatarajiwa kwamba mnaweza kumpenda Mungu kwa mioyo yenu yote, kwa akili zenu zote, na kwa nguvu zenu zote, jinsi tu mnavyotunza maisha yenu wenyewe. Je, haya siyo maisha yenye maana kuu zaidi? Ni wapi pengine ambapo mngeweza kupata maana ya maisha? Je, ninyi si vipofu kabisa? Uko radhi kumpenda Mungu? Je, Mungu anastahili upendo wa mwanadamu? Je, watu wanastahili ibada ya mwanadamu? Kwa hiyo, unapaswa kufanya nini? Mpende Mungu kwa ujasiri, bila kusita, na uone kila ambacho Mungu atakufanya. Uone kama Atakuchinja. Kwa muhtasari, kazi ya kumpenda Mungu ni muhimu zaidi kuliko kunukuu na kuandika mambo kwa ajili ya Mungu. Unapaswa kukipa kipaumbele kilicho muhimu zaidi, ili maisha yako yaweze kuwa ya thamani zaidi na yajae furaha, na kisha unapaswa kusubiri “hukumu” ya Mungu kwako. Nashangaa iwapo mpango wako utahusisha kumpenda—Ningependa kwamba mipango ya watu wote iwe ile inayokamilishwa na Mungu, na iwe ya uhalisi.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp