Siri Niliyoishikilia kwa Kina Ndani ya Moyo Wangu

13/01/2018

Wuzhi Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong

Katika majira ya kuchipua ya mwaka wa 2006, nilinyang’anywa cheo changu kama kiongozi na nikarudishwa nilikotoka kwa sababu nilifikiriwa kuwa “bwana ndiyo” sana. Niliporejea mara ya kwanza, nilitumbukia ndani ya kikalibu cha mateso na maumivu makubwa. Sikuwahi kufikiri kwamba baada ya miaka mingi ya uongozi mambo yangeharibika kwa sababu ya kuwa “bwana ndiyo.” Huu ulikuwa ndio mwisho kwangu, nilidhani, kila mtu aliyenijua angejua juu ya kushindwa kwangu na ningefanywa kama mfano mbaya katika kanisa. Ningewezaje kukabiliana na wengine baada ya haya yote? Jinsi nilivyozidi kufikiria, ndivyo nilivyozidi kuwa hasi, mpaka hatimaye nikapoteza imani ya kuendelea kutafuta ukweli. Hata hivyo, wakati nilifikiri juu ya sadaka zote na matumizi niliyoyatoa katika miaka hii michache iliyopita, sikuweza kushawishika kuondoka Na nikafikiria: “Kama nikijimaliza kabisa na kukubali kushindwa, si jitihada zangu zote zitakuwa bure? Si watu watanidunisha hata zaidi? Siwezi kuruhusu hilo lifanyike! Ni lazima nijitetee na nisiwaache wengine waniangalie kwa dharau. Sasa, bila kujali ni jinsi gani ninavyopaswa kujitahidi, ni makosa mangapi yanayonipata, ni lazima nifanye haraka—siwezi kuondoka nusu njia! Almradi ninakumbuka mafundisho ya kushindwa na kuzingatia kutafuta ukweli, labda siku moja naweza kuwa kiongozi tena.” Mawazo haya yakiwa katika kumbukumbu, uhasi wote na huzuni zilififia na nilihisi nguvu iliyofanywa upya katika ukimbizaji wangu.

Kutoka wakati huo kuendelea, nilifanya kazi saa nyingi kila siku, kwa bidii nikila na kunywa neno la Mungu ili kujiandaa na ukweli wakati nikitafakari na kufanya utambuzi katika makosa yangu ya zamani. Niliandika insha nyingi mno zikieleza uzoefu wangu wa maisha, pamoja na mahubiri. Muda mfupi baadaye, nilipoona kwamba mbili kati ya insha zangu zilikuwa zimechaguliwa, nilihisi imani hata zaidi katika ukimbizaji wangu. Nilijifikiria mwenyewe: Endelea tu kufanya kazi na hivi karibuni sana ndoto yangu itakuja kuwa. Kwa njia hiyo, niliendelea katika ukimbizaji wangu na nilihisi nimefarijiwa kuwa hali yangu ilikuwa imerudi kuwa takribani “ya kawaida”.

Siku moja wakati wa kukuzwa kwa roho, nilivutiwa na kifungu fulani cha neno la Mungu: “Kama watu wanafaa kujielewa, ni lazima waelewe hali zao za kweli. Kipengele cha muhimu zaidi katika kuielewa hali ya mtu ni kuwa na ufahamu juu ya fikira zake na mawazo yake. Katika kila kipindi cha muda, fikira za watu zimekuwa zikidhibitiwa na jambo moja kubwa. Ikiwa unaweza kudhibiti fikira zako, unaweza kudhibiti vitu vilivyo nyuma yazo(“Watu Ambao Hufanya Madai Daima kwa Mungu Ndio Wenye Busara Kidogo Zaidi” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Nikiwaza juu ya neno la Mungu, ghafla niligeuza swali kwangu mwenyewe: Ni nini kinachotawala mawazo yangu sasa? Ni nini kilicho ndani ya mawazo yangu yote? Nilianza kutafakari kwa uangalifu juu ya mchakato wangu wa mawazo na, kwa uongozi wa Mungu, nilikuja kutambua kuwa tangu nilipobadilishwa, mawazo yangu yalikuwa yametawaliwa na tamaa ya kwamba “ni lazima nipate tena kwa juhudi sifa yangu ya zamani na hadhi yangu na nijitetee. Siwezi kuendelea kuangaliwa kwa dharau na wengine.” Wazo hili lilikuwa kama nguzo ya kiroho, likiniruhusu kustahimili katika kikalibu cha kukata tamaa kwangu na kunipa msukumo wa kufuatilia lengo langu. Nikiwa na wazo hili katika kumbukumbu, nilikuwa nimebakia “thabiti na asiyekubali kushindwa” chini ya mfululizo wa daima wa “matusi na aibu.” Wakati huu, nilitambua kwamba ukimbizaji wangu ulikuwa mchafu, uliojaa tamaa na usiokuwa mzuri hata chembe.

Nikifikiria nyuma, naona kwamba Mungu alikuwa amenifichua ili kuniruhusu kutafakari juu yangu mwenyewe na kuelewa asili yangu mwenyewe ya kishetani ili niweze kuwa na msingi dhabiti na wazi katika ukimbizaji wangu wa ukweli, kutupa kwa uovu na dhambi na kupokea wokovu wa Mungu. Hata hivyo, kwa hakika sikumshukuru Mungu kwa zawadi Yake ya wokovu, wala kujichukia mwenyewe kwa maovu niliyoyafanya. Aidha, sikujilaumu au kuhisi kujuta kwa ajili ya kushindwa kufikia matarajio ya matumaini ya Mungu. Badala yake, nikiendeshwa na asili ya kiburi kwamba “ni lazima nishinde kwa vyovyote,” Nilijiingiza katika upangaji wa njama hii, nikifikiria tu siku ambapo ningepanda ngazi tena, kuteuliwa tena kama kiongozi, na kurejesha sifa ambayo nilikuwa nimeiharibu kabisa. Kwa ufanisi, nilikuwa na matumaini ya kujenga taswira yangu mwenyewe ili wengine waipende na kuiabudu. Nilikuwa na kiburi kupita kiasi na sikuwa na uchaji hata kidogo au kumuogopa Mungu ndani ya moyo wangu. Je, sikuwa nimekosa kutii mipango na mipangilio ya Mungu? Je, sikuwa najiweka mwenyewe katika upinzani na Mungu? Kutafakari nyuma juu ya hali yangu ya zamani, woga ulinijaa. Singewahi kufikiri kwamba tamaa kama hiyo isiyowezekana ilisababisha mawazo yangu. Si ajabu kwamba Mungu alisema, “ikiwa unaweza kudhibiti fikira zako, unaweza kudhibiti vitu vilivyo nyuma yazo.” Kweli. Katika siku za nyuma, niliona mawazo yangu kuwa dhana za muda mfupi tu na kamwe sikuchukua muda kuyachambua na kuyaelewa. Ni sasa tu ninapoelewa kwamba kuyafahamu mawazo ya mtu na kuyachambua kikamilifu mambo yaliyoshikiliwa ndani ya moyo wa mtu ni muhimu sana kwa kuelewa asili ya ndani ya mtu!

Asante Mungu kwa kunurishwa huku, ambako kumeniinua kutoka kwa upofu. Kama sivyo, ningekuwa bado ningehadaiwa na udanganyifu wangu mwenyewe—nikiinuka mbele na tamaa pofu kwelekea kwa mauti yangu ya karibu sana. Ni gutuko lililoje la kushangaza! Katika mchakato huo, nilitambua pia kwamba kwa kunibadilisha, Mungu alikuwa akinilinda na kunipa wokovu. Kwa mtu aliye na kiburi na jazba, kama singekuwa nimepitia kikalibu cha mateso cha kuadibu na hukumu ya Mungu, siku zote ningekuwa mpinga Kristo na kuyakaribisha mauti yangu mwenyewe. Ewe Mungu, ninaapa kuacha ukimbizaji wote usio sawa, kuacha majivuno na tamaa yangu na kuitii kila amri Yako. Nitafuatilia ukweli kwa bidii, kutimiza kila wajibu wangu na kuishi kama mtu halisi na wa kweli ili kuufariji moyo Wako.

Iliyotangulia: Ni Nini Husababisha Uongo

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Ni Nini Husababisha Uongo

Xiaojing Jijini Heze, Mkoani Shandong Kila mara nilipoona neno la Mungu likituomba kuwa watu waaminifu na kuzungumza kwa usahihi,...

Maneno ya Mungu Yameniamsha

Miao Xiao Mji wa Jinan, Mkoa wa Shandong Katika siku zilizopita, nilikuwa daima nikifikiri kuwa Mungu aliposema “kibaraka na msaliti...

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp