Mbona Ujihusishe na Hila Unapomtumikia Mungu

14/01/2018

Hu Qing Jijini Suzhou, Mkoani Anhui

Nilipoona maneno ya Mungu yakisema: “Wale ambao huhudumu kama viongozi daima hutaka kuwa na ubunifu mkubwa, kuwa wazuri kuliko wengine, kupata hila mpya ili Mungu aweze kuona jinsi kweli walivyo na uwezo. … Wao daima hutaka kuringa; si huu ni ufunuo kwa usahihi wa asili ya kiburi?” (“Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Nilifikiri mwenyewe: Nani ana ujasiri kama huo kujaribu kupata ujanja mpya ya ubunifu? Nani hajui kuwa tabia ya Mungu haistahimili kosa la mwanadamu? Bila shaka siwezi kuthubutu! Mimi binafsi niliamini kuwa nilikuwa na moyo wa kumcha Mungu, na katika kazi yangu sikuthubutu kujaribu kutafuta mbinu. Hata hivyo, ilikuwa tu katika ufunuo wa Mungu wa ukweli ndio nilitambua kuwa kujaribu kutafuta mbinu mpya sio kile mtu huthubutu au hathubutu kufanya—kunaamuliwa kabisa na asili ya kiburi.

Mbona Ujihusishe na Hila Unapomtumikia Mungu

Si muda mrefu uliopita, niligundua kuwa kulikuwa na kanisa lilikuwa na kiongozi ambaye hakuwa na uwezo wa kutosha. Alilala wakati wa mikusanyiko na hakuwa na asili ya ukarimu, wakati mbia wake alikuwa na majukumu mengi. Kwa hiyo, nilitaka kubadilisha kiongozi huyu wa kanisa na kuruhusu mbia wake kufanya kazi ya kiongozi wa kanisa. Hata hivyo, nilikuwa na wasiwasi kuwa hili lingemsababisha kiongozi wa kanisa kuwa hasi, dhaifu, na kuacha imani yake, au kuwa angevuruga mambo katika kanisa. Baada ya kutafakari sana, nilifikiria juu ya “mpango wa kijanja.” Ningemfanya mbia wake achukue mawanda nzima ya kazi kwa siri; kila kitu kilichopangwa na kanisa kingeshughulikiwa na mbia wake, na kiongozi wa kanisa hangekuwa chochote bali mkubwa wa jina tu. Hivyo sikuwa nimemtafuta Mungu wala kutazama mipangilio ya kazi na kanuni za kazi. Nilikuwa nimefanya jambo hili tu baada ya kumwambia mbia wa kiongozi wa wilaya na mhubiri wa wilaya. Baada ya hiyo, nilijipongeza sana, nikiamini kuwa nilikuwa mwerevu sana na nilikuwa na busara kabisa katika kazi yangu. Nilifikiria: Ikiwa kiongozi angejua kuhusu hili, bila shaka angesema kuwa nina uwezo katika kazi yangu, na labda hata mwishowe angenipandisha cheo. Lakini sikuwa nimefikiria kuwa nilipomwambia kiongozi kuhusu hili, angesema: “Huyu ni wewe ukijaribu kutafuta ujanja mpya. Ni wapi katika mipangilio ya kazi ilisemwa kuwa ungeweza kufanya hivi? Kiongozi asiye na uwezo wa kutosha anaweza kubadilishwa, lakini hatuwezi kufanya kazi kulingana na mapenzi yetu wenyewe na kuweka kando kanuni za kanisa. Huu ni upinzani mkali dhidi ya Mungu. …” Baada ya kusikia mawasiliano haya kutoka kwa kiongozi, nilishtuka. Kamwe kabisa sikuwahi kufikiri kuwa ningejaribu kutafuta ujanja mpya bila kujua. Nilichoamini kuwa “mpango wa kijanja” kwa kweli ulikuwa ni upinzani mkali dhidi ya Mungu, na kweli nilikuwa na aibu sana wakati nilikabiliwa ukweli. Wakati huo, sikuwa na budi ila kufikiria matamko ya Mungu: “Kwa mfano, kama kiburi na majivuno, vingekuwa ndani yako, ungeona kwamba haiwezekani kuepuka kumwasi Mungu; ungehisi kulazimishwa kumwasi. Hutafanya hivyo kimakusudi; utafanya hivyo chini ya utawala wa asili yako ya kiburi na majivuno. Kiburi na majivuno yako vitakufanya umdharau Mungu na kumwona kuwa asiye na maana …(“Ni Kwa Kufuatilia Ukweli Tu Ndiyo Unaweza Kupata Mabadiliko Katika Tabia Yako” katika Kumbukumbu za Hotuba za Kristo). Ilikuwa kweli. Nilipokabiliwa na suala hili sikuwa nimemtafuta Mungu, wala sikulifikiri kupitia kanuni za kanisa. Nilikuwa nimetenda tu kulingana na mapenzi yangu. Niliona asili yangu ya kiburi na majivuno, kwamba sikuwa na moyo wa kumcha Mungu, na kuwa Mungu hakuwa na nafasi katika moyo wangu. Ni wakati huo tu ndipo nilipogundua kuwa kutafuta ujanja mpya hakukuwa kitu ambacho nilithubutu au sikuthubutu kufanya, lakini kilikuwa kitu kilichoamuliwa na asili yangu ya kiburi. Ikiwa singetambua asili yangu ya kiburi, singeweza kamwe kujielewa. Siku moja pengine nitaweza hata kufanya kitu kumpinga Mungu ambacho kitamfanya Ahisi maudhi na chuki. Ni wakati huo tu ndio niliona kuwa kumtumikia Mungu sio jambo rahisi. Ikiwa sina ukweli, ikiwa hakuna mabadiliko katika tabia, ikiwa sitambui asili yangu ya kiburi, ningeweza kuikosea tabia ya Mungu bila kujua. Hiyo kwa hakika ni hatari sana! Kwa sababu ya nuru ya Mungu, nilielewa kutokana na tukio hili ni kwa nini nyumba ya Mungu mara kwa mara imetutaka tufanye kazi kulingana na mipangilio ya kazi na kanuni. Ni kwa sababu hatujapata ukweli na hatuwezi kuhakikisha kwamba maoni yetu yote ni sahihi na kile tunachofanya ni cha faida kwa kanisa na watu wateule wa Mungu, lakini asili yetu daima ni yenye kiburi na sisi sote tunatafuta kujigamba, “kufunua” uwezo wetu ili Mungu aone. Kwa hivyo, ni kwa kufanya kazi kwa uaminifu tu kulingana na mipangilio ya kazi ndio tunaweza kujilinda.

Ee Mungu! Asante kwa kufunua asili yangu ya kiburi na majivuno. Kuanzia siku hii na kuendelea, hakika nitachukulia hili kama onyo na kuweka juhudi zaidi katika kujua asili yangu. Nitafanya kazi hasa kulingana na mipangilio ya kazi. Kwa kweli nitakuwa mtu mwenye mantiki, anayezingatia kanuni, na aliye na moyo wa uchaji Kwako.

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Kuona Uhalisi Wangu Kwa Dhahiri

Xiaoxiao Jijini Xuzhou, Mkoani Jiangsu Kwa sababu ya mahitaji ya kazi ya kanisa, nilihamishwa mpaka mahali pengine ili kutimiza wajibu...

Leave a Reply

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp