Kipindi 06, Ukweli Kuhusu Mateso ya Kikatili ya CCP Dhidi ya Wakristo: Damu na Machozi ya Wakristo Wazee—Mtu Mwenye Umri wa Miaka 79 Ateswa Hadi Kufa kwa Kushikilia Imani Yake
18/02/2026
Mwaka wa 2024 ulikuwa mwaka wa kwanza wa "Vita Vigumu vya Miaka Mitatu" vya CCP dhidi ya Kanisa la Mwenyezi Mungu. Tangu mwanzo wa mwaka, ukamataji wa Wakristo nchini kote uliendelea bila pumziko. Mnamo Mei 23, 2024, mamlaka katika Jiji la Bozhou, Mkoa wa Anhui, zilianzisha operesheni iliyoratibiwa ya kuwakamata watu. Qin Mei mwenye umri wa miaka 79 na Wakristo wengine 21 walikamatwa kutoka manyumbani mwao kwa sababu ya imani yao katika Mungu. Baada ya kufungwa jela safari hii, watu walio katika kizuizi walijaribu mara kwa mara kumlazimisha Qin Mei na wale wengine watie saini "Kauli Tatu" (dhamana, toba, na ukanaji) na waiache imani yao. Qin Mei na wale wengine hawakusalimu amri, na walipata adhabu ya mwili, wakilazimishwa kuketi kwenye ubao mgumu kwa saa 13 hadi 14 kwa siku. Walitakiwa kuketi wakiwa wamekunja miguu, mikono ikiwa magotini, na kuweka miili yao ikiwa imenyooka kabisa na kutulia. Meno ya bandia ya Qin Mei pia yalinyang'anywa, na kufanya iwe vigumu kwake kula. Adhabu hiyo ya mwili ya muda mrefu ilikuwa zaidi ya vile mwanamke huyo mzee na dhaifu angeweza kuvumilia. Siku 21 tu baadaye, Qin Mei aliteswa hadi kufa kizuizini, akauawa kama shahidi na CCP. Kwa kuongezea, Wakristo walionusurika waliachwa wakisumbuliwa na magonjwa kutokana na mateso ya CCP. Ripoti hii itaendelea kufichua ukweli wa mateso ya CCP dhidi ya Wakristo.