48 Maisha Ya Kanisa Ni Ya Kupendeza Sana

1

Mwenyezi Mungu mwenye mwili,

tunainua sauti yetu kukusifu.

Tumeinuliwa mbele ya kiti cha enzi kuhudhuria sherehe.

Maneno Yako yatuongoza kwa maisha mapya.

Tunaona ukweli ni wa thamani

katika kutenda kwetu maneno ya Mungu.

Ukweli unatuweka huru kutokana na minyororo yote,

roho zetu zinajawa na furaha.

Tunanyunyiziwa na maneno ya Mungu,

tunafurahia upendo Wake.

Tuko mbele za Mungu kila siku,

utamu ulioje mioyoni mwetu.

Tuna furaha kuishi maisha ya kanisa.

Tumebarikiwa sana kuwa na uwepo wa Mungu na uongozi.

Kwa kumpenda Mungu na kupata sifa Zake,

tunaishi maisha ya furaha zaidi.

Maisha ya kanisa ni ya kupendeza sana,

na Mungu asifiwa milele.

Maisha ya kanisa ni ya kupendeza sana,

na Mungu asifiwa milele.

2

Tumeheshimiwa kupata hukumu ya Mungu,

tumeona upotovu wetu wa kina.

Ingawa tunaumia, tunaona upendo wa Mungu ni halisi.

Tunaingia katika ukweli, tunaona baraka Zake.

Tunahukumiwa, tunapata ukweli, tunakuwa na maisha mapya.

Asili yetu ya kishetani inatupiliwa mbali,

tunakuwa watu wapya.

Ukweli watuletea shangwe na kutuweka huru.

Tunafurahi kuishi maisha ya kanisa.

Tumebarikiwa sana kuwa na uwepo wa Mungu na uongozi.

Kwa kumpenda Mungu na kupata sifa Zake,

tunaishi maisha ya furaha zaidi.

Maisha ya kanisa ni ya kupendeza sana,

na Mungu asifiwa milele.

Maisha ya kanisa ni ya kupendeza sana,

na Mungu asifiwa milele.

3

Ndugu wanapatana,

kuishi kwa amani kwa kufuata maneno ya Mungu.

Tunapendana na kusaidiana,

mioyo yetu inapiga pamoja kama mmoja.

Tunatenda ukweli, safi na wazi,

na kujaribu kuwa watu waaminifu.

Tuna uvumilivu na ustahimilivu,

tukijaa upendo, tunaishi kama wanadamu.

Ndugu, sako kwa bako,

tunafanya kazi na kuwa na ushuhuda kwa Mungu,

tunatoa yote yetu kueneza injili ya ufalme.

Tunatimiza wajibu wetu kuufurahisha, kuufurahisha moyo wa Mungu.

Hukumu ya Mungu ni baraka, inatutakasa.

Neno la Mungu ni ukweli, linakuwa uzima wetu.

Tunamwabudu Mungu kwa roho na kweli, tunaishi katika nuru.

Ufalme wa Kristo ni nyumba yetu nzuri.

Ufalme wa Kristo ni nyumba yetu nzuri.

Iliyotangulia: 47 Maisha ya Kanisa Huleta Furaha Kuu

Inayofuata: 49 Anga Hapa ni Samawati Sana

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp