3 Mwenyezi Mungu, wa Kwanza na wa Mwisho

1

Kutoka mashariki hadi magharibi, ulimwengu wote unamshangilia Mungu.

Jina tukufu, takatifu limeenea.

Ee, Mwenyezi Mungu amekuwa mwili sasa.

Ameupata ufalme na umekuja chini duniani.

Ameijenga Sayuni kwa mamlaka Yake yote;

Ameonekana kwa mataifa yote kwa utukufu.

Kwa sababu ya wokovu Wake watakatifu wote wanasifu na kuimba;

kwa sababu ya jina hili, wanafurahi daima.

Mwenyezi Mungu hutawala kama Mfalme (akivikwa uadhama),

Hunena kwa haki, huleta wokovu (kwa nguvu Zake).

Maneno ya Mungu yanashikilia mamlaka juu ya dunia yote,

na ufalme Wake hauwezi kamwe kutikiswa.

Mataifa yote yanakuja kumwabudu Mwenyezi Mungu!

Tunainua sauti zetu kushangilia na kuimba pamoja.

Mwenye Uweza, wa Kwanza na wa Mwisho,

viumbe walioumbwa wanamsifu milele.

2

Kutoka mahali jua hutokea mpaka linapotua,

utukufu wa Mungu huangaza katika dunia nzima.

Hatuna budi kumwimbia Mwenyezi Mungu nyimbo mpya.

Matendo makuu ya Mwenyezi Mungu ni ya ajabu kweli!

Maneno ya Mungu huwashinda wanadamu, Amewashinda maadui wote,

na kuwaokoa wale wote ambao Amewapangia kabla na kuwachagua,

Huwaongoza katika mbingu na dunia mpya.

Watu wote wameona sasa utukufu wa Mungu.

Jina takatifu la Mungu ni zuri jinsi gani ( duniani kote)!

Wanadamu wa dunia! Mshangilieni Mungu (kwa sauti za ushindi)!

Mungu ni mshindi, Akiwashinda maadui wote.

Mwimbie Mungu, sifu hekima na uweza Wake.

Mataifa yote yanakuja kumwabudu Mwenyezi Mungu!

Tunainua sauti zetu kushangilia na kuimba pamoja.

Mwenye Uweza, wa Kwanza na wa Mwisho,

viumbe walioumbwa wanamsifu milele.

Mungu amemshinda Shetani, amepata utukufu wote.

Amefanya kikundi cha washindi,

ambao ni washindi pamoja na Kristo.

Mwenyezi Mungu anastahili sifa na heshima.

Amefungua kitabu, amefungua mihuri saba.

Maneno Aliyonena yanaenea kote duniani.

Haki ya Mungu inaangaza kama nuru ya kung’aa,

na maneno Yake kama taa iwakayo.

Mataifa yote yanakuja kumwabudu Mwenyezi Mungu!

Tunainua sauti zetu kushangilia na kuimba pamoja.

Mwenye Uweza, wa Kwanza na wa Mwisho,

viumbe walioumbwa wanamsifu milele.

Iliyotangulia: 2 Mwana wa Adamu Ameonekana

Inayofuata: 4 Mwenyezi Mungu, Kristo wa Siku za Mwisho

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

418 Umuhumi wa Maombi

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato...

Mipangilio

  • Matini
  • Mada

Rangi imara

Mada

Fonti

Ukubwa wa Fonti

Nafasi ya Mstari

Nafasi ya Mstari

Upana wa ukurasa

Yaliyomo

Tafuta

  • Tafuta Katika Maneno Haya
  • Tafuta Katika Kitabu Hiki

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp