Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 471

05/10/2020

Kazi ya Mungu katika siku za mwisho inahitaji imani kubwa—inahitaji imani kubwa zaidi hata kuliko ile ya Ayubu. Bila imani, watu hawataweza kuendelea kupata mazoea na hawataweza kukamilishwa na Mungu. Siku itakapokuja ambapo majaribu makuu yanakuja, watu wengine wataondoka kutoka kanisa hili, na wengine wataondoka kutoka kanisa lile. Kutakuwa na wengine ambao walikuwa wakifanya vizuri kiasi katika kufuata kwao katika siku za awali na haiko wazi mbona hawaamini tena. Vitu vingi vitafanyika na hutajua ni nini kinaendelea, na Mungu Hataonyesha dalili zozote ama ishara, ama kufanya chochote kisicho cha kawaida. Hii ni kuona kama unaweza kusimama imara—Mungu Anatumia ukweli kuwasafisha watu. Bado hujateseka sana. Hapo baadaye majaribu makuu yajapo, katika sehemu zingine kila mtu katika kanisa ataondoka, na wale umesikizana nao vizuri sana wataondoka na kuiacha imani yao. Utaweza kusimama imara wakati huo? Sasa, yale majaribu umepitia yamekuwa madogo, na pengine imekuwa vigumu kuyahimili. Hatua hii inajumuisha usafishaji na kukamilishwa kupitia neno pekee. Katika hatua inayofuata, ukweli utakuja juu yako kukusafisha, halafu utakuwa katikati ya hatari. Inapokuwa kubwa sana, Mungu Atakushauri uharakishe na uondoke, na watu wa kidini watajaribu kukushawishi ujiunge. Hii ni ili kuona kama unaweza kuendelea katika njia hiyo. Haya yote ni majaribu. Majaribu ya sasa ni madogo, lakini siku itakuja ambapo kunao wazazi nyumbani ambao hawaamini tena na kunao watoto nyumbani ambao hawaamini tena. Je, utaweza kuendelea mbele? Unapoenda mbele zaidi, ndivyo majaribu yako yanakuwa mengi zaidi. Mtu Anatekeleza kazi Yake ya kuwasafisha watu kulingana na mahitaji yao na kimo chao. Katika hatua ya Mungu kuwakamilisha wanadamu, haiwezekani kuwa idadi ya watu itaendelea kukua—itapunguka tu. Ni kwa kupitia usafishaji huu tu ndipo watu wataweza kukamilishwa. Kushughulikiwa, kuadhibiwa, kujaribiwa, kuadibiwa, kulaaniwa—ndipo unaweza kustahimili haya yote? Unapoona kanisa lililo na hali nzuri hasa, ndugu na dada wote wanatafuta kwa nguvu kubwa, wewe mwenyewe unahisi umetiwa moyo. Siku ikija ambapo wote wameondoka, wengine wao hawaamini tena, wengine wameondoka kufanya biashara ama kuolewa, na wengine wamejiunga na dini, utaweza kusimama imara wakati huo? Je, utaweza kubaki bila mabadiliko ndani? Kukamilishwa kwa wanadamu kwa Mungu siyo jambo rahisi! Anatumia vitu vingi kuwasafisha watu. Watu wanaona haya kama mbinu, lakini kwa nia asili ya Mungu hizi sizo mbinu hata kidogo, ila ni ukweli. Mwishowe, Atakapokuwa Amewasafisha watu kufikia kiwango fulani na hawana malalamishi yoyote tena, hatua hii ya kazi Yake itakuwa imekamilika. Kazi kuu ya Roho Mtakatifu ni kukukamilisha, na wakati ambapo Hafanyi kazi na Anajificha, hata zaidi ni kwa sababu ya kukukamilisha, na hivi inaweza kuonekana hasa kama watu wana upendo kwa Mungu, na kama wana imani ya kweli Kwake. Mungu Anaponena wazi, hakuna haja ya wewe kutafuta; ni wakati tu ambapo Amejificha ndipo unahitaji kutafuta, unahitaji kuhisi njia yako hadi upite. Unapaswa kuweza kutimiza wajibu wa kiumbe aliyeumbwa, na haijalishi matokeo yako ya usoni na hatima yako inaweza kuwa ipi, unapaswa kuweza kufuatilia maarifa na upendo kwa Mungu katika miaka ambayo uko hai, na haijalishi jinsi Mungu anavyokutendea, unapaswa kuweza kuepuka kulalamika. Kuna sharti moja kwa kazi ya Roho Mtakatifu ndani ya watu. Bora wana hamu na wanatafuta na hawasitisiti ama kuwa na shaka kuhusu matendo ya Mungu, nao wanaweza kushikilia wajibu wao kila wakati, hivi tu ndivyo wanaweza kupata kazi ya Roho Mtakatifu. Katika kila hatua ya kazi ya Mungu, kinachohitajika kwa wanadamu ni imani kuu na kutafuta mbele za Mungu—kupitia tu kwa mazoea ndipo watu wataweza kugundua jinsi Mungu Anavyopendeka na jinsi Roho Mtakatifu Anavyofanya kazi ndani ya watu. Usipopata uzoefu, usipoihisi njia yako kupitia hayo, usipotafuta, hutapata chochote. Lazima uhisi njia yako kupitia mazoea yako, na kwa kupitia mazoea yako tu ndipo utaona matendo ya Mungu, na kugundua maajabu Yake na mambo Yake yasiyoeleweka.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp