Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 442

10/09/2020

Kumshuhudia Mungu hasa ni suala la kuzungumza kuhusu maarifa yako ya kazi ya Mungu, kuhusu jinsi Mungu huwashinda watu, kuhusu jinsi Yeye huwaokoa watu, kuhusu jinsi Yeye huwabadili watu; ni suala la kuzungumza kuhusu jinsi Yeye huwaongoza watu kuingia katika uhalisi wa ukweli, Akiwawezesha washindwe, wakamilishwe na kuokolewa na Yeye. Kushuhudia kunamaanisha kuzungumza kuhusu kazi Yake na yote ambayo umepitia. Ni kazi Yake pekee inayoweza kumwakilisha, na ni kazi Yake pekee inayoweza kumfichua kwa umma, kwa ukamilifu Wake; kazi Yake inamshuhudia. Kazi na matamshi Yake vinamwakilisha Roho moja kwa moja; kazi Anayofanya inatekelezwa na Roho, na maneno Anayonena yanazungumzwa na Roho. Vitu hivi vinaonyeshwa tu kupitia mwili wa Mungu, lakini kwa kweli, ni maonyesho ya Roho. Kazi yote Anayofanya na maneno yote Anayozungumza yanawakilisha kiini Chake. Ikiwa Mungu hangezungumza ama kufanya kazi baada ya kujivika mwili na kuja miongoni mwa wanadamu, na kisha Awatake mjue uhalisi Wake, ukawaida Wake na kudura Yake, je, ungeweza? Je, ungeweza kujua kiini cha Roho? Je, ungeweza kujua sifa za kiasili za mwili Wake ni zipi? Ni kwa sababu tu mmepitia kila hatua ya kazi Yake ndiyo Anawataka mumshuhudie. Ikiwa hamngekuwa na uzoefu kama huu, basi Hangesisitiza kwamba mumshuhudie. Kwa hivyo, unapomshuhudia Mungu, hushuhudii tu kuhusu sura Yake ya nje ya ubinadamu wa kawaida, lakini pia kazi Anayofanya na njia Anayoongoza; unapaswa kushuhudia kuhusu jinsi ulivyoshindwa na Yeye na umekamilishwa katika vipengele vipi. Unapaswa kuwa na ushuhuda wa aina hii. Ikiwa kila uendapo unasema kwa sauti kubwa: “Mungu wetu amekuja kufanya kazi, na kazi Yake kweli ni ya vitendo! Ametupata bila matendo yasiyo ya kawaida, bila miujiza na maajabu yoyote hata kidogo!” Wengine watauliza: “Unamaanisha nini unaposema kwamba Hafanyi miujiza na maajabu? Anawezaje kuwa Amekushinda bila kufanya miujiza na maajabu?” Na unasema: “Anazungumza na bila kuonyesha miujiza ama maajabu yoyote, Ametushinda. Kazi Yake imetushinda.” Hatimaye, ikiwa huwezi kusema chochote cha maana, ikiwa huwezi kuzungumzia mambo maalum, je, huu ni ushuhuda wa kweli? Mungu mwenye mwili anapowashinda watu, ni maneno Yake ya uungu yanayofanya hivyo. Ubinadamu hauwezi kutimiza hili; silo jambo ambalo mtu yeyote anaweza kutimiza, na hata wale wenye ubora wa juu zaidi wa tabia miongoni mwa watu wa kawaida hawawezi kutimiza hili, kwani uungu Wake ni wa juu zaidi kuliko kiumbe yeyote. Hili ni jambo la ajabu kwa watu; hata hivyo Muumba ni wa juu zaidi kuliko kiumbe yeyote. Viumbe hawawezi kuwa wa juu zaidi kuliko Muumba; ungekuwa wa juu zaidi kumliko, Hangeweza kukushinda, na Anaweza tu kukushinda kwa sababu Yeye ni wa juu zaidi kukuliko. Yeye anayeweza kuwashinda wanadamu wote ndiye Muumba, na hakuna mwingine ila Yeye anayeweza kufanya kazi hii. Maneno haya ni “ushuhuda”—aina ya ushuhuda ambayo unapaswa kuwa nayo. Umepitia kuadibiwa, hukumu, usafishaji, majaribu, vipingamizi na majaribio hatua kwa hatua, na umeshindwa; umeweka kando matarajio ya mwili, nia zako binafsi, na maslahi ya ndani ya mwili. Yaani, maneno ya Mungu yameushinda moyo wako kabisa. Ingawa hujakua katika maisha yako kwa kiwango Anachotaka, unayajua mambo haya yote na unashawishika kabisa na kile Anachofanya. Kwa hivyo, hili linaweza kuitwa ushuhuda, ushuhuda ambao ni halisi na wa kweli. Kazi ambayo Mungu amekuja kufanya, kazi ya hukumu na kuadibu, inakusudiwa kumshinda mwanadamu, lakini pia Anahitimisha kazi Yake, akimaliza enzi na kutekeleza kazi ya hitimisho. Anakamilisha enzi nzima, Akiwaokoa wanadamu wote, Akiwakomboa wanadamu kutoka katika dhambi kabisa; Anawapata wanadamu Aliowaomba kikamilifu. Unapaswa kushuhudia haya yote. Umepitia kazi nyingi sana ya Mungu, umeiona kwa macho yako mwenyewe na kuipitia wewe binafsi; wakati umefika mwisho kabisa, ni lazima uweze kutenda kazi inayokupasa uifanye. Litakuwa jambo la kusikitisha kweli usipoweza! Katika siku zijazo, wakati injili inaenezwa, unapaswa kuweza kuzungumzia maarifa yako mwenyewe, ushuhudie yote uliyoyapata moyoni mwako na utumie jitihada yote. Kiumbe aliyeumbwa anapaswa kufanikisha hili. Umuhimu wa kweli wa hatua hii ya kazi ya Mungu ni upi? Athari yake ni ipi? Na ni kiwango chake kipi kinatekelezwa ndani ya mwanadamu? Watu wanapaswa kufanya nini? Unapoweza kuzungumza kwa uwazi kuhusu kazi yote ambayo Mungu mwenye mwili amefanya tangu aje duniani, basi ushuhuda wako utakuwa kamili. Unapoweza kuzungumza kwa uwazi kuhusu vitu hivi vitano: umuhimu wa kazi Yake; maudhui yake; kiini chake; tabia inayowakilisha; na kanuni zake, basi hili litathibitisha kwamba unaweza kumshuhudia Mungu, kwamba kweli una maarifa. Mahitaji yangu kwenu si ya juu sana, na yanaweza kutimizwa na wale wote wanaofuatilia kwa kweli. Ikiwa umeazimia kuwa mmoja wa mashahidi wa Mungu, ni lazima uelewe kile Mungu anachochukia sana na kile Mungu Anachopenda. Umepitia kazi Yake nyingi; kupitia kazi hii, ni lazima upate kujua tabia Yake, uelewe mapenzi Yake na mahitaji Yake kwa wanadamu, na utumie maarifa haya kumshuhudia na kutenda wajibu wako. Unaweza tu kusema: “Tunamjua Mungu. Hukumu na kuadibu Kwake havina huruma hata kidogo. Maneno Yake ni makali sana; ni ya haki na uadhama, na hayawezi kukosewa na mtu yeyote,” lakini maneno haya humkimu mwanadamu hatimaye? Yana athari gani kwa watu? Kweli unajua kwamba kazi hii ya hukumu na kuadibu ni ya manufaa zaidi kwako? Hukumu na kuadibu kwa Mungu vinafichua uasi na upotovu wako, sivyo? Vinaweza kutakasa na kuondoa vile vitu vichafu na vipotovu vilimo ndani yako, sivyo? Kusingekuwa na hukumu na kuadibu, hatima yako ingekuwa ipi? Kweli unafahamu kwamba Shetani amekupotosha kwa kiwango cha juu zaidi? Leo, mnapaswa kujitayarisha kwa vitu hivi na mvijue vyema.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Utendaji (7)

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp