Wimbo wa Kikristo | Matatizo Yote Yanaweza Kutatuliwa kwa Kufuatilia Ukweli

21/06/2020

Sasa kuufuata ukweli tu ndilo jambo la busara,

ni ufahamu tu wa asili yako potovu ndilo jambo la busara,

ni uwezo tu wa kumridhisha Mungu ndilo la busara.

Kuingia katika uhalisi wa ukweli

na kuishi kwa kudhihirisha mfano wa mtu halisi— huu ni uhalisi.

Uhalisi ni kumpenda Mungu, kumtii Mungu, na kumshuhudia Mungu.

Haya ndiyo matokeo ambayo Mungu anataka.

Uchunguzi wa mambo hayo yote ambayo huwezi kugusa wala kuona ni kupoteza muda.

Hayana uhusiano wowote na uhalisi,

na pia hayana uhusiano wowote na matokeo ya kazi ya Mungu.

Mtazamo wa mtu mwerevu kweli unafaa kuwa:

Sijali kile ambacho Mungu anafanya, au jinsi Mungu ananitendea mimi;

sijali nimepotoka kwa kina kiasi gani, au ubinadamu wangu ni wa jinsi gani;

sitayumbayumba katika kufuata kwangu kwa ukweli

na kufuata kwangu katika kumjua Mungu.

Ni kwa kumjua Mungu tu ndiyo mtu anaweza kutatua tabia yake potovu

na kutimiza wajibu wake kuridhisha mapenzi ya Mungu;

huu ni mwelekeo wa maisha,

hili ndilo ambalo mwanadamu anapaswa kutamani kufikia,

hii ndiyo njia pekee ya wokovu,

hii ndiyo njia pekee ya wokovu.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp