Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 61

21/06/2020

Taratibu za Enzi ya Sheria

Amri Kumi

Kanuni za Kujenga Madhabahu

Taratibu za Ushughulikiaji wa Watumishi

Taratibu za Wizi na Fidia

Kutimiza Mwaka wa Sabato na Karamu Tatu

Taratibu za Siku ya Sabato

Taratibu za Kutoa Sadaka

Sadaka zilizoteketezwa

Sadaka za Unga

Sadaka za Amani

Sadaka za Dhambi

Sadaka za Hatia

Taratibu za Sadaka za Kuhani (Aroni na Watoto Wake wa Kiume Waamrishwa Kutii)

Sadaka za Kuteketezwa na Kuhani

Sadaka za Unga na Kuhani

Sadaka za Dhambi na Kuhani

Sadaka za Hatia na Kuhani

Sadaka za Amani na Kuhani

Taratibu za Ulaji wa Sadaka na Kuhani

Wanyama Walio Halali na Wale Walio Haramu (Wale Wanaoweza na Wasioweza Kuliwa)

Taratibu za Utakasaji Wanawake Baada ya Kujifungua

Viwango vya Uchunguzi wa Ukoma

Taratibu kwa Wale Ambao Wameponywa Ukoma

Taratibu za Kuzitakasa Nyumba Zilizoambukizwa

Taratibu za Wale Wanaougua Kisonono Kisicho cha Kawaida

Siku ya Upatanisho Wa Mungu na Binadamu Ambayo Lazima Iadhimishwe Mara Moja Kwa Mwaka

Sheria za Kuchinja Ng’ombe na Mbuzi

Kuzuiliwa kwa Mazoea Yafuatayo Yanayochukiza Ya Watu wa Mataifa (Si Kutenda Kujamiiana Kwa Maharimu, na Kadhalika)

Taratibu Ambazo Lazima Zifuatwe na Watu (“Mtakuwa watakatifu: kwani Mimi Yehova Mungu wenu ni mtakatifu” (Walawi 19:2))

Kutendewa kwa Wale Wanaotoa Kafara Watoto Wao kwa Molka

Taratibu za Adhabu ya Uhalifu wa Uasherati

Sheria Zinazofaa Kufuatiliwa na Kuhani (Sheria za Tabia Yao Ya Kila Siku, Sheria za Matumizi ya Mambo matakatifu, Sheria za Kutoa Sadaka na Kadhalika)

Karamu Zinazofaa Kufuatiliwa (siku ya Sabato, Pentekoste, Siku ya Upatanisho wa Mungu na Binadamu kwa Maisha ya Kifo cha Yesu, na Kadhalika)

Taratibu Nyingine (Kuteketezwa kwa Taa, Mwaka wa Jubilii, Ukombozi wa Ardhi, Ulaji wa Viapo, Utoaji wa Zaka, na Kadhalika)

Taratibu za Enzi ya Sheria ni Thibitisho la Kweli la Maelekezo ya Mungu kwa Wanadamu Wote

Hivyo, mmezisoma taratibu na kanuni hizi za Enzi ya Sheria, kweli? Je, taratibu hizi zinajumuisha mseto mpana? Kwanza, zinajumuisha Amri Kumi, na baadaye kuna taratibu za namna ya kujenga madhabahu, na kadhalika. Hizi zinafuatwa na taratibu za kuitimiza Sabato na kuzidumisha zile karamu tatu, na baadaye kuna taratibu za kutoa sadaka. Je, mnaona ni aina ngapi za sadaka ambazo zimo? Kunazo sadaka zilizoteketezwa, sadaka za unga, sadaka za amani, sadaka za dhambi, na kadhalika, ambazo zinafuatwa na taratibu za sadaka za kuhani, zikiwemo sadaka zilizoteketezwa na sadaka za unga zilizotolewa na Kuhani, na aina nyingine za sadaka. Taratibu za nane ni za ulaji wa sadaka na Kuhani, na kisha kunazo taratibu zinazofaa kudumishwa wakati wa maisha ya watu. Kunayo masharti ya vipengele vingi vya maisha ya watu, kama vile taratibu zinazotawala kile wanachoweza au wasichoweza kula, kwa utakasaji wa wanawake baada ya wao kujifungua, na kwa wale ambao wameponywa ugonjwa wa ukoma. Katika taratibu hizi, Mungu Anafikia hadi kiwango cha kuzungumzia kuhusu ugonjwa, na kunazo hata sheria za kuchinja kondoo na ng’ombe, na kadhalika. Kondoo na ng’ombe waliumbwa na Mungu, na unafaa kuwachinja hata hivyo Mungu anakuambia kufanya hivyo; kunayo, bila shaka, sababu ya maneno ya Mungu, na ni sahihi bila shaka kutenda kama inavyokaririwa na Mungu, na kwa hakika itakuwa ya manufaa kwa watu! Kunazo pia karamu na sheria za kufuatwa, kama vile siku ya Sabato, Pasaka, na zaidi—Mungu aliweza kuzungumzia yote haya. Hebu tuangalie zile za mwisho: taratibu nyingine—kuteketezwa kwa taa, mwaka wa Jubilii, ukombozi wa ardhi, ulaji wa viapo, utoaji wa zaka, na kadhalika. Je, hizi zinajumuisha mseto mpana? Kitu cha kwanza cha kuzungumziwa ni suala la sadaka la watu, kisha kunazo taratibu za wizi na fidia, na udumishaji wa siku ya Sabato…; kila mojawapo ya maelezo ya maisha yanahusishwa. Hivi ni kusema, wakati Mungu alianza kazi Yake rasmi ya mpango Wake wa usimamizi, Aliweka wazi taratibu nyingi ambazo zilifaa kufuatwa na binadamu. Taratibu hizi zilikuwa ili kumruhusu binadamu kuishi maisha ya kawaida ya binadamu hapa duniani, maisha ya kawaida ya binadamu ambayo hayajatenganishwa na Mungu na uongozi Wake. Mungu alimwambia binadamu kwanza namna ya kuunda madhabahu, namna ya kuyaunda madhabahu. Baada ya hapo, Alimwambia binadamu namna ya kutoa sadaka, na kuamuru namna ambavyo binadamu alifaa kuishi—kile alichofaa kutilia maanani katika maisha, kile alichofaa kutii, kile anachofaa na hafai kufanya. Kile Mungu alichoweka wazi kwa binadamu kilikuwa kinakubalika chote, na pamoja na tamaduni, taratibu, na kanuni hizi Aliwastanisha tabia ya watu, kuongoza maisha yao, kuongoza uanzishaji wao wa sheria za Mungu, kuwaongoza kuja mbele ya madhabahu ya Mungu, kuwaongoza katika kuishi maisha miongoni mwa mambo mengine yote ambayo Mungu alikuwa amemuumbia binadamu na yaliyomilikiwa na mpangilio na marudio ya mara kwa mara na ya kiasi. Kwanza Mungu alitumia taratibu na kanuni hizi rahisi kuweka vipimo kwa binadamu, ili hapa duniani binadamu aweze kuwa na maisha ya kawaida ya kumwabudu Mungu, aweze kuwa na maisha ya kawaida; hivi ndivyo yalivyo maudhui mahususi ya mwanzo wa mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita. Taratibu na sheria zinajumuisha maudhui mapana mno, yote ni maelezo ya mwongozo wa Mungu wa mwanadamu wakati wa Enzi ya Sheria, lazima yangekubaliwa na kuheshimiwa na watu waliokuwa wamekuja kabla ya Enzi ya Sheria, ni rekodi ya kazi iliyofanywa na Mungu katika Enzi ya Sheria, na ni ithibati ya kweli ya uongozi na mwongozo wa Mungu kwa wanadamu wote.

Wanadamu Hawatenganishwi Milele na Mafundisho na Matoleo ya Mungu

Katika taratibu hizi tunaona kwamba mwelekeo wa Mungu katika kazi Yake, katika usimamizi Wake, na kwa wanadamu ukiwa wa kumakinikia zaidi, wa ukweli, wa bidii, na wa kuwajibika. Anaifanya kazi ambayo lazima Afanye miongoni mwa wanadamu kulingana na hatua Zake, bila ya hitilafu hata kidogo, Akiongea maneno ambayo lazima aongee kwa wanadamu bila ya kosa au upungufu hata kidogo, Akimruhusu binadamu kuona kwamba hawezi kutenganishwa na uongozi wa Mungu, na Akimwonyesha namna ambavyo yale yote ambayo Mungu anafanya na kusema yalivyo muhimu kwa wanadamu. Licha ya kile ambacho binadamu alivyo katika enzi ijayo, kwa ufupi, wakati wa mwanzo kabisa—wakati wa Enzi ya Sheria—Mungu alifanya mambo haya rahisi. Kwa Mungu, dhana za watu kumhusu Mungu, ulimwengu na mwanadamu katika enzi hiyo zilikuwa za kidhahania na zisizoeleweka, na ingawaje walikuwa na fikra na nia fulani husika, zote zilikuwa hazina uwazi na si sahihi, na hivyo wanadamu walikuwa hawawezi kutenganishwa kutoka kwa mafundisho na matoleo ya Mungu kwao. Wanadamu wa mapema zaidi hawakujua chochote, na hivyo Mungu alilazimika kuanza kumfunza binadamu kutoka kwenye kanuni za juujuu na za kimsingi zaidi kwa minajili ya uwepo na taratibu zinazohitajika za kuishi, kutia moyoni mambo haya yote kwenye moyo wa binadamu kidogo kidogo, na kumpa binadamu uelewa wa Mungu kwa utaratibu, kutambua na kuelewa uongozi wa Mungu kwa utaratibu, na dhana ya kimsingi ya uhusiano kati ya binadamu na Mungu, kupitia kwa taratibu hizi na kupitia kwa sheria hizi, ambazo zilikuwa za maneno. Baada ya kutimiza athari hii, ndipo tu Mungu aliweza, kidogo kidogo, kufanya kazi ambayo Angeweza kufanya baadaye, na hivyo taratibu hizi na kazi iliyofanywa na Mungu kwenye Enzi ya Sheria zikawa ndiyo msingi wa kazi Yake ya kuwaokoa wanadamu na hatua ya kwanza ya kazi katika mpango wa usimamizi wa Mungu. Ingawaje, kabla ya kazi ya Enzi ya Sheria, Mungu alikuwa ameongea naye Adamu, Hawa, na babu zao, amri na mafunzo hayo hayakuwa ya hatua kwa hatua sana au mahususi ili kutolewa moja baada ya nyingine kwa mwanadamu, na hayakuwa yameandikwa, wala hayakuwa taratibu. Hii ni kwa sababu, kwa wakati huo, mpango wa Mungu haukuwa umeenda mbali kiasi hicho; na Mungu alipokuwa amemwongoza binadamu hadi katika hatua hii tu ndipo Alipoweza kuongea taratibu hizi za Enzi ya Sheria, na kuanza kumfanya binadamu kuzitekeleza. Ulikuwa ni mchakato unaohitajika, na matokeo yasingeweza kuepukika. Tamaduni na taratibu hizi rahisi zinaonyesha binadamu hatua za usimamizi wa kazi ya Mungu na hekima ya Mungu inayofichuliwa katika mpango Wake wa usimamizi. Mungu anayajua maudhui yapi na mbinu zipi za kutumia ili kuanza, mbinu zipi za kutumia kuendelea na mbinu zipi za kutumia kumaliza ili aweze kupata kundi la watu lililo na ushuhuda Kwake Yeye, Aweze kupata kundi la watu walio na akili sawa na Yake. Anajua kile kilicho ndani ya binadamu, na kujua kile kinachokosa kwa binadamu, Anajua kile anachofaa kutoa, na namna Anavyofaa kumwongoza binadamu, na pia ndivyo Anavyojua kile binadamu anafaa na hafai kufanya. Binadamu ni kama kikaragosi: Ingawaje hakuwa na uelewa wowote wa mapenzi ya Mungu, alilazimika kuongozwa na kazi ya Mungu ya usimamizi, hatua kwa hatua hadi leo. Hakukuwa na kutodhihirika kokote katika moyo wa Mungu kuhusu kile Alichofaa kufanya; katika moyo Wake kulikuwa na mpango wazi na kamilifu kabisa, na Alitekeleza kazi hiyo ambayo Yeye mwenyewe alitaka kufanya kulingana na hatua Zake na mpango Wake, Akiendelea mbele kutoka katika hali ya juujuu hadi ile hali ya ndani kabisa. Ingawaje Hakuwa ameonyesha kazi ambayo Alifaa kufanya baadaye, kazi Yake ya baadaye bado iliendelea kutekelezwa na kuendelea mbele kulingana kabisa na mpango Wake, ambayo ni maonyesho ya kile Mungu anacho na alicho, na pia ni mamlaka ya Mungu. Licha ya ni awamu gani ya mpango Wake wa usimamizi ambayo Anafanya, tabia Yake na kiini chake kinamwakilisha Yeye mwenyewe—na hakuna kosa katika haya. Licha ya enzi, au awamu ya kazi, aina ya watu ambao Mungu anapenda, aina ya watu ambao Anachukia, tabia Yake, na chote ambacho Anacho na alicho hakitawahi kubadilika. Ingawaje taratibu na kanuni hizi ambazo Mungu alianzisha katika kazi ya Enzi ya Sheria zinaonekana rahisi na za juujuu kwa watu wa leo, na Ingawaje ni rahisi kuelewa na kutimiza, ndani ya hizo kunayo bado hekima ya Mungu, na kunayo bado tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho. Kwani ndani ya taratibu hizi zinazoonekana rahisi, uwajibikaji na utunzaji wa Mungu kwa wanadamu unaonyeshwa, na kiini kizuri cha fikira zake, kumruhusu binadamu kutambua kwa kweli ukweli kwamba Mungu anatawala mambo yote na mambo yote yanadhibitiwa kwa mkono Wake. Haijalishi ni kiwango kipi cha maarifa ambacho wanadamu watajifunza au nadhari au mafumbo mangapi wanaelewa, kwa Mungu hakuna chochote kati ya hivi ambavyo vinaweza kusawazisha toleo Lake kwa, na uongozi wa wanadamu; wanadamu milele hawatatenganishwa na mwongozo wa Mungu na kazi ya kibinafsi ya Mungu. Huu ndiyo uhusiano kati ya binadamu na Mungu usiotenganishwa. Licha ya kama Mungu anakupa amri, au taratibu, au Anakupa ukweli ili kuyaelewa mapenzi Yake, haijalishi ni nini Anachofanya, nia ya Mungu ni kumwongoza binadamu hadi katika siku nzuri ya kesho. Maneno yaliyotamkwa na Mungu na kazi Anayofanya ni ufunuo wa kipengele kimoja cha kiini Chake na vilevile ni ufunuo wa kipengele kimoja cha tabia Yake na hekima Yake, zote hizi ni hatua zisizozuilika katika mpango Wake wa usimamizi. Hili halifai kupuuzwa! Mapenzi ya Mungu yamo katika chochote Anachofanya; Mungu haogopi maoni yasiyo mahali pake wala haogopi dhana au fikira zozote za binadamu kuhusu Yeye. Yeye hufanya kazi Yake tu, na kuendeleza usimamizi Wake, kulingana na mpango Wake wa usimamizi, usiozuiliwa na mtu yeyote, suala lolote au kifaa chochote.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp