Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 345

12/10/2020

Ingawa nyinyi vijana wote ni kama simba wachanga, kwa nadra mnakuwa na njia ya kweli mioyoni mwenu. Ujana wenu hauwezi kuwapa nafasi ya kupata kazi Yangu zaidi; kinyume na hilo, daima nyinyi husababisha chuki Yangu kwenu. Ingawa nyinyi ni wachanga, ama mnakosa uhai au hamna tamaa ya makuu, daima nyinyi hamjihusishi na siku zenu zijazo; ni kana kwamba hamjali, na pia mnawaza sana. Ingeweza kusemwa kuwa uchangamfu, maadili, na msimamo yanayochukuliwa ambayo yanapaswa kupatikana kwa vijana hayawezi kabisa kupatikana kwenu; nyinyi, vijana wa aina hii, mnakosa msimamo na hamna uwezo wa kutofautisha kati ya sahihi na isiyo sahihi, mema na maovu, mazuri na mabaya. Haiwezekani kupata dalili zozote zenu ambazo ni mpya. Nyinyi karibu mmepitwa na wakati kabisa, na nyinyi, vijana wa aina hii, pia mmejifunza kukubali tu, kuwa bila mantiki. Hamwezi kamwe kutofautisha kwa dhahiri mazuri kutoka kwa mabaya, hamwezi kutofautisha kati ya ukweli na uongo katika masuala, kamwe hamjitahidi kupata ubora, wala hamwezi kusema nini ni sahihi na nini si sahihi, nini ni ukweli, na nini ni unafiki. Ndani yenu kunabakia mipulizo ya ghafla ya dini hata zaidi na hata mikubwa zaidi kuliko kwa watu wazee. Nyinyi hata ni wenye kiburi na msio na busara, nyinyi ni wa ushindani, na kupenda kwenu uchokozi ni mzito sana—kijana wa aina hii anawezaje kumiliki ukweli? Mtu asiyeweza kuchukua msimamo anawezaje kushuhudia? Mtu asiye na uwezo wa kutofautisha kati ya yaliyo sahihi na yasiyo sahihi anawezaje kuitwa kijana? Mtu asiye na uhai, nguvu, utulivu, ubichi, utulivu na udhabiti wa kijana anawezaje kuitwa mfuasi Wangu? Mtu asiye na ukweli wowote wala hisia ya haki, lakini hupenda kucheza na kupigana anawezaje kufaa kuwa shahidi Wangu? Macho ambayo yamejaa uongo na chuki bila sababu kwa watu siyo wanayopaswa kuwa nayo vijana, na wale wanaotekeleza vitendo vya uharibifu, vinavyochukiza mno hawapaswi kuwa vijana. Hawapaswi kuwa bila maadili, matarajio, au tabia ya maendeleo ya shauku; hawapaswi kuvunjika moyo juu ya matarajio yao wala hawapaswi kupoteza matumaini maishani au kupoteza imani katika siku zijazo; wanapaswa kuwa na uvumilivu kuendelea na njia ya ukweli ambayo sasa wamechagua kufanikisha matamanio yao ya kutumia maisha yao yote kwa ajili Yangu; hawapaswi kuwa bila ukweli, wala kuficha unafiki na udhalimu, bali wanapaswa kusimama imara katika msimamo unaofaa. Hawapaswi tu kuzurura, bali wanapaswa kuwa na roho ya kuthubutu kujitolea mhanga na kujitahidi kwa ajili ya haki na ukweli. Vijana wanapaswa kuwa na ujasiri wa kutoshindwa na ukandamizaji wa nguvu za giza na kubadili umuhimu wa uwepo wao. Vijana hawapaswi kukubali shida bila kulalamika, bali wanapaswa wawe wazi na wa kusema bila kuficha, na roho ya msamaha kwa ndugu wao. Bila shaka haya ni mahitaji Yangu ya kila mtu pamoja na ushauri Wangu kwa kila mtu. Hata zaidi, ni maneno Yangu ya kutuliza kwa vijana wote. Mnapaswa kutenda kulingana na maneno Yangu. Hasa vijana hawapaswi kuwa bila azimio la utambuzi katika masuala, na la kutafuta haki na ukweli. Yale mnayopaswa kufuata ni mambo yote mazuri na mema, na mnapaswa kupata uhalisi wa mambo yote mazuri, na pia kuwajibika juu yaa maisha yenu—hampaswi kuyachukulia kwa wepesi. Watu huja duniani na ni nadra kupatana na Mimi, na pia ni nadra kuwa na fursa ya kutafuta na kupata ukweli. Kwa nini msithamini wakati huu mzuri kama njia sahihi ya kutafuta katika maisha haya? Na ni kwa nini daima nyinyi hupuuza sana ukweli na haki? Kwa nini daima nyinyi hujikanyaga na kujiangamiza kwa ajili ya ule udhalimu na uchafu ambao huchezea watu? Na kwa nini mnajishughulisha na kile ambacho wadhalimu hufanya kama watu wazee? Kwa nini mnaiga njia za zamani za mambo ya kale? Maisha yenu yanapaswa kujaa haki, ukweli, na utakatifu; maisha yenu hayapaswi kupotoshwa katika umri mdogo hivyo, yakiwasababisha kuanguka kuzimuni. Je, hamhisi kwamba hili ni la kusikitisha sana? Je, hamhisi kwamba hili silo haki kwenu sana?

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp