Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 451

27/09/2020

Katika mkondo wa sasa, kila mtu anayempenda Mungu kwa kweli ana fursa ya kukamilishwa na Yeye. Bila kujali kama yeye ni kijana au mzee, mradi tu anatazamia kwa hamu kumtii Mungu na kumheshimu Yeye, wataweza kukamilishwa na Yeye. Mungu huwakamilisha watu kulingana na kazi zao tofauti. Mradi tu umefanya yote kwa nguvu yako na kuitii kazi ya Mungu utakuwa na uwezo wa kukamilishwa na Yeye. Kwa sasa hakuna hata mmoja wenu aliye mkamilifu. Wakati mwingine mnaweza kutekeleza aina moja ya kazi na wakati mwingine mnaweza kutekeleza mbili; mradi tu mnatoa nguvu zenu zote kujitumia kwa ajili ya Mungu, hatimaye mtafanywa wakamilifu na Mungu.

Vijana wana falsafa chache za maisha, na hawana hekima na ufahamu. Mungu amekuja hapa kukamilisha hekima na ufahamu wa mwanadamu, na neno la Mungu huyafidia mambo haya ambayo hawana. Hata hivyo, tabia za vijana si thabiti na hii inahitaji mbadiliko na Mungu. Vijana wana mawazo machache ya kidini na falsafa chache za maisha Wanafikiri kwa maneno rahisi, na fikira zao sio ngumu kufahamika. Hiki ni kipengele ambacho ubinadamu wao bado haujachukua umbo na ni kipengele cha kupendeza, lakini vijana hawajui na hawana hekima, na hii ni sehemu ambayo inahitaji kukamilishwa na Mungu. Kupitia kukamilishwa na Mungu, mnaweza kukuza utambuzi na kuweza kuelewa mambo mengi ya kiroho, na hatua kwa hatua mgeuke kuwa watu wanaostahili kutumiwa na Mungu. Ndugu na dada wakubwa pia wanaweza kutekeleza kazi fulani na hawajaachwa na Mungu. Na ndugu na dada wakubwa, wao pia wana mambo yanayofaa na baadhi ya mambo yasiyofaa. Ndugu na dada wakubwa wana falsafa zaidi za maisha, wana mawazo zaidi ya kidini, vitendo vyao vimekwama katika mfumo usiopindika, hufuata sheria kama roboti, wao huvitumia bila kufikiri, na hawawezi kubadilika. Hiki sicho kipengele kinachofaa. Hata hivyo, ndugu na dada wakubwa ni watulivu na wenye kijidhibiti nafsi kuelekea chochote kinachojitokeza; tabia zao ni imara, na hawana hisia kali zisizoweza kutabiriwa. Wanaweza kuwa wapole katika kukubali mambo, lakini hii siyo kasoro kubwa. Mradi mnaweza kutii; mradi mnaweza kuyakubali maneno ya sasa ya Mungu, ikiwa hamchunguzi maneno ya Mungu, ikiwa hamsiti kutii na kufuata, ikiwa hakika hutoi hukumu au kuwa na mawazo mengine mabaya, na ikiwa mnakubali maneno Yake na kuyaweka katika matendo—ikiwa mnakidhi hali hizi—mtaweza kukamilishwa.

Bila kujali kama ninyi ni ndugu au dada wadogo au wakubwa, mnajua kazi mnayopaswa kutekeleza. Wale walio katika ujana wao sio wenye kiburi; wale walio wakubwa zaidi sio wasioonyesha hisia na hawarudi nyuma. Nao wanaweza kutumia nguvu za kila mmoja kufidia upungufu wao, na wanaweza kuhudumiana bila ubaguzi wowote. Daraja la urafiki linajengwa kati ya ndugu na dada wadogo na wakubwa. Kwa sababu ya upendo wa Mungu mnaweza kuelewana vizuri zaidi. Ndugu wadogo hawawadharau ndugu wakubwa, na ndugu wakubwa sio wa kujidai. Je! Huu si ushirikiano patanifu? Ikiwa ninyi nyote mna uamuzi huu, basi mapenzi ya Mungu hakika yatatimizwa katika kizazi chenu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp