Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 400

03/09/2020

Mungu Anajibidiisha kumfanya binadamu kuwa kamili. Haijalishi ni mtazamo gani anaoongelea Yeye, yote ni kwa minajili ya kuwafanya watu hawa kuwa watimilifu. Maneno yaliyotamkwa kutoka kwenye mtazamo wa Roho ni magumu kwa binadamu kuelewa, na binadamu hawezi kupata njia ya kufanyia mazoezi, kwani binadamu ana uwezo finyu wa kupokea. Kazi ya Mungu hutimiza athari tofauti, na kila hatua ya kazi hiyo ina kusudio Lake. Aidha, lazima Aongee kutoka mitazamo tofauti ili kumfanya binadamu kuwa mtimilifu. Kama Angetoa sauti Yake kutoka kwenye mtazamo wa Roho pekee, awamu hii ya kazi ya Mungu isingeweza kukamilishwa. Kutokana na mkazo wa sauti Yake, unaweza kuona Anayo bidii ya kufanya kundi hili la watu kamilifu. Kama mmoja anayependa kufanywa kuwa mtimilifu na Mungu, ni hatua gani ya kwanza ambayo lazima uchukue? Lazima kwanza ujue kazi ya Mungu. Huku mbinu mpya zikitumika na enzi ikiwa imebadilika kutoka moja hadi nyingine, mbinu ambazo Mungu hufanyia kazi pia zimebadilika, sawa tu na njia ambazo Mungu huongelea. Sasa, si mbinu tu za kazi Yake zilizobadilika, lakini pia enzi yenyewe. Awali ilikuwa ni Enzi ya Ufalme, awamu ya kazi ambamo ulistahili kumpenda Mungu. Sasa, ni Enzi ya Ufalme wa Milenia—Enzi ya Neno—yaani, enzi ambamo Mungu hutumia njia nyingi za kuongea ili kumfanya binadamu kuwa mtimilifu na Huongea kutoka kwa mitazamo tofauti ili kumruzuku binadamu. Punde tu nyakati zilipopita hadi katika Enzi ya Ufalme wa Milenia, Mungu alianza kutumia neno ili kumfanya binadamu kuwa mtimilifu, kumwezesha binadamu kuingia katika uhalisia wa maisha na kumwongoza binadamu hadi kwenye njia sahihi. Binadamu amepitia hatua nyingi sana za kazi Yake na ameona kwamba kazi ya Mungu haibakii vilevile. Badala yake, inabadilika kila mara na kuwa yenye kina. Baada ya muda mrefu sana wa uzoefu, kazi imegeuka na kubadilika tena na tena, lakini kwa mabadiliko yoyote yale, haijawahi kutoka kwa lengo la Mungu la kumfinyanga binadamu. Hata kupitia mabadiliko elfu kumi, kusudio lake asilia halibadiliki kamwe, na haliondoki kamwe kutoka kwenye ukweli au uzima. Mabadiliko kwenye mbinu ambazo kazi inafanywa ni mabadiliko tu katika mpangilio wa kazi na mtazamo wa kuongea, na wala si badiliko kwenye lengo kuu la kazi Yake. Mabadiliko katika mkazo wa sauti na mbinu za kufanya kazi yanafanywa ili kutimiza athari fulani. Mabadiliko katika mkazo wa sauti hayamaanishi mabadiliko katika kusudio au kanuni ya kazi. Kiini halisi cha binadamu kusadiki Mungu ni kutafuta uzima. Kama unasadiki Mungu lakini hutafuti uzima au ukweli au maarifa ya Mungu, basi hakuna kusadiki Mungu kokote! Je, ni jambo la kihalisia kwamba ungali unatafuta kuingia kwenye ufalme kuwa mfalme? Mafanikio tu ya upendo wa kweli kwa Mungu kupitia kwa utafutaji wa uzima ndilo jambo la kihalisia; ufuatiliaji na utendaji wa ukweli vyote ni vya kihalisia. Pitia maneno ya Mungu wakati ukisoma maneno Yake; kwa njia hii utaweza kung’amua maarifa ya Mungu kupitia kwa uzoefu halisi. Huu ni ufuatiliaji wa kweli.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Enzi ya Ufalme Ni Enzi ya Neno

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp