Wimbo wa Injili | Maneno Ya Mungu Ni Ukweli Usiobadilika Milele

31/03/2020

Maneno ya Mungu ndiyo ukweli usiobadilika milele.

Mungu Ndiye msambazaji wa binadamu na kiongozi wa pekee wa mwanadamu.

Thamani na maana ya maneno ya Mungu

haibainishwi na kama yanakubaliwa au kutambuliwa na mwanadamu,

ila ni kwa kiini cha maneno yenyewe.

Hata kama hakuna mtu hata mmoja duniani anaweza kupokea maneno ya Mungu,

thamani ya maneno Yake na usaidizi wake kwa mwanadamu

hayapimiki na mwanadamu yeyote.

Kwa hivyo, Ninapokumbwa na wanadamu wengi wanaoasi, kukataa

au kudharau kabisa maneno ya Mungu,

msimamo Wake ni huu tu:

Wacha wakati na ukweli uwe ushahidi wa Mungu

na uonyeshe kuwa maneno Yake ndiyo ukweli, njia na uhai.

Wacha vionyeshe kuwa yote Aliyoyasema ni ya ukweli,

na kuwa ni yale ambayo mwanadamu lazima apewe,

na, zaidi ya yote, yale ambayo mwanadamu anafaa akubali.

Nitawaruhusu wote wanaomfuata wajue ukweli huu:

Wote wasioyakubali maneno Yake kikamilifu,

wale wasioyaweka maneno Yake katika vitendo,

wale wasiopata sababu ndani ya maneno Yake,

na wale wasiopata wokovu kwa sababu ya maneno Yake,

ni wale ambao wamehukumiwa na maneno Yake na,

zaidi ya hayo, wamepoteza wokovu Wake,

na fimbo Yake haitaondoka kamwe miongoni mwao.

Wacha wakati na ukweli uwe ushahidi wa Mungu

na uonyeshe kuwa maneno Yake ndiyo ukweli, njia na uhai.

Wacha wakati na ukweli uwe ushahidi wa Mungu

na uonyeshe kuwa maneno Yake ndiyo ukweli, njia na uhai,

ndiyo ukweli, njia na uhai.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp