Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kazi na Kuonekana kwa Mungu | Dondoo 53

07/10/2020

Mwenyezi Mungu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani, Mungu wetu Anatawala! Mwenyezi Mungu anaweka miguu Yake kwenye Mlima wa Mizeituni. Uzuri ulioje! Sikiliza! Sisi walinzi tunapaza sauti zetu: tunaimba kwa pamoja kwa sauti zetu, kwa kuwa Mungu amerudi Sayuni. Tunaona kwa macho yetu wenyewe ukiwa wa Yerusalemu. Furahieni na kuimba kwa sauti kwa pamoja, kwa kuwa Mungu ametufariji na Ameukomboa Yerusalemu. Mungu ameweka wazi mkono Wake mtakatifu machoni pa mataifa yote, mtu halisi wa Mungu amejitokeza! Miisho yote ya dunia imeona wokovu wa Mungu wetu.

Ee, Mwenyezi Mungu! Roho saba wametumwa kutoka kwa kiti Chako cha enzi kwa makanisa yote ili kufichua siri Zako zote. Unaketi kwenye kiti Chako cha enzi cha utukufu na Umesimamia ufalme Wako na kuuimarisha na kuushikilia kwa haki; Umeyadhibiti mataifa yote mbele Yako. Ee, Mwenyezi Mungu! Umeilegeza mikanda ya wafalme, Umeyafungua wazi malango ya mji mbele Yako, yasifungike tena. Kwa maana nuru Yako imefika na utukufu Wako unajitokeza na kuangaza uzuri wake. Giza linaifunika dunia na giza totoro imewafunika watu. Ee, Mungu! Hata hivyo, Wewe, umeonekana na kutuangazia mwanga Wako, na utukufu Wako utaonekana kwetu; mataifa yote yatakuja kwa nuru Yako na wafalme kwa upendo Wako. Unayainua macho Yako na kuangalia kila mahali: Wana Wako wanakusanyika mbele Yako, na wanatoka mbali; Mabinti Zako wanabebwa mikononi. Ee, Mwenyezi Mungu! Upendo Wako mkubwa umetushika; ni Wewe unayetuongoza mbele kwenye njia inayouelekea ufalme Wako na ni maneno Yako matakatifu yanayopenya na kuenea ndani mwetu.

Ee, Mwenyezi Mungu! Tunakushukuru na kukusifu! Hebu tukuheshimu, tukushuhudie, tukusifu, na kukuimbia kwa mioyo safi, yenye utulivu, na thabiti. Hebu tuwe na akili moja na kujengwa pamoja, na Utufanye tuwe wanaoupendeza moyo Wako hivi karibuni, wanaotumika na Wewe. Tunatamani kwamba mapenzi Yako yatekelezwe katika nchi yote bila kuzuiwa.

kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp