Ushuhuda wa Kweli | Ndoto Yangu ya Kuwa Mwelekezi

26/07/2020

Ndoto Yangu ya Kuwa Mwelekezi ni ushuhuda wa Mkristo anayepitia hukumu ya Mungu na kuadibu Kwake. Mhusika mkuu anapokuwa akitekeleza wajibu wake kanisani, anatamani sana kuwa mwelekezi na kupendwa na wengine. Anafanya juu chini kupata haya huku akivumilia magumu na kulipa gharama. Lakini baada ya kupitia ushinde na vipingamizi mara mbili, ni kwa njia tu ya hukumu na kuadibu kwa neno la Mungu ndiyo hatimaye anaelewa kuwa nia zake katika kutekeleza wajibu wake zilikuwa kupata sifa, faida, na hadhi, na pia anaona waziwazi kiini na hatari kubwa ya mwisho ya kufuatilia mambo haya. Kuanzia wakati huo na kuendelea, halengi tena hadhi yake katika wajibu wake, lakini anafuatilia ukweli kwa unyenyekevu, na anaondokana na utumwa na vizuizi vya sifa na faida polepole. Mwishowe, anagundua kwa kweli kwamba hukumu na kuadibu kwa Mungu ni upendo na ulinzi Wake mkuu kwa wanadamu.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp