Video ya Injili | "Kutoka Kinywani mwa Mauti" | Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

30/07/2018

Liu Zhen, mwenye umri wa miaka 78, ni mke wa nyumbani wa kawaida wa mashambani. Baada ya kumwamini Mungu, alihisi furaha isiyo na kisawe na kusoma maneno Yake na kuimba nyimbo za kumsifu siku zote, na mara nyingi kukusanyika pamoja na ndugu zake kushirikiana juu ya ukweli. ... Hata hivyo, mambo mazuri hayadumu. Anakamatwa na kuteswa na serikali ya Kikomunisti ya China, ikimtia katika shida mbaya sana. Polisi wanampeleka kwenye kituo cha polisi kwa ajili ya kuhojiwa mara tatu, na kumwonya asimwamini Mungu tena. Wanamchunguza na kwenda nyumbani kwake ili kumtisha. Chini ya shinikizo la serikali ya Kikomunisti ya China, mumewe, mwanawe, na mkwe wake pia wanapinga na kuzuia imani yake kwa Mungu. Kupitia maumivu haya, anamtegemea na kumtazamia Mungu kwa kweli, na maneno Yake yanampa imani na nguvu, yakimruhusu kusimama imara kati ya mateso na dhiki. Katika kilele cha mateso yake wakati hajiwezi kabisa, anamlilia Mungu kwa dharura. Anasikia sala yake na kumfungulia njia. Jioni moja, ghafla anapoteza fahamu na hawezi kuamshwa. Daktari anasema kuwa hawezi kuokolewa na anaiambia familia yake ijiandae kwa ajili ya kuaga kwake, lakini baada ya masaa 18, kimiujiza anaamka. Muujiza huu wa Mwenyezi Mungu unawashangaza wale walio karibu na yeye na kumfungulia njia mpya. ... Baada ya uzoefu huu, Liu Zhen anakuja kuelewa kwa undani kwamba maisha ya watu hayana uhakika, na hakuna yeyote kati yetu anayeweza kuyadhibiti—ni Mungu pekee ndiye Anayetawala jaala ya watu na ana maisha yetu, mauti, mafanikio, na bahati mbaya mikononi Mwake. Pia anakuja kupata uzoefu kwamba ni Mungu pekee ndiye ambaye Aliyepo kwa ajili yetu, daima Yuko karibu kutusaidia, na ni Yeye tu tunayeweza kumwamini na kumtegemea!

Baadhi ya taarifa katika video hii zinatoka kwa:

www.stockfootage.com

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp