Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 551

26/10/2020

Kuwa na utambuzi, kuwa na utii, na kuwa na uwezo wa kubaini mambo ili uwe hodari katika roho ina maana kuwa maneno ya Mungu yanakuangaza na kukupa nuru ndani mara tu unapokabiliwa na kitu fulani. Huku ni kuwa hodari katika roho. Kila kitu ambacho Mungu hufanya ni kwa ajili ya kusaidia kufufua roho za watu. Kwa nini Mungu daima husema kuwa watu ni wa kujijali na wajinga? Ni kwa sababu roho za watu zimekufa, na wamekuwa wa kutojali kiasi kwamba hawajui kabisa mambo ya roho. Kazi ya Mungu ni kuyafanya maisha ya watu yaendelee na ni kusaidia roho za watu zichangamke, ili waweze kubaini mambo ya roho, na wao daima waweze kumpenda Mungu mioyoni mwao na kumridhisha Mungu. Ufikaji mahali hapa huonyesha kwamba roho ya mtu imefufuliwa, na wakati mwingine atakapokabiliwa na kitu fulani, anaweza kuonyesha hisia mara moja. Yeye huitikia mahubiri, na kuonyesha hisia haraka kwa hali mbalimbali. Huku ndiko kufanikisha uhodari wa roho. Kuna watu wengi ambao wana majibu ya haraka kwa tukio la nje, lakini mara tu kuingia katika uhalisi au mambo kinaganaga ya roho yanapotajwa, wao huwa wa kutojali na wajinga. Wao huelewa kitu tu kikiwa ni dhahiri. Hizi zote ni ishara za kuwa wa kutojali kiroho na mjinga, za kuwa na uzoefu kidogo wa mambo ya roho. Watu wengine ni hodari wa roho na wana utambuzi. Mara tu wanaposikia maneno yanayoonyesha hali zao, wanaharakisha kuyaandika. Mara wanaposikia maneno kuhusu kanuni za kutenda, wanaweza kuyakubali na kuyatumia katika uzoefu wao unaofuata. Huyu ni mtu ambaye ni hodari katika roho. Kwa nini anaweza kuonyesha hisia haraka hivyo? Ni kwa sababu yeye hulenga mambo haya katika maisha ya kila siku. Anaposoma maneno ya Munu, anaweza kuzipima hali zake kwa kuyatumia na kujitafakari. Anaposikia ushirika na mahubiri na kusikia maneno yanayoleta nuru na mwanga, anaweza kuyapokea mara moja. Ni sawa na kumpa mtu mwenye njaa chakula; anaweza kula mara moja. Ukimpa chakula mtu asiye na njaa, hana haraka kuonyesha hisia. Daima wewe humwomba Mungu, na kisha unaweza kuonyesha hisia mara moja unapokabiliwa na kitu fulani: kile Mungu huhitaji katika jambo hili, na jinsi unavyopaswa kutenda. Mungu alikuongoza juu ya suala hili mara ya mwisho; unapokabiliwa na kitu cha aina hii leo, kwa kawaida utajua jinsi ya kutenda kwa namna inayoridhisha moyo wa Mungu. Ikiwa unatenda daima kwa njia hii na daima upate uzoefu kwa njia hii, wakati fulani utakuwa stadi kwayo. Wakati unasoma neno la Mungu unajua ni mtu wa aina gani Mungu anamzungumzia, unajua ni aina gani ya hali za roho Anayozungumzia, na unaweza kuelewa jambo muhimu na kulitia katika vitendo; hii inaonyesha kuwa unaweza kupata uzoefu. Kwa nini watu wengine hawana jambo hili? Ni kwa sababu hawaweki jitihada nyingi katika kipengele cha kutenda. Ingawa wako tayari kutia ukweli katika vitendo, hawana umaizi wa kweli katika utondoti wa huduma, katika utondoti wa ukweli katika maisha yao. Wanachanganyikiwa jambo linapotokea. Kwa njia hii, unaweza kupotoshwa nabii wa uongo au mtume wa uongo anapokuja. Lazima ushiriki mara nyingi kuhusu maneno na kazi ya Mungu—ni kwa njia hii tu ndiyo utaweza kuuelewa ukweli na kukuz utambuzi. Ikiwa huelewi ukweli, basi hutakuwa na utambuzi. Kwa mfano, kile Mungu husema, jinsi Mungu hufanya kazi, yale yaliyo matakwa Yake kwa watu, ni watu wa namna gani unapaswa kuwasiliana nao, na ni watu wa aina gani unaopaswa kuwakataa—ni lazima ushiriki mara nyingi kuhusu mambo haya. Ukipitia neno la Mungu kwa njia hii daima, utaelewa ukweli na uelewe vizuri vitu vingi, na utakuwa na utambuzi pia. Ni nini kufundishwa nidhamu na Roho Mtakatifu, ni nini lawama inayotokana na nia ya mwanadamu, ni nini mwongozo kutoka kwa Roho Mtakatifu, ni nini mpango wa mazingira, ni nini maneno ya Mungu yanatolea nuru ndani, kama huna uhakika juu ya mambo haya, hutakuwa na utambuzi. Unapaswa kujua kile ambacho huja kutoka kwa Roho Mtakatifu, ni nini tabia ya uasi, jinsi ya kulitii neno la Mungu, na jinsi ya kuacha uasi wako mwenyewe; ikiwa una ufahamu wa vitendo wa mambo haya, utakuwa na msingi; kitu kinapotendeka, utakuwa na ukweli unaofaa wa kutumia kukipima na maono yanayofaa kama msingi. Utakuwa na kanuni katika kila kitu unachofanya, na utaweza kutenda kulingana na ukweli. Halafu maisha yako yatajazwa na nuru ya Mungu, yatajazwa na baraka za Mungu. Mungu hatamtendea vibaya mtu yeyote ambaye humtafuta kwa kweli. Hatamtendea vibaya mtu yeyote ambaye huishi kwa kumdhihirisha na ambaye hushuhudia kwa ajili Yake, na hatamlaani mtu yeyote ambaye kwa kweli anaweza kuona kiu ya ukweli. Ikiwa, unapokula na kunywa maneno ya Mungu, unaweza kuzingatia hali yako mwenyewe ya kweli, kuzingatia vitendo vyako mwenyewe, na kuzingatia ufahamu wako mwenyewe, basi, unapokabiliwa na tatizo, utapokea nuru na utapata ufahamu wa utendaji. Kisha utakuwa na njia ya kutenda na utakuwa na utambuzi kwa kila kitu. Mtu aliye na ukweli si rahisi kudanganywa, na rahisi kutenda kwa vurugu au kutenda kwa kupita kiasi. Kwa sababu ya ukweli amelindwa, na pia kwa sababu ya ukweli yeye hupata ufahamu zaidi. Kwa sababu ya ukweli ana njia zaidi za kutenda, hupata fursa zaidi za Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yake, na hupata fursa zaidi za kukamilishwa.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

God Will Bless Those Who Sincerely Pursue the Truth

What is discipline by the Holy Spirit? What is blame born of man’s will? What is guidance from the Holy Spirit? The arrangement of an environment? What is God’s words enlightening within? If you’re not clear about these things, you’ll have no discernment. God will not mistreat those sincerely seeking Him or anyone who lives Him out and bears witness. He will not curse a person able to sincerely thirst for truth.

You should know what comes from the Spirit, what rebellion is, how to obey God’s word, escaping your rebelliousness. If you understand these things, you’ll have a foundation; when something happens, you’ll have truth to compare to, with suitable visions grounding you, principled in all you do, acting according to the truth, enlightened and blessed by God. God will not mistreat those sincerely seeking Him or anyone who lives Him out and bears witness. He will not curse a person able to sincerely thirst for truth.

When eating and drinking God’s words, if you see your true condition and pay attention to your practice and your own understanding, then when you meet a problem, you will be enlightened, gain understanding and discernment, and have a path of practice. A person with truth is unlikely to be deceived, or cause disruptions, acting excessively. Because of truth he’s protected and gains more understanding, more paths to practice, more chances for the Holy Spirit’s work and perfection. God will not mistreat those sincerely seeking Him or anyone who lives Him out and bears witness. He will not curse a person able to sincerely thirst for truth.

from Follow the Lamb and Sing New Songs

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp