Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 469

05/10/2020

Kama watu hawana imani yoyote, sio rahisi kuendelea katika njia hii. Kila mtu sasa anaweza kuona kuwa kazi ya Mungu hailingani hata kidogo na fikira za watu. Mungu amefanya kazi nyingi sana na kuzungumza maneno mengi sana, ambayo hayalingani kabisa na dhana za binadamu. Hivyo, lazima watu wajiamini na wawe na utashi kuweza kusimama na kile wameshakiona na kile wamepata kutoka kwa uzoefu wao. Haijalishi ni nini Mungu Anafanya kwa watu, lazima washikilie kile walicho nacho, wawe waaminifu mbele za Mungu, na wasalie wenye kujitolea Kwake hadi mwisho. Huu ni wajibu wa wanadamu. Lazima watu watetee kile wanachopaswa kufanya. Imani katika Mungu inahitaji utiifu Kwake na uzoefu wa kazi Yake. Mungu Amefanya kazi nyingi sana—inaweza semekana kuwa kwa watu yote ni kukamilishwa, yote ni usafishaji, na hata zaidi, yote ni kuadibu. Hakujakuwa na hatua hata moja ya kazi ya Mungu ambayo imelingana na dhana za binadamu; kile watu wamefurahia ni maneno makali ya Mungu. Mungu Atakapokuja, watu wanapaswa kufurahia enzi Yake na hasira Yake, lakini haijalishi maneno Yake yalivyo makali, Anakuja kuokoa na kukamilisha binadamu. Kama viumbe, watu wanapaswa watekeleze wajibu ambao wanafaa kufanya, na kusimama shahidi kwa Mungu katikati ya usafishaji. Katika kila jaribio wanapaswa washikilie ushahidi ambao wanapaswa washuhudie, na kushuhudia ushuhuda mkubwa kwa Mungu. Huyu ni mshindi. Haijalishi Mungu Anavyokuboresha, unabaki kuwa na imani kubwa na kutopoteza imani katika Mungu. Ufanye kile mwanadamu anafaa kufanya. Hiki ndicho Mungu Anahitaji kwa mwanadamu, na moyo wa binadamu unapaswa kuweza kurudi Kwake kikamilifu na kumwelekea katika kila wakati. Huyu ni mshindi. Wale wanaoitwa washindi na Mungu ni wale ambao bado wanaweza kusimama kama mashahidi, wakidumisha imani yao, na ibada yao kwa Mungu wanapokuwa chini ya ushawishi wa Shetani na kuzingirwa na Shetani, hiyo ni, wanapokuwa katika nguvu za giza. Kama bado unaweza kudumisha moyo wa utakaso na upendo wako wa kweli kwa Mungu kwa vyovyote vile, unasimama shahidi mbele ya Mungu, na hii ndio Mungu Anaita kuwa mshindi. Kama kufuata kwako ni bora kabisa Mungu Anapokubariki, lakini unarudi nyuma bila baraka Zake, si huu ni utakaso? Kwa sababu una uhakika kuwa njia hii ni ya kweli, lazima uifuate hadi mwisho; lazima udumishe ibada yako kwa Mungu. Kwa sababu umeona kuwa Mungu Mwenyewe amekuja duniani kukukamilisha, lazima umpe moyo wako Kwake kabisa. Haijalishi ni nini Anafanya, hata kama Anaamua tokeo lisilofaa kwako mwishowe, bado unaweza kumfuata. Hii ni kudumisha usafi wako mbele za Mungu. Kupeana mwili wa kiroho mtakatifu na bikira safi kwa Mungu inamaanisha kuweka moyo mwaminifu mbele za Mungu. Kwa wanadamu, uaminifu ni usafi, na kuweza kuwa mwaminifu kwa Mungu ni kudumisha usafi. Hii ndiyo unafaa kuweka katika matendo. Unapopaswa kuomba, omba; unapopaswa kukusanyika pamoja katika ushirika, fanya hivyo; unapopaswa kuimba nyimbo za kidini, imba nyimbo za kidini; na unapopaswa kuunyima mwili, unyime mwili. Unapotekeleza wajibu wako hulimalizi kwa kubahatisha; unapokumbana na majaribu unasimama imara. Hii ni ibada kwa Mungu. Usiposhikilia kile ambacho watu wanapaswa kufanya, basi kuteseka kwako na maazimio ya hapo awali yalikuwa ya bure.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp