Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 436

26/10/2020

Ili kurudisha mfanano wa mtu wa kawaida, yaani, kutimiza ubinadamu wa kawaida, watu hawawezi tu kumpendeza Mungu kwa maneno yao. Wanajiumiza wenyewe kwa kufanya hivyo, na haileti faida yoyote kwa kuingia na kubadili kwao. Kwa hivyo, ili kufikia mbadiliko, watu lazima watende kidogo kidogo, waingie taratibu, watafute na kuchunguza kidogo kidogo, waingie ndani kutoka kwa halisi, na kuishi maisha ya utendaji wa ukweli, maisha ya watakatifu. Tangu sasa kuendelea, inahusisha mambo halisi, vitu halisi, na mazingira halisi, kuwaruhusu watu kuwa na mafunzo ya utendaji. Haiwahitaji hao kutoa maneno matupu; badala yake, inahitaji mafunzo katika mazingira halisi. Watu huja kutambua kuwa wao ni wenye ubora duni wa tabia, na kisha wana kula na kunywa halisii kwa maneno ya Mungu halisi, kuingia halisi, na utandaji halisi, hivi ndivyo wanavyopokea uhalisi na hivi ndivyo kuingia kunaweza kufanyika hata haraka zaidi. Ili kuwabadili watu, lazima kuwe na utendaji, lazima wafanye mazoezi na mambo halisi, vitu halisi, na mazingira halisi. Kwa kutegemea tu maisha ya kanisa, inawezekana kutimiza mafunzo ya kweli? Je, mwanadamu angeingia katika uhalisi? La. Iwapo mwanadamu hawezi kuingia katika maisha halisi, basi yeye hawezi kubadili njia zake za zamani za kufanya mambo na kuishi maisha. Sio tu kwa sababu ya uvivu wa mwanadamu au utegemezi wake wa nguvu, bali ni kwa sababu mwanadamu hana uwezo wa kuishi, na zaidi, hana ufahamu wa kiwango cha mfanano wa mtu wa kawaida. Hapo kale, watu walikuwa daima wakiongea, wakinena, wakiwa na ushirika, hata wakawa “wanenaji hodari”; lakini hakuna yeyote kati yao alitafuta mabadiliko katika tabia ya maisha; walishikilia tu kutafuta nadharia za kina. Kwa hivyo, leo inapasa mbadili maisha haya ya kidini ya kumwamini Mungu. Lazima muingie ndani na kutenda kwa kulenga kitu kimoja, jambo moja, mtu mmoja. Lazima mfanye mambo na malengo—hapo tu ndio mtafikia matokeo. Ili kuwabadili watu, lazima kuanze na kiini chao. Kazi lazima ilenge kiini cha watu, maisha yao, uvivu, utegemezi, na utumwa wa watu, na kwa njia hii tu ndio wanaweza kubadilishwa.

Ijapokuwa maisha ya kanisa yanaweza kuleta matokeo katika sehemu nyingine, msingi bado ni kuwa maisha halisi yanaweza kuwabadilisha watu, na hali yao ya kale haiwezi kubadilika bila maisha halisi. Hebu tuchukue kazi ya Yesu katika Enzi ya Neema. Yesu alipoharamisha sheria za awali na kuanzisha amri za enzi mpya, Alinena kupitia mifano ya maisha halisi. Wakati Yesu Alipowaongoza wanafunzi wake kupita katika shamba la ngano siku ya Sabato, wanafunzi Wake walihisi njaa na wakatunda na kula masuke ya nafaka, Mafarisayo walipoona hivi walisema kuwa hawakuitii Sabato. Pia walisema kuwa watu hawakuruhusiwa kuwaokoa ndama walioanguka shimoni katika siku ya Sabato, wakisema kuwa hakuna kazi ingepaswa kufanywa wakati wa Sabato. Yesu alitumia matukio haya ili kutangaza rasmi amri za enzi mpya hatua kwa hatua. Wakati huo, Alitumia mambo mengi ya kiutendaji ili watu waelewe na kubadilika. Hii ndiyo kanuni ambayo kwayo Roho Mtakatifu hutekeleza kazi Yake, na ni njia hii pekee inayoweza kubadili watu. Wanapokosa mambo ya kiutendaji, watu wanaweza tu kupata ufahamu katika nadharia na wanaweza kuelewa tu mambo kiakili—hii si njia ya kufaa kubadili watu. Tukiongea juu ya kupata busara na ufahamu kupitia mafundisho, hili lingetimizwaje? Je, mwanadamu angeweza kupata busara na ufahamu kwa kusikiza, kusoma na kukuza ujuzi wake tu? Je, hili linasababishaje kupata busara na ufahamu? Mtu lazima afanye bidii kuelewa na kuwa na uzoefu kupitia maisha halisi. Kwa hivyo, mafunzo hayawezi kukosa na mtu hawezi kuacha maisha halisi. Mtu lazima azingatie hali tofauti na aingie kwa hali mbalimbali: kiwango cha elimu, ufafanuzi, uwezo wa kuona mambo, utambuzi, uwezo wa kuelewa maneno ya Mungu, maarifa ya kawaida na kanuni za ubinadamu, na vitu vingine vinavyohusiana na ubinadamu ambavyo mtu lazima awe navyo. Baada ya ufahamu kufikiwa, mtu lazima alenge kuingia, na hapo tu ndio mabadiliko yanaweza kufikiwa. Iwapo mwanadamu amefikia ufahamu lakini anakaidi utendaji, mabadiliko yanawezaje kutokea? Sasa, mwanadamu amefahamu mengi, lakini haishi kwa kudhihirisha uhalisi, hivyo basi anaweza kuwa tu na ufahamu halisi kidogo wa maneno ya Mungu. Umepata nuru kwa kiasi kidogo, umepokea mwangaza kidogo kutoka kwa Roho Mtakatifu, lakini huna kuingia katika maisha halisi, au hata huenda hujali juu ya kuingia, hivyo basi utakuwa na mabadiliko kidogo tu. Baada ya muda mrefu hivyo, watu wameelewa mengi na wanaweza kusema mengi juu ya ujuzi wao wa nadharia, lakini tabia yao ya nje husalia ile ile, na ubora wa tabia yao wa asili hudumu bila upandaji hadhi hata kidogo. Iwapo mambo yako hivi, mtaingia lini humo hatimaye?

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp