Swahili Christian Testimony Video | Baada ya Uwongo

20/05/2020

Baada ya Uwongo ni ushuhuda wa Mkristo anayepitia hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu. Kupitia kusoma maneno ya Mungu, mhusika mkuu anakuja kuelewa kwamba Mungu anawapenda wale waaminifu na kuwadharau wale wadanganyifu, na kwamba ni waaminifu tu ndio wanaoweza kuokolewa kikamilifu na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwa hivyo, anaanza kutafuta kuwa mtu mwaminifu. Lakini anapokabiliwa na mambo ambayo yanaweza kuathiri sifa na hadhi yake katika maisha ya kila siku, bado hawezi kujizuia kusema uwongo na kudanganya, na wakati mwingine anaficha uwongo wake baada ya ukweli. Anakuja kuhisi wasiwasi sana na anagundua kuwa ni njia ngumu na ya kuchosha ya kuishi. Baadaye, kupitia hukumu na ufunuo wa maneno ya Mungu, anapata ufahamu kiasi kuhusu tabia yake ya kishetani ambayo humfanya aseme uwongo na kudanganya. Anaona chanzo, asili, na matokeo ya kusema uwongo, anaanza kujuta, na anatubu kwa Mungu. Yeye anatia kuwa mtu mwaminifu katika vitendo, akiwafungulia roho kina ndugu ili kufichua nia zake za udanganyifu, na anapitia furaha ya kusema ukweli na kuwa mwaminifu.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp