New Swahili Christian Video "Kufufuka" | Hukumu ya Mungu katika Siku za Mwisho Iliniokoa

12/06/2018

Jina lake ni Zheng Lu, na tangu utotoni, alikuwa hasa ovyo. Kwa sababu ya ushawishi wa kijamii na elimu ya utamaduni wa kidesturi wa Kichina, alisoma bila kuchoka, akitumai kufikia chuo kikuu na kufanikisha ndoto yake ya kuwapiku marika wake na kuwa na mafanikio, lakini ajali isiyotarajiwa ilimharibia ndoto yake. Wakati tu alipohisi vibaya, mnyonge, na asiyeweza kuupata mwelekeo maishani, wokovu wa Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho ulimpata. Baada ya kuanza kumsadiki Mungu, alifuatilia kwa shauku, akatenda wajibu wake kwa kujitolea, akapata idhini ya kaka na dada zake na miaka miwili baadaye alichaguliwa kuwa kiongozi wa kanisa. Lakini bila kujua, tamanio lake la ufanisi lilianza tena kukua ndani yake, na kiburi, majivuno na tamanio lake la umaarufu na heshima na fahari kuu ya asili yake ya kishetani vyote vilijifichua kila mara katika wajibu wake, na kutatiza pakubwa kazi ya kanisa. Kwa kupitia hukumu tena na tena, kuadibu, upogoaji, na kushughulikiwa na neno la Mungu, anatafakari kwa kina, na hatimaye kuona waziwazi kwamba amekuwa mpotovu sana na ametiwa sumu za kishetani kama vile "Kupata fanaka, kutaka kuwa bora zaidi kuliko wengine," "Kama vile mti huishi kwa sababu ya ganda lake, mtu huishi kwa sababu ya uso wake," "Mtu huacha jina lake nyuma popote akaapo, kama vile bata bukini hutetea popote arukapo," vyote ambavyo vilimsababisha kuwa hasa mwenye kiburi na asili ya majivuno na kuabudu cheo na mamlaka, na kumsababisha yeye kuzingatia pakubwa kuufuatilia umaarufu na fahari kuu kutokana na miaka yake ya kuwa na imani katika Mungu badala ya kuufuatilia ukweli. Bila ya yeye kujijua, alikuwa ameitembelea njia ya mpingakristo. Wakati uo huo anapopata upenyezi wa kina katika kiini na hatari za ufuatiliaji wa umaarufu na cheo, anaanza kuuchukia sana umaarufu, cheo na asili yake binafsi ya kishetani, anabadilisha mtazamo wake wa kimakosa wa kimaisha na maadili na kwa taratibu anaanza kuitembelea njia bora na sahihi ya maisha, ile ya ufuatiliaji wa ukweli.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp