Wimbo wa Kikristo | Matendo Ya Mungu Yanajaza Ulimwengu Mzima Tupu

19/09/2018

Mungu anatazama chini juu ya vitu vyote kutoka juu, na Anatawala vitu vyote kutoka juu.

Wakati huo huo, Mungu ametuma wokovu Wake juu ya dunia.

Mungu anaangalia kutoka mahali Pake pa siri kila wakati,

kila hatua ya mwanadamu, kila kitu anachosema na kufanya.

Mungu anamjua mwanadamu kama kiganja cha mkono Wake.

Mahali pa siri ni makao ya Mungu, anga ndicho kitanda Mungu akilaliacho.

Nguvu ya Shetani haiwezi kumfikia Mungu, kwani Yeye amejawa na utukufu, haki, na hukumu.

Mungu amekanyaga vitu vyote na miguu Yake, Yeye ananyosha mtazamo Wake juu ya ulimwengu.

Na Mungu ametembea kati ya wanadamu,

ameonja utamu na uchungu, ladha zote za dunia ya mwanadamu;

lakini wanadamu, kamwe hawakumtambua Mungu kweli, wala hawakumwona Mungu alipokuwa akitembea ughaibuni.

Kwa sababu Mungu alikuwa kimya, na hakufanya matendo yasiyo ya kawaida,

hivyo, hakuna aliyemwona kweli.

Vitu haviko vilivyokuwa awali:

Mungu anaenda kufanya vitu ambavyo, katika enzi zote, ulimwengu haujawahi kuona,

Mungu anaenda kunena maneno ambayo, katika enzi zote, wanadamu hawajawahi kusikia,

kwa sababu Yeye anawataka binadamu wote waje kumjua Mungu katika mwili.

kwa sababu Yeye anawataka binadamu wote waje kumjua Mungu katika mwili.

kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp