Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kupata Mwili | Dondoo 131

27/09/2020

Mungu akiwa mkuu zaidi katika ulimwengu wote, na katika ulimwengu wa juu, Angeweza kujieleza Mwenyewe kwa ukamilifu kwa kutumia mfano wa mwili? Mungu hujivika Mwenyewe mwili ili kufanya hatua ya kazi Yake. Hakuna umuhimu mahsusi kwa sura ya mwili, na haina uhusiano na kupita kwa enzi, na haina uhusiano wowote na tabia ya Mungu. Kwa nini Yesu hakuruhusu sura Yake kubaki? Kwa nini hakumruhusu mtu kuchora sura Yake, ili iweze kupitishwa kwa vizazi vya baadaye? Kwa nini Hakuruhusu watu kukubali kwamba sura yake ilikuwa sura ya Mungu? Ingawa sura ya mwanadamu iliumbwa kwa mfano wa Mungu, ni kwa jinsi gani sura ya mwanadamu ingewakilisha mfano wa Mungu aliyeinuliwa? Mungu anapopata mwili, Yeye anashuka tu kutoka mbinguni na kuingia ndani ya mwili maalumu. Roho Wake ashuka kingia ndani ya mwili, kwa njia ambayo Yeye hufanya kazi ya Roho. Roho huonyeshwa katika mwili, na Roho hufanya kazi Yake katika mwili. Kazi iliyofanyika katika mwili inawakilisha Roho kwa ukamilifu, na mwili ni kwa ajili ya kazi, lakini hilo halimaanishi kwamba sura ya mwili ni mbadala wa sura halisi ya Mungu Mwenyewe; hili silo kusudi na umuhimu wa Mungu kupata mwili. Anapata mwili tu ili Roho apate mahali pa kuishi Akifanya kazi Yake, ili Apate kufanikisha kazi Yake katika mwili, ili watu waweze kuona matendo Yake, waelewe tabia Yake, kusikia maneno Yake, na kujua ajabu ya kazi Yake. Jina Lake linawakilisha tabia Yake, kazi Yake inawakilisha utambulisho Wake, lakini Hajawahi kusema kuwa kuonekana Kwake katika mwili kunawakilisha sura Yake; hiyo ni fikira tu ya mwanadamu. Na kwa hiyo, hoja muhimu za kupata mwili kwa Mungu ni jina Lake, kazi Yake, tabia Yake, na jinsia Yake. Yeye hutumia hivi kuwakilisha usimamizi wake katika enzi hii. Kuonekana Kwake katika mwili hakuna uhusiano na usimamizi Wake, na ni kwa ajili tu ya kazi Yake wakati huo. Hata hivyo haiwezekani kwa Mungu mwenye mwili kutokuwa na kuonekana maalumu, na kwa hiyo Anachagua jamii inayofaa ili kuamua kuonekana Kwake. Ikiwa kuonekana kwa Mungu kuna umuhimu wa uwakilishi, basi wale wote ambao wana sifa muhimu za uso sawa na Zake pia wanawakilisha Mungu. Hilo silo kosa la kupita kiasi? Picha ya Yesu ilichorwa na mwanadamu ili mwanadamu angeweza kumwabudu. Wakati huo, hakuna maagizo maalum yaliyotolewa na Roho Mtakatifu, na kwa hiyo mwanadamu alipitisha picha hiyo iliyodhaniwa hadi leo. Kwa kweli, kulingana na kusudi la Mungu, mwanadamu hakupaswa kufanya hivyo. Ni ari tu ya mwanadamu ambayo imesababisha picha ya Yesu kubaki hadi siku hii. Mungu ni Roho, na mwanadamu hataweza kamwe kuwa na uwezo wa kutoa muhtasari wa hasa sura Yake ni nini. Sura Yake inaweza tu kuwakilishwa na tabia Yake. Huwezi kufafanua kuonekana kwa pua Lake, kwa mdomo Wake, kwa macho Yake, na kwa nywele Zake. Wakati ufunuo ulipofika kwa Yohana, aliona sura ya Mwana wa Adamu: Kutoka mdomoni mwake ulikuwa upanga mkali ukatao kuwili, macho Yake yalikuwa kama miale ya moto, kichwa Chake na nywele vilikuwa vyeupe kama sufu, miguu Yake ilikuwa kama shaba iliyong’arishwa, na kulikuwa na mshipi wa dhahabu unaozunguka kifua Chake. Ingawa maneno yake yalikuwa wazi sana, sura ya Mungu aliyoieleza haikuwa sura ya kiumbe. Aliyoona ni maono tu, na sio sura ya mtu kutoka ulimwengu yakinifu. Yohana alikuwa ameona maono, lakini hakuwa ameshuhudia kuonekana kwa kweli kwa Mungu. Sura ya mwili wa Mungu uliopata mwili ni sura ya uumbaji, na haiwezi kuwakilisha tabia ya Mungu kwa ukamilifu wake. Wakati Yehova alipoumba wanadamu, Alisema kuwa Alifanya hivyo kwa mfano Wake na Akaumba mume na mke. Wakati huo, Alisema Alifanya mume na mke katika mfano wa Mungu. Ingawa sura ya mwanadamu inafanana na sura ya Mungu, haimaanishi kuwa kuonekana kwa mwanadamu ni sura ya Mungu. Huwezi kutumia lugha ya mwanadamu kufanya muhtasari wa sura ya Mungu kwa ukamilifu, kwa maana Mungu ameinuliwa sana, ni mkubwa sana, wa ajabu sana na Asiyeeleweka!

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp