Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 315

01/09/2020

Wengine wanajivika mapambo mazuri, lakini ya juujuu: Kina dada wanajivika mapambo mazuri kama maua, na kina ndugu wanavalia kama wana wa wafalme ama wambuji wadogo matajiri. Wanajali tu kuhusu vitu vya nje, kama vitu wanavyokula na kuvalia; ndani yao, wao ni mafukara na hawamfahamu Mungu hata kidogo. Hili lina maana gani? Na kisha kuna wengine wanaovalia kama waombaji maskini—kweli wanaonekana kama watumwa wa Asia Mashariki! Je, kweli hamwelewi Ninachotaka kutoka kwenu? Shirikini kwa karibu: Mmepata nini kweli? Mmemwamini Mungu kwa miaka hii yote, lakini mmevuna hili tu—je, hamna aibu? Je, hamwoni haya? Mmekuwa mkifuatilia kwenye njia ya kweli kwa miaka hii yote, lakini leo kimo chenu bado ni cha chini kuliko cha jurawa! Watazame mabibi wadogo walio miongoni mwenu, warembo kama picha mkiwa mmevalia mavazi na vipodozi vyenu, mkijilinganisha kati yenu—na ni nini mnacholinganisha? Starehe zenu? Matakwa yenu? Je, mnadhani kwamba Nimekuja kuandikisha waonyesha mitindo? Hamna aibu! Maisha yenu yako wapi? Je, kile mnachokifuatilia si tamaa zilizopita kiasi tu? Unadhani kuwa wewe ni mrembo sana, lakini ingawa umevalia kila aina ya umaridadi, kwa kweli wewe si buu anayegaagaa, aliyezaliwa katika rundo la kinyesi? Leo, huna bahati ya kufurahia baraka hizi za mbinguni kwa ajili ya uso wako mrembo, ila kwa sababu Mungu anafanya jambo la kipekee kwa kukuinua. Je, bado huelewi ulikotoka? Maisha yanapotajwa, unafunga mdomo wako na husemi chochote, na unakimya kama sanamu, lakini bado una ujasiri wa kuvalia vizuri! Bado unataka kupaka uso wako rangi nyekundu na poda! Na watazame wambuji walio miongoni mwenu, wanaume waliopotoka wanaoshinda siku kutwa wakitembea huku na kule polepole, wakaidi, na wenye sura tepetevu usoni pao. Je, hivi ndivyo mtu anapaswa kutenda? Je, kila mmoja kati yenu, awe mwamamume ama mwanamke, anazingatia nini siku nzima? Je, mnajua mnamtegemea nani kujilisha? Tazama mavazi yako, tazama kile ulichovuna mikononi mwako, sugua kitambi chako—umefaidika nini kutoka kwa gharama ya damu na jasho ambayo umelipa katika miaka hii yote ya imani? Bado unafikiri kwenda kutalii sehemu maarufu, bado unafikiri kupamba mwili wako unukao—ufuatiliaji usio na maana! Unaombwa uwe mtu wa kawaida, lakini sasa wewe si mtu asiye wa kawaida tu, wewe ni mpotovu. Mtu kama wewe anawezaje kuwa na ujasiri wa kuja mbele Zangu? Ukiwa na ubinadamu kama huu, ukionyesha uzuri wako na kuringa kwa ajili ya mwili wako, ukiishi daima ndani ya tamaa za mwili—je, wewe si mzao wa mashetani wachafu na pepo waovu? Sitamruhusu shetani mchafu kama huyu aendelee kuishi kwa muda mrefu! Na usifikiri kwamba Sijui kile unachofikiri moyoni mwako. Unaweza kudhibiti vikali tamaa na mwili wako, lakini Nawezaje kukosa kujua fikira zilizo moyoni mwako? Nawezaje kukosa kujua tamaa zote za macho yako? Je, ninyi mabibi wadogo hamjirembeshi sana ili kuonyesha miili yenu? Wanaume wana faida gani kwenu? Je, kweli wanaweza kuwaokoa kutoka katika bahari ya mateso? Na kwa wambuji miongoni mwenu, nyote huvalia ili kujifanya muonekane waungwana na wa heshima, lakini, je, hii si hila iliyokusudiwa kuvuta macho kwa sura zenu changamfu? Mnafanya hili kwa sababu ya nani? Wanawake wana faida gani kwenu? Je, wao si chanzo cha dhambi yenu? Enyi wanaume na wanawake, Nimewaambia maneno mengi sana, lakini mmetii machache tu. Masikio yenu hayataki kusikia, macho yenu yamefifia, na mioyo yenu ni migumu kiasi kwamba kuna tamaa tu katika miili yenu, kiasi kwamba mmetegwa nayo, msiweze kutoroka. Ni nani anayetaka kuwakaribia ninyi mabuu, ninyi mnaojifurukuta katika uchafu na masizi? Msisahau kwamba ninyi tu ni wale Niliowatoa kutoka katika rundo la kinyesi, kwamba mwanzoni hamkuwa na ubinadamu wa kawaida. Ninachotaka kutoka kwenu ni ule ubinadamu wa kawaida ambao hamkuwa nao mwanzoni, si kwamba muonyeshe tamaa zenu ama muachilie miili yenu iliyooza, ambayo imeelekezwa na ibilisi kwa miaka mingi sana. Mnapojivisha nguo hivyo, je, hamwogopi kwamba mtategwa kwa kina zaidi? Je, hamjui kwamba mwanzoni mlikuwa wenye dhambi? Je, hamjui kwamba miili yenu imejaa tamaa sana kiasi kwamba hata inavuja kutoka kwa mavazi yenu, ikifichua hali zenu kama mashetani wabaya na wachafu kukithiri? Je, si kweli kwamba mnajua hili vyema zaidi kuliko yeyote mwingine? Mioyo yenu, macho yenu, midomo yenu—je, si vyote vimenajisiwa na mashetani wachafu? Je, hizi sehemu zenu si chafu? Je, unadhani kwamba alimradi hutendi, basi wewe ndiwe mtakatifu kabisa? Je, unadhani kwamba kuvalia mavazi mazuri kunaweza kuficha nafsi zenu duni? Hilo haliwezekani! Nawashauri muwe wenye uhalisi zaidi: Msiwe wadanganyifu na bandia, na msijigambe. Mnaonyeshana tamaa zenu, lakini yote mtakayopata kama malipo ni mateso ya milele na kurudiwa kikatili! Mna haja gani ya kupepeseana macho yenu na kujiingiza katika mapenzi? Je, hiki ndicho kipimo cha uaminifu wenu, kiasi cha uadilifu wenu? Nawachukia kabisa wale miongoni mwenu wanaojihusisha katika uganga na uchawi; Nawachukia sana wale wanaume na wanawake wadogo miongoni mwenu wanaopenda miili yao wenyewe. Ni vyema mjizuie, kwa sababu sasa mnahitajika kuwa na ubinadamu wa kawaida, na hamruhusiwi kuonyesha tamaa zenu—lakini mnachukua kila fursa muwezayo, kwani miili yenu imejaa sana, na tamaa zenu ni kubwa mno!

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Utendaji (7)

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp