Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 450

03/09/2020

Ikiwa huna maarifa ya kazi ya Mungu, hutajua jinsi ya kushirikiana na Mungu. Ikiwa hujui kanuni za kazi ya Mungu, na hujui jinsi Shetani anavyofanya kazi kwa mwanadamu, hutakuwa na njia ya kutenda. Ufuatiliaji wenye ari pekee hautakuruhusu ufikie matokeo yanayohitajiwa na Mungu. Mbinu kama hiyo ya kupitia ni sawa na ile ya Lawrence: kutotofautisha hali yoyote kabisa na kusisitiza uzoefu tu, kutojua kabisa kazi ya Shetani ni nini, kutojua kazi ya Roho Mtakatifu ni nini, jinsi mwanadamu alivyo bila kuwepo kwa Mungu, na ni watu wa aina gani ambao Mungu anataka kuwakamilisha. Ni kanuni gani zinapaswa kukubaliwa wakati wa kushughulikia aina tofauti za watu, jinsi ya kuelewa vizuri mapenzi ya Mungu sasa, jinsi ya kujua tabia ya Mungu, na ni kwa watu, mazingira, na enzi gani ndiyo huruma, uadhama, na haki ya Mungu huelekezwa—hana utambuzi wowote kuhusu yoyote kati ya haya. Ikiwa watu hawana maono mengi kama msingi wa uzoefu wao, basi uzima haupo, sembuse uzoefu; wanaweza kuendelea kutii na kuvumilia kila kitu kwa upumbavu. Watu kama hawa ni vigumu sana kuwakamilisha. Inaweza kusemwa kuwa ikiwa huna maono yoyote yaliyotajwa hapo juu, hili ni thibitisho tosha kwamba wewe ni mpumbavu, wewe ni kama nguzo ya chumvi ambayo husimama daima katika Israeli. Watu kama hawa ni bure, vinyangarika! Watu wengine hutii kila mara bila kufikiri, wao daima hujitambua na hutumia njia zao wenyewe za kutenda wanaposhughulikia masuala mapya, au wanatumia “hekima” kushughulikia mambo madogo na yasiyofaa kutajwa. Watu kama hao hawana utambuzi, ni kama kwamba asili yao ni kukubali kuonewa bila kulalamika, na wao daima huwa vilevile, hawabadiliki kamwe. Watu kama hawa ni wapumbavu ambao hawana utambuzi hata kidogo. Kamwe hawajaribu kulinganisha matendo kwa hali au watu tofauti. Watu kama hawa hawana uzoefu. Nimewaona watu fulani ambao hushughulika sana katika ujuzi wao wenyewe kiasi kwamba wanapokabiliwa na watu walio na kazi ya pepo waovu, huinamisha vichwa vyao na kukiri dhambi zao, bila kuthubutu kusimama na kuwashutumu. Na wanapokabiliwa na kazi dhahiri ya Roho Mtakatifu, hawathubutu kutii. Wanaamini kwamba pepo hawa waovu pia wako mikononi mwa Mungu, na hawana ujasiri hata kidogo wa kusimama na kuwapinga. Watu kama hawa wanamwaibisha Mungu, na hawawezi kabisa kubeba mzigo mzito kwa ajili ya Mungu. Wapumbavu kama hawa hawaleti tofauti ya aina yoyote. Kwa hivyo, mbinu kama hiyo ya kupata uzoefu, inapaswa kusafishwa, kwani haiwezi kuthibitishwa machoni pa Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuhusu Uzoefu

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp