Filamu za Kikristo | Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu? (Dondoo Teule)

26/02/2018

Waumini wengine huamini kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini wamechaguliwa na kuteuliwa na Bwana, na kwamba wote ni watu wanaomtumikia Bwana. Hivyo wanaamini kwamba kuwatii tu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumtii Bwana, na kwamba kuwaasi au kuwahukumu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumpinga Bwana. Wao huamini hata kuwa, katika makanisa, wachungaji na wazee wa kanisa peke ndio huelewa Biblia na huweza kuelezea Biblia, na almradi kile kinachohubiriwa au kufanywa na wachungaji na wazee wa kanisa kinakubaliana na Biblia na kina msingi katika Biblia, basi watu wanapaswa kuwatii na kuwafuata. Hivyo aina hii ya utiifu kwa wachungaji na wazee wa kanisa inakubaliana na ukweli? Je, ufahamu wa maarifa ya Biblia unawakilisha ufahamu wa ukweli na maarifa ya Mungu? Tunapaswa kuchukua mtazamo upi hasa kwa wachungaji na wazee wa kanisa ambao unafuata mapenzi ya Mungu?

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp