Wimbo wa Kusifu | Unyenyekevu wa Mungu ni wa Kupendeza Sana
01/04/2020
Mungu amejinyenyekeza Mwenyewe kwa kiwango fulani,
kufanya kazi Yake katika watu hawa wachafu na wapotovu,
na kukikamilisha kikundi hiki cha watu.
Mungu hakupata mwili tu ili kuishi na kula kati ya watu,
kuwalisha watu, kutoa wanachohitaji watu.
Jambo muhimu zaidi ni
kwamba Yeye hufanya kazi Yake kubwa ya wokovu na ushindi
kwa watu hawa walio na upotovu usiovumilika.
Alikuja katika kiini cha joka kubwa jekundu ili kuwaokoa watu hawa wapotovu mno,
ili watu wote waweze kubadilishwa na kufanywa wapya.
Tatizo kubwa ambalo Mungu huvumilia
siyo tu shida ambayo Mungu mwenye mwili huvumilia,
lakini hasa ni kwamba Roho wa Mungu hupitia udhalilishaji uliokithiri—
Yeye hujinyenyekeza na kujificha Mwenyewe sana kiasi kwamba Yeye huwa mtu wa kawaida.
Mungu alipata mwili na kuchukua mfano wa mwili
ili watu waone kwamba Ana maisha ya kawaida ya binadamu,
na kwamba ana mahitaji ya kawaida ya binadamu.
Hili linatosha kuthibitisha kwamba Mungu amejinyenyekeza Mwenyewe kwa kiwango fulani.
Roho wa Mungu hufanyika katika mwili.
Roho Wake ni wa juu sana na mkuu,
lakini Yeye huchukua mfano wa mwanadamu wa kawaida,
wa mwanadamu asiye muhimu
ili kufanya kazi ya Roho Wake.
Ubora wa tabia, umaizi,
hisi, ubinadamu, na maisha ya kila mmoja
wenu vinaonyesha kwamba hamfai kweli kupokea kazi ya Mungu ya aina hii.
Hakika hamfai kumruhusu Mungu kuvumilia shida kama hiyo kwa ajili yenu.
Mungu ni mkubwa sana. Mungu ni mkubwa sana.
Yeye ni mkuu sana, na watu ni duni sana na wa hali ya chini,
lakini Yeye bado huwafanyia kazi.
Yeye hakupata mwili tu ili kuwaruzuku watu, kuzungumza na watu,
Yeye hata huishi pamoja na watu.
Mungu ni mnyenyekevu sana, wa hupendeka sana.
kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?
Aina Nyingine za Video