Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 523

Alipokuwa akiadibiwa na Mungu, Petro aliomba, “Ee Mungu! Mwili wangu ni mkaidi, na unaniadibu na kunihukumu mimi. Nafurahi katika adabu Yako na hukumu, na hata kama Hunitaki mimi, katika hukumu Yako mimi ninaona tabia Yako takatifu na tabia Yako ya haki. Unaponihukumu, ili wengine wapate kuiona hali Yako ya haki katika hukumu Yako, ninaridhika. Iwapo hukumu Yako itaonyesha tabia Yako, na kuruhusu tabia Yako ya haki kuonekana na viumbe wote, na iwapo inaweza kufanya upendo wangu Kwako uwe safi zaidi, ili niweze kufikia mfano wa mwenye haki, basi hukumu Yako ni nzuri, kwa maana hivyo ndivyo mapenzi Yako ya neema yalivyo. Najua kwamba bado kuna mengi ndani yangu yaliyo ya uasi, na kwamba mimi bado sifai kuja mbele Yako. Ningependa unihukumu hata zaidi, iwe ni kupitia mazingira ya uhasama au mateso makubwa; haijalishi jinsi Utakavyonihukumu, kwangu itakuwa ya thamani. Upendo Wako ni mkuu, na mimi niko tayari kujiweka katika huruma Yako bila malalamiko hata kidogo.” Huu ni ufahamu wa Petro baada ya yeye kuiona kazi ya Mungu, na pia ni ushahidi wa upendo wake kwa Mungu. Leo hii, nyinyi tayari mmeshashindwa—lakini ni jinsi gani ushindi huu unaonekana ndani yenu? Baadhi ya watu wanasema, “Ushindi Wangu ni neema kuu na kuinuliwa kwa Mungu. Ni sasa tu ndipo ninapotambua kwamba maisha ya mwanadamu ni bure na yasiyo na maana. Kuishi hakuna maana, afadhali nife. Ingawa mtu anatumia maisha yake kukimbia huku na kule, kuzalisha na kuongeza kizazi baada ya kizazi cha watoto, mtu hatimaye huwachwa bila chochote. Leo, baada tu ya kushindwa na Mungu ndio nimeona kwamba hakuna thamani ya kuishi kwa njia hii; kwa kweli ni maisha yasiyo na maana. Afadhali nife na kuyasahau haya!” Je, watu kama hao ambao wameshindwa wanaweza kukombolewa na Mungu? Je, wanaweza kuwa vielelezo na mifano? Watu kama hao ni somo katika kutoshughulika, hawana matarajio, na wala kujitahidi kujiboresha wenyewe! Ingawa wao huhesabiwa kama walioshindwa na Mungu, watu kama hao wasioshughulika hawawezi kufanywa wakamilifu. Karibu mwishoni mwa maisha yake, baada ya yeye kufanywa kuwa mkamilifu, Petro akasema, “Ee Mungu! Kama ningeweza kuishi miaka michache zaidi ya hapa, ningependa kufikia usafi zaidi na upendo wa ndani Kwako.” Alipokuwa karibu kusulubiwa, katika moyo wake akaomba, “Ee Mungu! Wakati Wako umewadia, wakati ulionitayarishia umefika. Mimi lazima nisulubiwe kwa ajili Yako, lazima niwe na ushuhuda huu Kwako, na ninatumai kwamba upendo wangu utaweza kukidhi mahitaji Yako, na kwamba unaweza kuwa safi zaidi. Leo, kuwa na uwezo wa kufa kwa ajili Yako, na kusulubiwa kwa ajili Yako, ni faraja na ya kutia moyo kwangu, kwa maana hakuna kinachonifurahisha kuliko kuweza kusulubiwa kwa ajili Yako na kukidhi matakwa Yako, na kuweza kujitoa Kwako, kutoa maisha yangu Kwako. Ee Mungu! Wewe ni wa kupendeza kweli! Kama Ungeniruhusu niishi, ningenuia kukupenda zaidi. Mradi tu ninaishi, mimi nitakupenda. Natamani kukupenda kwa undani zaidi. Unanihukumu, Unaniadibu, na kunijaribu kwa sababu mimi si mwenye haki, kwa sababu nimetenda dhambi. Na tabia Yako ya haki inakuwa dhahiri zaidi kwangu. Hii ni baraka kwangu, kwa maana ninapata uwezo wa kukupenda kwa undani zaidi, na mimi niko tayari kukupenda kwa njia hii hata kama Hunipendi. Mimi niko tayari kutazama tabia Yako ya haki, kwa maana inafanya niweze kuishi maisha ya maana zaidi. Mimi ninahisi kwamba maisha yangu sasa ni ya maana zaidi, kwa maana nimesulubiwa kwa ajili Yako, na ni jambo la maana kufa kwa ajili Yako. Hata hivyo bado mimi sijaridhika, kwa maana najua kidogo sana kukuhusu, najua kwamba siwezi kutimiza matakwa Yako kikamilifu, na kuwa nimekulipa kidogo mno. Katika maisha yangu, sijaweza kurudisha nafsi yangu Kwako kikamilifu; Niko mbali sana na hili. Nikitazama nyuma kwa wakati huu, mimi huhisi kuwa nina mzigo mkubwa wa madeni kwako, na sina muda mwingine ila huu kwa ajili ya kurekebisha makosa yangu na upendo wote ambao sijakulipa Wewe.”

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp