Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 174

29/07/2020

5. Bubujiko la Hewa

Kitu cha tano ni kipi? Kitu hiki kinahusiana sana na maisha ya kila siku ya mwanadamu, na uhusiano huu thabiti. Ni kitu ambacho mwili wa mwanadamu hauwezi kuishi bila katika ulimwengu huu yakinifu. Kitu hiki ni bubujiko la hewa. “Bubujiko la hewa” ni neno ambalo watu wote labda wanaelewa. Hivyo bubujiko la hewa ni nini? Jaribuni kueleza katika maneno yenu wenyewe. (Bubujiko la hewa ni kububujika kwa hewa.) Mngesema hilo. Kububujika kwa hewa kunaitwa “bubujiko la hewa.” Bubujiko la hewa ni upepo ambao jicho la mwanadamu haliwezi kuona. Pia ni njia ambayo gesi husonga. Lakini ni bubujiko la hewa gani tunalozungumzia hapa? Mtaelewa punde Nitakaposema. Dunia hubeba milima, bahari, na vitu vyote inapogeuka, na inapogeuka kuna spidi. Hata ikiwa huwezi kuhisi kuzunguka kokote, mzunguko wake upo kweli. Mzunguko wake huleta nini? Ni nini hufanyika mtu anapokimbia? Huwa kuna upepo kando ya masikio yako unapokimbia? (Ndiyo.) Ikiwa upepo unaweza kuzalishwa unapokimbia, inawezekanaje kutokuwepo kwa nguvu za upepo dunia inapozunguka? Dunia inapozunguka, vitu vyote viko katika mwendo. Iko katika mwendo na kuzunguka katika spidi fulani, wakati vitu vyote duniani daima vinazaa na kukua. Kwa hiyo, kusonga kwa spidi fulani kwa kawaida kutaleta bubujiko la hewa. Hilo ndilo bubujiko la hewa. Bubujiko la hewa hilo litaathiri mwili wa mwanadamu kwa kiasi fulani? Taiwan na Hong Kong zote zina tufani. Tufani hizo hazina nguvu sana, lakini zinapotokea, watu hawawezi kusimama kwa utulivu na huona vigumu kutembea katika upepo huo. Ni vigumu hata kutembea hatua moja. Ina nguvu sana, baadhi ya watu wanasukumwa na upepo dhidi ya kitu na hawawezi kusonga. Hii ni mojawapo ya njia ambazo bubujiko la hewa linaweza kuathiri wanadamu. Ikiwa dunia nzima ingekuwa imejaa tambarare, ingekuwa vigumu mno kwa mwili wa binadamu kuhimili bubujiko la hewa ambalo lingezalishwa na mzunguko wa dunia na mwendo wa vitu vyote katika spidi fulani. Ingekuwa vigumu zaidi kustahimili. Ingekuwa hivyo, hili bubujiko la hewa halingeleta tu madhara kwa wanadamu, bali uharibifu. Hakuna ambaye angeweza kuendelea kuishi katika mazingira hayo. Ndio maana Mungu hutumia mazingira ya kijiografia mbalimbali kutatua aina hiyo ya bubujiko za hewa, kudhoofisha bubujiko za hewa kama hizo kwa kubadilisha mwelekeo, spidi na nguvu zake kupitia kwa mazingira mbalimbali. Ndio maana watu wanaweza kuona mazingira ya jiografia mbalimbali, kama vile milima, safu za milima, tambarare, vilima, vidimbwi, mabonde, uwanda wa juu, na mito. Mungu hutumia haya mazingira mbalimbali ya jiografia kubadilisha spidi, mwelekeo na nguvu za bubujiko la hewa, akitumia mbinu kama hiyo kupunguza au kuiendesha kuwa spidi ya upepo, mwelekeo wa upepo, na nguvu za upepo zinazofaa, ili wanadamu waweze kuwa na mazingira ya kuishi ya kawaida. Je, ni lazima kufanya hivyo? (Ndiyo.) Kufanya jambo kama hilo kunaonekana kuwa vigumu kwa wanadamu, lakini ni rahisi kwa Mungu kwa sababu Anaangalia kwa makini vitu vyote. Kwa Yeye kuumba mazingira yenye bubujiko la hewa linalofaa wanadamu ni kitu sahili sana, rahisi sana. Kwa hiyo, katika mazingira kama hayo yaliyoumbwa na Mungu, kila kitu na vitu vyote miongoni mwa vitu vyote ni vya lazima. Kuna thamani na umuhimu katika kila kuwepo kwa vitu hivyo. Hata hivyo, Shetani na wanadamu wapotovu hawaelewi aina hiyo ya falsafa. Wanaendelea kuharibu na kukuza, wakiota bure juu ya kugeuza milima kuwa ardhi tambarare, kujaza korongo kuu, na kujenga magorofa juu ya ardhi tambarare kuunda misitu ya saruji. Ni matumaini ya Mungu kwamba wanadamu wataishi kwa furaha, kukua kwa furaha, na kutumia kila siku kwa furaha katika mazingira ya kufaa zaidi Aliyowatayarishia. Ndiyo maana Mungu hajawahi kuwa mzembe inapohusu kushughulikia mazingira ya kuishi ya wanadamu. Kutoka kwa halijoto mpaka kwa hewa, kutoka kwa sauti mpaka kwa nuru, Mungu amefanya mipango na utaratibu tatanishi, ili mazingira ya kuishi ya wanadamu na miili yao visiweze kupatwa na kuharibiwa kokote kutoka kwa hali za asili, na badala yake wanadamu waweze kuishi na kuongezeka kawaida na kuishi na vitu vyote kawaida kwa kuishi pamoja kwa amani yenye kuridhisha. Hii yote inapeanwa na Mungu kwa vitu vyote na wanadamu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp