Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 319

Nyinyi nyote mna furaha kupokea tuzo mbele ya Mungu na kutambuliwa na Mungu. Haya ni matakwa ya kila mtu baada ya yeye kuanza kuwa na imani kwa Mungu, kwani mwanadamu kwa moyo wake wote hutafuta mambo yaliyo juu na hakuna aliye tayari kubaki nyuma ya wengine. Hii ndiyo njia ya mwanadamu. Kwa sababu hii, wengi kati yenu wanajaribu daima kupata neema ya Mungu mbinguni, lakini kwa kweli, uaminifu wenu na uwazi kwa Mungu ni wa kiasi kidogo sana ukilinganishwa na uaminifu na uwazi wenu kwenu wenyewe. Mbona Nasema hivi? Kwa sababu Sikiri uaminifu wenu kwa Mungu kabisa, na zaidi Nakana kuwepo kwa Mungu ndani ya mioyo yenu. Hiyo ni kusema, Mungu mnayemwabudu, Mungu asiye dhahiri mnayempenda, hayupo kabisa. Kinachonifanya niseme haya kwa uhakika ni kwamba mko mbali sana na Mungu wa kweli. Uaminifu mnaomiliki unatokana na kuishi kwa sanamu nyingine mioyoni mwenu, na kunihusu Mimi, Mungu anayechukuliwa kama asiye mkubwa wala mdogo ndani ya macho yenu, hamnitambui na chochote ila maneno. Ninaposema juu ya umbali wenu kutoka kwa Mungu, Ninamaanisha jinsi mlivyo mbali na Mungu wa kweli, ilhali Mungu asiye dhahiri Anaonekana kuwa karibu. Nisemapo “asiye mkubwa,” inamaanisha jinsi Mungu mnayemwamini siku ya leo anaonekana tu kuwa mwanadamu asiye na uwezo wa nguvu; mwanadamu asiye bora sana. Na Nisemapo, “asiye mdogo,” inamaanisha kuwa ingawa mwanadamu huyu hawezi kuita upepo na kuamuru mvua, Anaweza kumwita Roho wa Mungu kufanya kazi inayotingisha mbingu na dunia, hivyo kumchanganya mwanadamu. Kwa nje, nyote mnaonekana kuwa watiifu kwa huyu Kristo aliye duniani, lakini kwa kiini hamna imani Kwake wala kumpenda. Ninachomaanisha ni kwamba yule mliye na imani kwake kwa kweli ni yule Mungu asiye dhahiri katika hisia zenu, na yule kweli mnayempenda ni Mungu mnayemtamani usiku na mchana, lakini bado hamjamwona kamwe kibinafsi. Na kwa huyu Kristo, imani yenu ni sehemu tu, na upendo wenu Kwake si kitu. Imani inamaanisha imani na tumaini; upendo unamaanisha kuabudu na kusifu ndani ya mioyo yenu, bila kuondoka. Lakini imani yenu na upendo wenu kwa Kristo wa siku ya leo vimepunguka chini ya hili. Ikujapo kwa imani, mna imani Kwake jinsi gani? Ikujapo kwa upendo, mnampenda jinsi gani? Hamjui chochote kuhusu tabia Yake, wala hata kiini Chake, hivyo ni jinsi gani kwamba mna imani Kwake? Uko wapi ukweli wa imani yenu Kwake? Mnampenda jinsi gani? Uko wapi ukweli wa upendo wenu Kwake?

Wengi wamenifuata bila kusita hadi leo, na kwa miaka hii, nyote mmeteseka sana uchovu mwingi. Nimefahamu vizuri tabia na mazoea ya kila mmoja wenu. Ilikuwa vigumu sana kushirikiana nanyi. Cha huruma ni kwamba ingawa nina maarifa nyingi kuwahusu, hamna ufahamu hata kidogo kunihusu. Sio ajabu wengine wanasema mlidanganywa na mwanadamu katika wakati wa mkanganyiko. Hakika, hamwelewi chochote kuhusu tabia Yangu, na hata chini zaidi hamwezi kufahamu yaliyo akilini Mwangu. Sasa kutoelewana kwenu Kwangu ni kuongeza chumvi kwenye jeraha, na imani yenu Kwangu inabaki ile ya mkanganyiko. Badala ya kusema mna imani na Mimi, ingekuwa bora kusema kwamba nyote mnajaribu kupata neema Yangu na kujipendekeza Kwangu. Nia zenu ni rahisi—yeyote anayeweza kunituza, nitamfuata, na yeyote anayeweza kuniwezesha kutoroka majanga makubwa, nitaamini kwake, awe Mungu ama Mungu fulani yeyote. Hakuna kati ya haya yanayonihusu. Kuna wanadamu wengi kama hao kati yenu, na hali hii ni nzito sana. Ikiwa siku moja, majaribio yatafanywa kuona wangapi kati yenu wanamwamini Mungu kwa sababu mna umaizi kuhusu kiini Chake, basi Nahofia kwamba hakuna mmoja wenu atakuwa Ninavyotamani. Hivyo haitakuwa hoja kwa kila mmoja wenu kuzingatia swali hili: Mungu mliye na imani na Yeye ni tofauti sana na Mimi, hivyo nini basi ni kiini cha imani yenu kwa Mungu? Kadri mnavyoamini katika mnayemwita Mungu wenu, ndivyo mnavyozidi kupotea mbali sana Nami. Nini, basi, ni msingi wa suala hili? Nina uhakika hakuna mmoja wenu amewahi kufikiria suala hili, lakini mmefikiria uzito wake? Mmetoa mawazo kwa matokeo ikiwa mtaendelea na namna hii ya imani?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jinsi ya Kumjua Mungu Duniani

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp