Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 77
Kufufuka kwa Lazaro Kwampa Mungu Utukufu Yohana 11:43-44 Na baada ya yeye kuzungumza, akasema kwa sauti kuu, Lazaro, kuja nje. Na yeye...
Tunawakaribisha watafutaji wote wanaotamani sana kuonekana kwa Mungu!
Maisha yako yakiendelea, lazima daima uwe na kiingilio kipya na ufahamu mpya na wa juu zaidi, unaokua kwa kina na kila hatua. Hiki ndicho wanadamu wote wanapaswa kuingia ndani. Kupitia kuwasiliana, kusikiza ujumbe, kusoma neno la Mungu, ama kushughulikia suala, utapata ufahamu mpya na kupata nuru upya. Huishi ndani ya kanuni za zamani na nyakati za zamani. Unaishi milele ndani ya mwangaza mpya, na hupotei mbali na neno la Mungu. Hii ndiyo inafikiriwa kuwa kwa njia sawa. Kulipa tu gharama ya juu juu hakutasaidia. Neno la Mungu linakuwa juu zaidi na mambo mapya yanajitokeza kila siku. Ni muhimu pia kwa mwanadamu kuingia upya kila siku. Mungu anavyozungumza, ndivyo Anatimiza yote ambayo Amezungumzia; kama huwezi kwenda sambamba, basi unalegea nyuma. Maombi yako lazima yawe ya kina; lazima ule na kunywa zaidi neno la Mungu, kuimarisha ufunuo unaopokea, na kupunguza mambo ambayo ni hasi. Lazima uimarishe hekima yako ili uweze kupata ufahamu, na kwa kuelewa kile kilicho kwa roho, kupata ufahamu wa mambo ya nje na kuelewa kiini cha suala lolote. Kama huna sifa kama hizi, utawezaje kuliongoza kanisa? Iwapo unazungumzia tu barua na mafundisho ya dini bila uhalisi wowote na bila njia ya kutenda, unaweza tu kuendelea kwa muda mfupi. Inaweza kukubaliwa kidogo kwa waumini wapya, lakini baada ya muda, wakati waumini wapya wanapata tajriba halisi, basi hutaweza tena kuwasambazia. Basi unafaa aje kwa matumizi ya Mungu? Huwezi kufanya kazi bila kupata nuru upya. Walio bila kupata nuru upya ni wale wasiojua jinsi ya kuwa na uzoefu, na wanadamu kama hao kamwe hawapati elimu mpya ama tajriba. Na hawawezi kamwe kufanya jukumu lao la kusambaza uhai, wala hawawezi kufaa kwa ajili ya matumizi na Mungu. Mwanadamu kama huyu ni dhaifu na hana maana. Kwa kweli, wanadamu kama hawa hawawezi kufanya jukumu lao kabisa kwa kazi na wote hawana faida. Wanashindwa kufanya jukumu lao na pia kwa kweli wanaweka mzigo mwingi usiohitajika juu ya kanisa. Nawahimiza hawa “wanaume wazee” kuharakisha na kuondoka kanisani ili wengine wasilazimishwe kuwaona tena. Wanaume kama hawa hawaelewi kazi mpya lakini wamejawa na dhana. Hawafanyi chochote kanisani; badala, wanachochea na kusambaza asili hasi, hata kushiriki katika kila namna ya utovu wa nidhamu na vurugu kanisani, na hivyo kuwarusha wale wasiobagua katika vurugu na machafuko. Haya mashetani hai, haya mapepo mabaya wanapaswa kuondoka kanisani haraka iwezekanavyo, isije kanisa likaharibiwa kama matokeo. Labda huogopi kazi ya leo, lakini huogopi adhabu ya haki ya kesho? Kuna idadi kubwa ya watu kanisani ambao ni vimelea, na pia kuna mbwa mwitu wengi wanaotaka kuvuruga kazi asili ya Mungu. Hawa wote ni mapepo yaliyotumwa na Ibilisi na ni mbwa mwitu wakali wanaotaka kuwala kondoo wasio na hatia. Kama hawa wanaodaiwa kuwa wanadamu hawatafukuzwa, basi wanakuwa vimelea kwa kanisa na nondo wanaokula sadaka. Hawa nondo wanaochukiza, wajinga, wabaya, na makuruhu wataadhibiwa siku moja karibuni!
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Wanaomtii Mungu kwa Moyo wa Kweli Hakika Watapatwa na Mungu
Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?
Kufufuka kwa Lazaro Kwampa Mungu Utukufu Yohana 11:43-44 Na baada ya yeye kuzungumza, akasema kwa sauti kuu, Lazaro, kuja nje. Na yeye...
Watu wengi huyashika maneno ya Mungu kuyasoma siku baada ya siku, kiasi kwamba wanaviweka akilini vifungu vyote maarufu humo kama vitu vyao...
Mungu anakuwa mwili bila nia ya kumfanya mwanadamu apate kuujua mwili Wake, ama kukubali mwanadamu kutofautisha tofauti kati ya mwili wa...
Kutoka kwa tofauti katika kiini cha Paulo na kiini cha Petro unapaswa kufahamu kuwa wale wote ambao hawafuati uzima wanafanya kazi ya bure!...