Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 399

Maneno ya Roho Mtakatifu leo ni nguvu za kazi ya Roho Mtakatifu, na kuendelea kwa Roho Mtakatifu kumpa nuru mwanadamu wakati wa kipindi hiki ni mwelekeo wa kazi ya Roho Mtakatifu. Na mwelekeo ni upi katika kazi ya Roho Mtakatifu leo? Ni uongozi wa watu ndani ya kazi ya Mungu leo, na ndani ya maisha ya kiroho ya kawaida. Kuna hatua kadhaa za kuingia katika maisha ya kiroho ya kawaida:

1. Kwanza, lazima uumimine moyo wako ndani ya maneno ya Mungu. Lazima usiyafuatilie maneno ya Mungu katika siku za zamani, na lazima usiyasome wala kuyafananisha na maneno ya sasa. Badala yake, lazima uumimine moyo wako kabisa katika maneno ya sasa ya Mungu. Kama kuna watu ambao bado wangependa kuyasoma maneno ya Mungu, vitabu vya kiroho, au maelezo mengine ya mahubiri kutoka kwa siku za zamani, ambao hawafuati maneno ya Roho Mtakatifu leo, basi wao ni wapumbavu zaidi ya watu wote; Mungu huchukia sana watu kama hao. Kama uko radhi kukubali nuru ya Roho Mtakatifu leo, basi mimina moyo wako kabisa katika matamshi ya Mungu leo. Hili ni jambo la kwanza ambalo lazima utimize.

2. Lazima uombe juu ya msingi wa maneno yaliyonenwa na Mungu leo, uingie ndani ya maneno ya Mungu na uwasiliane kwa karibu na Mungu, na ufanye maazimio yako mbele ya Mungu, ni viwango vipi ambavyo ungependa kufuatilia ufanikishaji wake.

3. Lazima ufuatilie kuingia kwa maana sana ndani ya ukweli juu ya msingi wa kazi ya Roho Mtakatifu leo. Usishikilie matamshi na nadharia zilizopitwa na wakati kutoka zamani.

4. Lazima utafute kuguswa na Roho Mtakatifu, na kuingia katika maneno ya Mungu.

5. Lazima ufuatilie kuingia katika njia ambayo Roho Mtakatifu anatembea leo.

Na ni vipi ambavyo wewe hutafuta kuguswa na Roho Mtakatifu? Kilicho muhimu ni kuishi ndani ya maneno ya sasa ya Mungu, na kuomba juu ya msingi wa masharti ya Mungu. Baada ya kuomba kwa njia hii, Roho Mtakatifu kwa kweli atakugusa. Kama hutafuti kwa kutegemea msingi wa maneno yaliyonenwa na Mungu leo, basi hili ni bure. Unapaswa kuomba, na kusema: “Ee Mungu! Mimi hukupinga Wewe, na unanidai Mimi mengi sana; mimi ni mkaidi sana, na siwezi kamwe kukuridhisha Wewe. Ee Mungu, natamani Wewe uniokoe, natamani kukupa Wewe huduma hadi mwisho kabisa, natamani kufa kwa ajili Yako. Wewe hunihukumu na kuniadibu, na sina malalamiko; mimi hukupinga Wewe na nastahili kufa, ili watu wote waweze kutazama tabia Yako yenye haki katika kifo changu.” Wakati ambapo wewe huomba kutoka moyoni mwako kwa njia hii, Mungu atakusikia, na atakuongoza; kama huombi juu ya msingi wa maneno ya Roho Mtakatifu leo, basi hakuna uwezekano wa Roho Mtakatifu kukugusa wewe. Kama wewe huomba kwa kadri ya mapenzi ya Mungu, na kwa kadri ya kile ambacho Mungu hutaka kufanya leo, utasema: “Ee Mungu! Nataka kukubali maagizo Yako na kuwa mwaminifu kwa maagizo Yako, na niko radhi kuyatoa maisha yangu yote kwa utukufu Wako, ili yote nifanyayo yaweze kufikia kiwango cha watu wa Mungu. Moyo wangu na uweze kuguswa na Wewe. Nataka Roho Wako anipe nuru wakati wowote, kusababisha yote nifanyayo yalete aibu kwa Shetani, ili hatimaye nipatwe na Wewe.” Kama wewe huomba kwa njia hii, ukilenga mapenzi ya Mungu, basi Roho Mtakatifu atafanya kazi ndani yako bila kuzuilika. Haijalishi maneno ya maombi yako ni mangapi—kilicho muhimu ni kama unaelewa mapenzi ya Mungu au la. Huenda ninyi nyote mmekuwa na tukio lifuatalo: Wakati mwingine, ukiwa unaomba katika kusanyiko, nguvu za kazi ya Roho Mtakatifu hufikia kilele chake, kusababisha nguvu za kila mtu kuongezeka. Watu wengine hulia kwa uchungu na kutoa machozi huku wakiomba, kwa kulemewa na majuto mbele ya Mungu, na watu wengine huonyesha azimio lao, na kuweka nadhiri. Hiyo ndiyo athari ya kutimizwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Leo, ni ya muhimu sana kwamba watu wote wamimine mioyo yao kabisa ndani ya maneno ya Mungu. Usisisitize kwa maneno yaliyonenwa awali; kama bado unashikilia kilichokuja awali, basi Roho Mtakatifu hatafanya kazi ndani yako. Je, waona vile hili ni muhimu?

Je, mnajua njia ambayo Roho Mtakatifu hutembea leo? Mawazo makuu kadhaa hapo juu ni kile kitakachotimizwa na Roho Mtakatifu leo na katika siku za baadaye; ni njia inayofuatwa na Roho Mtakatifu, na kuingia ambako kunapaswa kufuatiliwa na mwanadamu. Katika kuingia kwako maishani, kwa kiasi kidogo sana lazima umimine moyo wako ndani ya maneno ya Mungu, na uweze kukubali hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu; moyo wako lazima uwe na shauku kwa Mungu, lazima ufuatilie kuingia kwa maana sana katika ukweli, na malengo ambayo Mungu hutaka. Wakati ambapo unakuwa na nguvu hizi, basi hilo huonyesha kuwa umeguswa na Mungu, na moyo wako umeanza kuelekea kwa Mungu.

Hatua ya kwanza ya kuingia katika uzima ni kuumimina moyo wako kabisa ndani ya maneno ya Mungu, na hatua ya pili ni kukubali kuguswa na Roho Mtakatifu. Ni nini athari ya kutimizwa kwa kukubali kuguswa na Roho Mtakatifu? Kuweza kuwa na shauku ya, kutafuta, na kuchunguza ukweli wa maana sana, na kuwa na uwezo wa kushirikiana na Mungu katika njia nzuri. Leo, wewe hushirikiana na Mungu, ambalo ni kusema kuna lengo kwa ukimbizaji wako, kwa maombi yako, na kwa mawasiliano yako ya maneno ya Mungu, na wewe hutekeleza wajibu wako kwa mujibu wa masharti ya Mungu—huku pekee ndiko kushirikiana na Mungu. Ukizungumza tu kuhusu kumwacha Mungu atende, lakini usichukue hatua yoyote, wala kuomba au kutafuta, basi hili lingeweza kuitwa ushirikiano? Kama huna chochote kuhusu ushirikiano ndani yako, na umeondolewa mafunzo ya kuingia ambayo yana lengo, basi wewe hushirikiani? Watu wengine husema: “Kila kitu hutegemea majaaliwa ya Mungu, yote hufanywa na Mungu mwenyewe: kama Mungu hangelifanya, basi mwanadamu angewezaje?” Kazi ya Mungu ni ya kawaida, na siyo ya rohoni hata kidogo, na ni kupitia tu kwa utafutaji wako wa utendaji ndiyo Roho Mtakatifu hufanya kazi, kwani Mungu hamlazimishi mwanadamu—lazima umpe Mungu nafasi ya kufanya kazi, na kama hufuatilii au kuingia, na kama hakuna shauku hata kidogo ndani ya moyo wako, basi Mungu hana nafasi ya kufanya kazi. Ni kwa njia ipi ndio unaweza kutafuta kuguswa na Mungu? Kupitia maombi, na kuja karibu na Mungu. Lakini la muhimu zaidi, kumbuka, lazima iwe juu ya msingi wa maneno yanayonenwa na Mungu. Wakati ambapo unaguswa mara kwa mara na Mungu, hutawaliwi kabisa na mwili: Mume, mke, watoto, na pesa—yote ni yasiyoweza kukufunga wewe, na wewe hutamani kufuatilia tu ukweli na kuishi mbele ya Mungu. Wakati huu, utakuwa mtu anayeishi katika eneo la uhuru.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jua Kazi Mpya Zaidi ya Mungu na Ufuate Nyayo Zake

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp