Mwenyezi Mungu na Kanisa la Mwenyezi Mungu

Makala 5

Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake

Kama wale mamia ya mamilioni ya wengine wanaomfuata Bwana Yesu Kristo, tunafuata sheria na amri za Biblia, kufurahia neema tele ya Bwana Yesu Kristo, na kukusanyika pamoja, kuomba, kusifu, na kuhudumu kwa jina la Bwana Yesu Kristo—na haya yote sisi hufanya chini ya utunzaji na ulinzi wa Bwana.

09/06/2017

Utangulizi Mfupi Kuhusu Usuli wa Kuonekana kwa Kazi ya Kristo wa Siku za Mwisho Nchini China

China ni nchi ambamo joka kubwa jekundu hukaa, na ni mahali ambapo pamempinga na kumshutumu Mungu zaidi sana katika historia. China ni kama ngome ya mapepo na gereza linalodhibitiwa na shetani, lisilopenyeka na lisiloingilika. Zaidi ya hayo, utawala wa joka kubwa jekundu husimama ukilinda katika ngazi zote na umeanzisha ulinzi katika kila kaya. Matokeo yake, hakuna mahali pagumu zaidi ya hapa kueneza injili ya Mungu na kufanya kazi ya Mungu. Wakati Chama cha Kikomunisti Cha China kiliposhika madaraka mwaka wa 1949, imani za kidini katika China bara zilizimwa kabisa na kupigwa marufuku. Mamilioni ya Wakristo walipitia mateso na fedheha hadharani, na kifungo. Makanisa yote yalifungwa kabisa na kufutiliwa mbali. Hata mikutano ya nyumbani ilipigwa marufuku. Iwapo mtu yeyote alibambwa akishiriki mkutano, angetiwa gerezani na hata angekatwa kichwa. Wakati huo, shughuli za kidini karibu zitoweke bila kupatikana. Ni idadi ndogo tu ya Wakristo iliendelea kuamini katika Mungu, lakini wangeweza tu kumwomba Mungu kimyakimya na kuimba nyimbo za sifa kwa Mungu katika mioyo yao, wakimwomba Mungu kufufua kanisa. Hatimaye, katika mwaka wa 1981, kanisa lilifufuka kwa dhati, na Roho Mtakatifu akaanza kazi kwa kiasi kikubwa katika China. Makanisa yakachipuka kama machipukizi ya mianzi baada ya mvua ya majira ya kuchipua, na watu zaidi na zaidi wakaanza kuamini katika Mungu. Katika mwaka wa 1983, wakati uamshaji wa kanisa ulifika kilele chake, Chama cha Kikomunisti Cha China kikaanza duru mpya ya ukandamizaji wa kikatili. Mamilioni ya watu walikamatwa, wakawekwa kizuizini, na kuelimishwa kwa njia ya kazi. Utawala wa joka kubwa jekundu uliwaruhusu waumini katika Mungu kujiunga tu na Kanisa la Nafsi Tatu la Kizalendo (Three-Self Patriotic Church) lililoanzishwa na serikali. Serikali ya Chama cha Kikomunisti Cha China (CCP) lilianzisha Kanisa la Nafsi Tatu la Kizalendo (Three-Self Patriotic Church) katika jaribio la kuzima kanisa la siri la nyumbani na kuwaleta wale waumini wa Bwana imara chini ya utawala wa serikali. Iliamini kwamba hii ilikuwa njia pekee ya kufikia lengo lake la kupiga marufuku imani na kugeuza China kuwa nchi isiyokuwa na Mungu. Lakini Roho Mtakatifu aliendelea kufanya kazi nyingi katika kanisa la nyumbani na katika wale ambao kweli waliamini katika Mungu, ambao serikali ya CCP ilishindwa kuwakomesha. Wakati huo, katika kanisa la nyumbani ambapo Roho Mtakatifu alifanya kazi, Kristo wa siku za mwisho kwa siri Alionekana Akifanya kazi, na kuanza kuonyesha ukweli na kufanya kazi ya hukumu Akianza na nyumba ya Mungu.

09/06/2017

Asili na Maendeleo ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu lilikuja kuwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu—Bwana Yesu aliyerudi—Kristo wa siku za mwisho, na pia chini ya hukumu Yake ya haki na kuadibu. Kanisa limejumuisha wale wote ambao wanaikubali kwa kweli kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho na wameshindwa na kuokolewa na neno la Mungu. Liliasisiwa kabisa na Mwenyezi Mungu mwenyewe, na linaongozwa na kuchungwa binafsi na Yeye, na kamwe halikuanzishwa na mtu yeyote. Huu ni ukweli unaokubaliwa na watu wote waliochaguliwa katika Kanisa la Mwenyezi Mungu.

09/06/2017

Kueneza kwa Injili ya Ufalme wa Mwenyezi Mungu Nchini China

Mwaka wa 1995, kazi ya kushuhudia kwa injili ya ufalme ya Mwenyezi Mungu ilianza rasmi China Bara. Kwa njia ya shukrani kwa Mungu na kwa upendo ambao ulikuwa wa kweli, tulishuhudia kwa kuoenekana na kazi ya Mwenyezi Mungu kwa ndugu wa kiume na kike katika madhehebu mbalimbali na makundi ya kidini. Hatukutarajia hata kidogo kukumbwa na upinzani na kukashifiwa kulikokithiri kutoka kwa viongozi wao. Tungeweza tu kuja mbele ya Mwenyezi Mungu kusali kwa ari, tukimsihi Mungu kufanya kazi binafsi. Kutoka 1997 na kuendelea, tulimwona Roho Mtakatifu akifanya kazi kwa kiwango kikubwa. Kulikuwa na ongezeko la haraka la washirika wa makanisa katika maeneo mbalimbali. Wakati huo huo, ishara nyingi na maajabu vilitokea, na watu wengi katika madhehebu mbalimbali na makundi ya kidini yakarudi kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu ya kupokea ufunuo au kuona hizi ishara na maajabu. Kama Roho Mtakatifu hangekuwa amefanya kazi, mtu angefanya nini? Hili lilitufanya kutambua: Ingawa tulielewa baadhi ya ukweli, hatungeweza kutoa ushuhuda kwa Mwenyezi Mungu kwa nguvu zetu za kibinadamu pekee. Baada ya watu hawa kutoka madhehebu mbalimbali na makundi ya kidini kumkubali Mwenyezi Mungu, wao hatua kwa hatua walipata uhakika wa Mwenyezi Mungu katika mioyo yao kupitia kula na kunywa na kufurahia neno la Mwenyezi Mungu, na baada ya muda fulani, kulifanyika ndani yao imani halisi na utii. Watu kutoka kila dhehebu na kundi la kidini kwa hivyo waliinuliwa mbele ya kiti cha enzi, na hawakutarajiwa tena "kukutana na Bwana angani" kama walivyokuwa wamefikiri.

09/06/2017

Ole Wao Wale Wamsulubishae Mungu Mara Nyingine Tena

Katika siku za mwisho, Mungu amepata mwili katika nchi ya China kufanya kazi, na Ameonyesha mamilioni ya maneno, Akishinda na kuokoa kundi la watu kwa neno Lake na kuikaribisha enzi mpya ya hukumu ikianza na nyumba ya Mungu. Leo, kuenea kwa kazi ya Mungu katika siku za mwisho kumefikia kilele chake katika China Bara. Wengi wa watu katika Kanisa Katoliki na madhehebu yote ya Kikristo na makundi ya kidini ambayo yanafuatilia ukweli wamerudi mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Mungu mwenye mwili Amekamilisha kazi ya "ujio wa siri wa Mwana wa Adamu" Aliyetabiriwa katika Biblia, na hivi karibuni Ataonekana kwa umma katika kila taifa na sehemu ulimwenguni. Watu wote katika kila taifa na sehemu walio na kiu cha kuonekana kwa Mungu watatarajia kuonekana kwa Mungu hadharani. Hakuna nguvu zinazoweza kuzuia au kuangamiza ufalme wa Mungu, na mtu yeyote ambaye anapinga Mungu ataadhibiwa na ghadhabu ya Mungu, kama vile inavyosemwa katika maneno ya Mungu: “Ufalme Wangu unaenea katika ulimwengu mzima, na kiti Changu cha enzi kimenyakua mioyo ya matrilioni ya watu. Kwa usaidizi wa malaika wa mbinguni, utimilifu Wangu mkuu utakamilika hivi karibuni. Halaiki zote za Wanangu na watu Wangu, wanangoja kwa hamu kurejea Kwangu, wakitarajia kuunganishwa Kwangu nao, tusije tukatengana tena. Itawezekanaje watu wote wa ufalme Wangu wasikimbie wakifurahiana kila mmoja kwa kuunganika pamoja na Mimi tena? Inawezekana huu uwe muungano usio na gharama? Mimi Ninaheshimiwa machoni pa kila mtu, Ninadhihirika katika maneno ya kila mtu. Nitakaporejea, Nitashinda nguvu zote za adui mara tena. Wakati umewadia! Ninataka kazi Yangu ianze, Ninataka kuwa kiongozi mkuu juu ya mwanadamu! Tazama, Ninarejea! Ninaondoka! Hili ndilo kila mmoja anatarajia, ndilo kila mmoja anatumainia. Nataka kila mmoja ashuhudie kufika kwa siku Yangu na aikaribishe siku Yangu kwa furaha tele!” "Wale wote ambao Nawapenda wataishi milele kwa hakika, na wale wote wanaosimama dhidi Yangu wataadhibiwa na Mimi milele kwa hakika. Kwani Mimi ni Mungu mwenye wivu, Sitawasamehe kwa urahisi wanadamu kwa kile watakachokuwa wametenda. Nitaiangalia dunia yote, na, Nikitokea Mashariki ya dunia na haki, adhama, gadhabu, na adhabu, Nitajionyesha binafsi kwa wanadamu wengi wa tabaka mbalimbali!"

09/06/2017

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp