Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 302
Chanzo cha ufunuo wa upotovu wa tabia ya mwanadamu ni dhamiri yake iliyofifia, asili yake mbovu na akili yake isiyo timamu; kama dhamiri ya...
Tunawakaribisha watafutaji wote wanaotamani sana kuonekana kwa Mungu!
Matamshi na kazi ya Yesu wakati huo hayakushikilia mafundisho, na hakufanya kazi Yake kulingana na kazi ya sheria ya Agano la Kale. Yalilingana na kazi iliyopaswa kufanywa kwa Enzi ya Neema. Alitenda kulingana na kazi Aliyokuwa ameleta mbele, kulingana na mipango Yake, na kulingana na huduma Yake; Hakufanya kazi kulingana na sheria ya Agano la Kale. Hakuna Alichofanya kilicholingana na Agano la Kale, na Hakuja kufanya kazi ili kutimiza maneno ya manabii. Kila hatua ya kazi ya Mungu haikuwa wazi ili kutimiza utabiri wa manabii wa zamani, na Hakuja kuyafuata mafundisho au kutambua makusudi utabiri wa manabii wa kale. Bado vitendo Vyake havikuvuruga utabiri wa manabii wa kale, wala havikuvuruga kazi Aliyokuwa amefanya awali. Hatua muhimu ya kazi Yake haikuwa kufuata mafundisho yoyote, na kufanya kazi ambayo Yeye Mwenyewe anapaswa kufanya. Yeye hakuwa nabii wala mwaguzi, ila mtendaji, aliyekuja kufanya hiyo kazi Aliyopaswa kufanya, na aliyekuja kufungua enzi Yake mpya na kufanya kazi Yake mpya. Bila shaka, Yesu alipokuja kufanya kazi Yake, pia Alitimiza maneno mengi yaliyosemwa na manabii wa zamani kwa Agano la Kale. Hivyo pia kazi ya leo imetimiza utabiri wa manabii wa zamani wa Agano la Kale. Ni vile tu Sishikilii hiyo “kalenda njano ya zamani,” hayo tu. Kwani kuna kazi zaidi ambayo lazima Nifanye, kuna maneno zaidi ambayo lazima Niwazungumzie, na kazi hii na maneno haya ni ya umuhimu mkubwa kuliko kueleza vifungu kutoka Biblia, kwa sababu kazi kama hiyo haina maana ama thamani kubwa kwenu, na haiwezi kuwasaidia, au kuwabadilisha. Ninanuia kufanya kazi mpya sio kwa ajili ya kutimiza kifungu chochote kutoka Biblia. Ikiwa Mungu alikuja duniani tu kutimiza maneno ya manabii wa Biblia, basi ni nani aliye mkuu, Mungu wa mwili ama hao manabii wa zamani. Na hata hivyo, hao manabii ni wasimamizi wa Mungu, ama Mungu ni msimamizi wa manabii? Unaweza kueleza haya maneno jinsi gani?
Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuhusu Majina na Utambulisho
Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?
Chanzo cha ufunuo wa upotovu wa tabia ya mwanadamu ni dhamiri yake iliyofifia, asili yake mbovu na akili yake isiyo timamu; kama dhamiri ya...
Mtazamo na Matendo Bora ya Mtu Anayependa Kujinyenyekeza katika Mamlaka ya Mungu Mwanadamu anatakiwa kuwa na mtazamo gani sasa katika kujua...
Kutoka juu hadi chini na kuanzia mwanzo hadi mwisho, Shetani amekuwa akiisumbua kazi ya Mungu na kutenda kinyume na Yeye. Mazungumzo yote...
Watu wote wana tamaa ya kuona uso wa kweli wa Yesu na wote hutaka kuwa pamoja Naye. Naamini kuwa hakuna mmoja wa ndugu au dada anayeweza...