Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 150

Kwanza Mungu alimwumba Adamu na Hawa, na pia Alimwumba nyoka. Miongoni mwa mambo haya yote, nyoka ndiye aliyekuwa mwenye sumu zaidi; mwili wake ulikuwa na sumu, na Shetani aliitumia sumu hiyo ili kufaidika. Ni nyoka aliyemjaribu Hawa hadi akatenda dhambi. Adamu alitenda dhambi baada ya Hawa kutenda, na wawili hawa waliweza kutofautisha kati ya mema na maovu. Kama Yehova Alikuwa Amejua kwamba nyoka angemjaribu Hawa, na kwamba Hawa angemjaribu Adamu, kwa nini Akawaweka wote pale katika bustani? Kama Aliweza kutabiri mambo haya kwa nini Akamwumba nyoka na kumweka ndani ya Bustani ya Edeni? Kwa nini Bustani ya Edeni ilikuwa na tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya? Alinuia wao walile hilo tunda? Wakati Yehova alipokuja, Adamu wala Hawa hawakuthubutu kumkabili Yeye, na ulikuwa tu wakati huu ambapo Yehova alijua kwamba walikuwa wamelila tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya na kujipata katika ujanja wa yule nyoka. Hatimaye Alimlaani nyoka, na Akamlaani Adamu na Hawa. Yehova hakuwa na habari wakati wawili hawa walipolila tunda lile la mti. Binadamu walipotoka hadi kufikia kiwango cha kuwa na uovu na uasherati wa kimapenzi, hadi kufikia awamu ya mambo haya yote waliyoyahifadhi katika mioyo yao yakawa maovu na yasiyo ya haki; yote yalikuwa machafu. Yehova hivyo basi alijutia kwa kuumba binadamu. Baadaye Alitekeleza kazi Yake ya kuharibu ulimwengu kwa gharika, ambayo Nuhu na watoto wake wa kiume walinusurika. Baadhi ya mambo kwa hakika hayajaendelea na kuzidi maumbile ya kawaida kama vile watu wanavyoweza kufikiria. Baadhi wanauliza: Kwa sababu Mungu alijua malaika mkuu angemsaliti Yeye, kwa nini alimwumba? Hizi ndizo hoja: Wakati nchi haikuwepo, malaika mkuu ndiye aliyekuwa malaika mkuu zaidi mbinguni. Alikuwa na mamlaka juu ya malaika wote kule mbinguni; haya ndiyo yaliyokuwa mamlaka ambayo Mungu alimpa. Kando na Mungu, ndiye aliyekuwa malaika mkubwa zaidi mbinguni. Wakati Mungu alipouumba binadamu baadaye, malaika mkuu alitekeleza usaliti mkuu zaidi dhidi ya Mungu nchini. Nasema kwamba alimsaliti Mungu kwa sababu alitaka kuwasimamia binadamu na kumzidi Mungu katika mamlaka. Ni malaika mkuu ambaye alimjaribu Hawa hadi akatenda dhambi; alifanya hivyo kwa sababu alipenda kuanzisha ufalme wake nchini na kuwafanya binadamu kumsaliti Mungu na kumtii badala yake. Aliona kwamba kulikuwa na vitu vingi ambavyo vilimtii; malaika walimtii sawa na vile ambavyo watu walivyomtii duniani. Ndege na wanyama, miti, misitu, milima, mito na viumbe vyote vilivyo nchini vilikuwa katika utunzaji wa binadamu—yaani, Adamu na Hawa—huku nao Adamu na Hawa wakimtii. Malaika mkuu hivyo basi alitamani kuzidi mamlaka ya Mungu na kumsaliti Mungu. Baadaye aliwaongoza malaika wengi kumsaliti Mungu, ambao baadaye walikuja kuwa pepo wachafu mbalimbali. Je, huoni kwamba maendeleo ya binadamu hadi siku ya leo yamesababishwa na upotoshaji wa malaika mkuu? Binadamu wako tu namna walivyo leo kwa sababu malaika mkuu alimsaliti Mungu na kuwapotosha binadamu. Kazi hii ya hatua kwa hatua haipo popote pale karibu na dhahania na nyepesi kama vile watu wanavyofikiria. Shetani alitekeleza usaliti wake kwa sababu fulani, ilhali watu hawawezi kufahamu kitu chepesi kama hicho. Kwa nini Mungu akaiumba mbingu na nchi na viumbe vyote, na pia kumwumba Shetani? Kwa sababu Mungu anamdharau Shetani sana, naye Shetani ni adui Wake, kwa nini akamwumba Shetani? Kwa kumwumba Shetani, hakuwa anamwumba adui? Mungu kwa hakika hakuumba adui; badala yake, Alimwumba malaika, na baadaye malaika akamsaliti Yeye. Hadhi yake ilikuwa kubwa mno kiasi cha kwamba alitaka kumsaliti Mungu. Mtu anaweza kusema kwamba hali hii ilikuwa ya sadfa, lakini ulikuwa pia mtindo usiokwepeka. Ni sawa na vile ambavyo mtu atakufa akiwa na umri fulani bila uwezo wa kuzuia hali hiyo; mambo yamefikia tayari katika awamu fulani. Kunao hata baadhi ya wale wa kipumbavu wanaosema: “Kwa sababu Shetani ni adui Yako, kwa nini Ukamwumba? Kwani hukujua kuwa malaika huyu mkuu angekusaliti Wewe? Kwani Huwezi kukazia macho kutoka kwa milele moja hadi nyingine? Kwani Wewe huijui asili yake? Kwa sababu ulijua waziwazi kuwa angekusaliti Wewe, basi kwa nini ukamfanya kuwa malaika mkuu? Hata kama mtu atapuuza suala la usaliti wake, aliweza bado kuwaongoza malaika wengi na akashuka hadi kwa ulimwengu wa binadamu wasiodumu ili kuwapotosha binadamu; hadi siku ya leo umeshindwa kukamilisha mpango Wako wa usimamizi wa miaka elfu sita.” Hayo ni kweli? Je, huoni kwamba unajiweka kwenye matatizo mengi zaidi kuliko inavyohitajika? Wengine bado husema: Kama Shetani asingewapotosha binadamu hadi siku ya leo, Mungu asingewaokoa binadamu kwa njia hii. Katika mfano huu, hekima na uweza wa Mungu vyote vingekuwa havionekani; hekima Yake ingewezaje kujionyesha? Hivyo basi Mungu alikiumba kizazi cha binadamu kwa minajili ya Shetani; katika siku za usoni, Mungu angefichua uweza Wake—vinginevyo, binadamu angewezaje kugundua hekima Yake? Kama binadamu asingempinga Yeye na kuchukua hatua ya kumwasi Yeye, isingehitajika kwa vitendo Vyake kujionyesha. Kama uumbaji wote ungemwabudu Yeye na kumtii Yeye, Asingekuwa na kazi ya kufanya. Hali hii nayo ni mbali zaidi na uhalisia wa mambo, kwani hakuna uchafu wowote kuhusu Mungu, na hivyo basi Hawezi kuumba uchafu. Yeye hufichua tu vitendo Vyake ili kuweza kuwashinda kabisa adui Zake, ili kuokoa binadamu, ambao aliuumba, ili kuyashinda mapepo na Shetani, ambao wanamchukia, wanamsaliti Yeye na wanampinga Yeye, ambao walikuwa katika utawala Wake na walimilikiwa na Yeye mwanzo kabisa; Anataka kuwashinda hawa mapepo na katika kufanya hivyo kuufichua uweza Wake kwa viumbe vyote. Binadamu na viumbe vyote vilivyomo nchini sasa hivi vimemilikiwa na Shetani na katika utawala wa waovu. Mungu anataka kuvifichua vitendo Vyake kwa viumbe vyote ili watu waweze kumjua Yeye, na hivyo kuishia kumshinda Shetani na kuangamiza kabisa adui Zake. Uzima wa kazi hii unakamilishwa kupitia matendo Yake yanayofichua. Viumbe Vyake vyote vimemilikiwa na Shetani, na hivyo basi Anapenda kuufichua uweza Wake kwa viumbe hivyo, kwa hivyo kumshinda Shetani. Kama Shetani asingekuwepo, Asingehitaji kuvifichua matendo Yake Kama usingekuwa unyanyasaji wa Shetani, angewaumba binadamu na kuuongoza kuishi katika Bustani ya Edeni. Kwa nini Hakuwahi kufichua vitendo Vyake vyote kwa malaika au malaika mkuu kabla ya kusalitiwa na Shetani? Kama malaika na malaika mkuu wangalimjua Yeye, na pia kumtii Yeye pale mwanzoni, basi Asingewahi kutekeleza vile vitendo vya kazi visivyo na maana. Kwa sababu ya uwepo wa Shetani na mapepo, watu humpinga na wanajazwa hadi pomoni na tabia ya uasi, na hivyo basi Mungu angependa kufichua vitendo Vyake. Kwa sababu Angependa kupigana vita na Shetani, lazima Atumie mamlaka Yake kumshinda Shetani na kutumia vitendo Vyake vyote kumshinda Shetani; kwa njia hii, kazi Yake ya wokovu Anayotekeleza miongoni mwa binadamu itawafanya watu waone hekima na uwezo Wake. Kazi anayofanya Mungu leo ni yenye maana na haifanani kwa vyovyote vile na ile baadhi watu wanayoisema: “Je, kazi hii Unayofanya haihitilafiani? Je, huu mfuatano wa kazi si mazoezi ya kujitatiza Wewe tu? Ulimwumba Shetani, kisha baadaye ukamruhusu Akakusaliti na kukupinga Wewe. Uliwaumba binadamu, na kisha ukamkabidhi Shetani, na Ukaruhusu Adamu na Hawa kujaribiwa. Kwa sababu uliyafanya mambo haya yote kimakusudi, kwa nini Unawachukia binadamu? Kwa nini Unachukia Shetani? Mambo haya si ya kujitungia Wewe? Ni nini kipo cha Wewe kuchukia?” Watu wengi wa kipumbavu watasema hayo. Wanatamani kumpenda Mungu, lakini mioyoni mwao wanalalamika kumhusu Mungu—ukinzani jinsi gani! Wewe huelewi ukweli, unazo fikira nyingi sana za kimiujiza, na pia unadai kwamba hili ni kosa la Mungu—wewe ni mpumbavu kiasi kipi! Ni wewe unayecheza na ukweli; si kosa la Mungu! Baadhi ya watu wataweza hata kulalamika na kulalamika: Ni wewe uliyemwumba Shetani, na ni Wewe uliyempa Shetani binadamu. Binadamu wanamiliki tabia ya kishetani; badala ya kuwasamehe, Unauchukia kwa kiwango fulani. Mwanzo Uliupenda binadamu kwa kiwango fulani. Ulimtimua Shetani hadi ulimwenguni mwa binadamu, na sasa Unawachukia binadamu. Ni wewe unayewachukia na kuwapenda binadamu—maelezo ya kauli hii ni yapi? Je, huu si ukinzani? Bila kujali ni vipi mnavyoangalia suala hili, hivi ndivyo ilivyofanyika mbinguni; malaika mkuu alimsaliti Mungu kwa njia hii, nao binadamu wakapotoshwa kwa njia hii, na ukaendelea mpaka leo kwa njia hii. Bila kujali ni vipi mnavyopangilia kauli hizi, hii ndiyo hadithi yote. Hata hivyo, lazima muelewe kwamba Mungu anaifanya kazi ya leo ili kuwaokoa nyinyi, na ili kumshinda Shetani.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Unapaswa Kujua Namna Ambavyo Binadamu Wote Wameendelea Hadi Siku ya Leo

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp