Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 417

Mtu huingiaje katika sala ya kweli?

Unapoomba, lazima uwe na moyo ambao ni mtulivu mbele ya Mungu, na lazima uwe na moyo mwaminifu. Wewe kweli unawasiliana kwa karibu na kuomba na Mungu—usimdanganye Mungu kwa kutumia maneno ya kupendeza. Sala lazima ilenge kile ambacho Mungu anataka kukamilisha leo. Mwombe Mungu akupe nuru na mwangaza mwingi zaidi, na ulete hali halisi na matatizo yako mbele za Mungu kuomba, na ufanye azimio mbele za Mungu. Sala sio kufuata utaratibu, bali ni kumtafuta Mungu kwa kutumia moyo wako wa kweli. Omba kwamba Mungu aulinde moyo wako, na Aufanye uwe na amani mara nyingi mbele za Mungu, Akuwezeshe kujijua, na kujidharau, na kujitupa katika mazingira ambayo Mungu amekuwekea, hivyo kukuruhusu uwe na uhusiano wa kawaida na Mungu na kukufanya mtu anayempenda Mungu kweli.

Ni nini umuhimu wa sala?

Sala ni mojawapo ya njia ambazo mwanadamu hutumia kushirikiana na Mungu, ni njia ambayo mwanadamu hutumia kumwita Mungu, na ni mchakato ambao mtu huguswa na Roho wa Mungu. Inaweza kusemwa kwamba wale ambao hawana sala ni wafu wasio na roho, ushahidi kwamba hawana uwezo wa kuguswa na Mungu. Bila sala, watu hawawezi kupata maisha ya kawaida ya kiroho, sembuse kuifuata kazi ya Roho Mtakatifu; bila sala, wao huvunja uhusiano wao na Mungu, na hawawezi kupokea kibali cha Mungu. Ukiwa mtu anayemwamini Mungu, kadri unavyoomba, ndivyo unavyozidi kuguswa na Mungu. Watu kama hao wana azimio kubwa zaidi na wanaweza kupokea zaidi nuru ya hivi karibuni kutoka kwa Mungu; kwa hivyo, watu kama hawa pekee ndio wanaweza kukamilishwa mapema iwezekanavyo na Roho Mtakatifu.

Je, ni matokeo gani yanayofaa kutimizwa kwa sala?

Watu wanaweza kutekeleza mazoea ya sala na kuelewa umuhimu wa sala, lakini matokeo yanayofaa kutimizwa kwa sala sio jambo rahisi. Sala sio jambo la kupitia urasmi wa kisheria, au kufuata utaratibu, au kukariri maneno ya Mungu, ambalo ni kusema, sala haimaanishi kuiga maneno kama kasuku na kuwaiga wengine. Katika sala, lazima umpe Mungu moyo wako, ukishiriki maneno yaliyo ndani ya moyo wako na Mungu ili uweze kuguswa na Mungu. Ikiwa maombi yako yatakuwa na matokeo, basi lazima yategemee usomaji wako wa maneno ya Mungu. Ni kwa kuomba tu katikati ya maneno ya Mungu ndipo utaweza kupokea nuru na mwangaza zaidi. Sala ya kweli huonyeshwa kwa kuwa na moyo ambao unatamani sana matakwa yaliyowekwa na Mungu, na kuwa tayari kutimiza matakwa haya; utaweza kuchukia yote ambayo Mungu huchukia, kwa msingi huo utakuwa na maarifa, na utajua na kuelewa wazi kuhusu ukweli ulioelezwa na Mungu. Kuwa na azimio, na imani, na maarifa, na njia ya kufanya mazoezi baada ya kuomba—huku tu ndiko kuomba kwa kweli, na sala kama hii tu ndiyo inaweza kuwa na ufanisi. Lakini sala lazima ijengwe juu ya msingi wa kufurahia maneno ya Mungu na kuwasiliana kwa karibu na Mungu katika maneno Yake, moyo wako ukiweza kumtafuta Mungu na kuwa na amani mbele ya Mungu. Sala kama hiyo tayari imefikia kiwango cha kuwasiliana kwa kweli na Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuhusu Desturi ya Sala

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp