Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 415

Ili kuishi maisha ya kawaida ya kiroho, lazima mtu aweze kupokea mwanga mpya kila siku na afuatilie ufahamu wa kweli wa maneno ya Mungu. Ni lazima mtu aone ukweli vyema, apate njia ya utendaji katika masuala yote, agundue maswali mapya kupitia kusoma maneno ya Mungu kila siku, na atambue upungufu wake mwenyewe ili aweze kuwa na moyo unaotamani na kutafuta ambao unaigusa nafsi yake nzima, na ili aweze kutulia mbele za Mungu nyakati zote, akiogopa sana kubaki nyuma. Mtu aliye na moyo kama huu unaotamani na kutafuta, aliye tayari kupata kuingia bila kusita, yuko kwenye njia sahihi ya maisha ya kiroho. Wale wanaoguswa na Roho Mtakatifu, wanaotaka kufanya vizuri zaidi, walio tayari kufuatilia kukamilishwa na Mungu, wanaotamani ufahamu wa kina wa maneno ya Mungu, wasiofuatilia jambo la mwujiza lakini badala yake wanalipa gharama ya kweli, wanaoyajali mapenzi ya Mungu kwa kweli, ambao kwa kweli wanapata kuingia ili uzoefu wao uwe wa kweli na halisi zaidi, wasiofuatilia maneno na mafundisho matupu ama kufuatilia kuhisi jambo la mwujiza, wasiomwabudu mtu yeyote mashuhuri—hawa ndio wale ambao wameingia katika maisha ya kawaida ya kiroho. Kila kitu wanachofanya kinanuiwa kufanikisha ukuaji zaidi katika maisha na kuwafanya wawe wapya na wachangamfu katika roho, na daima wanaweza kupata kuingia kwa shauku. Bila wao kujua, wanakuja kuuelewa ukweli na kuingia katika uhalisi. Wale walio na maisha ya kawaida ya kiroho hupata ukombozi na uhuru wa roho kila siku, na wanaweza kutenda maneno ya Mungu kwa njia huru mpaka Aridhike. Kwa watu hawa, kuomba si jambo la kidesturi ama utaratibu; kila siku, wanaweza kuwa sambamba na mwanga mpya. Kwa mfano, watu hujifunza kuituliza mioyo yao mbele za Mungu, na mioyo yao inaweza kutulia mbele za Mungu kwa kweli, na hawawezi kusumbuliwa na yeyote. Hakuna mtu, tukio ama jambo linaloweza kuzuia maisha yao ya kawaida ya kiroho. Mafunzo kama hayo yananuiwa kuleta matokeo; hayanuiwi kuwafanya watu wafuate kanuni. Utendaji huu hauhusu kufuata kanuni, lakini badala yake unahusu kukuza ukuaji katika maisha ya watu. Ikiwa unaona utendaji huu kuwa kanuni za kufuatwa tu, maisha yako hayatawahi kubadilika. Unaweza kuwa umeshiriki katika matendo sawa kama wengine, lakini wakati wao wanaweza hatimaye kuwa sambamba na kazi ya Roho Mtakatifu, unaondolewa kutoka katika mkondo wa Roho Mtakatifu. Je, hujidanganyi? Lengo la maneno haya ni kuwawezesha watu waitulize mioyo yao mbele za Mungu, waigeuze mioyo yao kumwelekea Mungu, ili kazi ya Mungu ndani yao iweze kutozuiwa na iweze kuzaa matunda. Ni baada ya hayo tu ndiyo watu wataweza kukubaliana na mapenzi ya Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kuhusu Maisha ya Kawaida ya Kiroho

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp