Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IX

Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (III) (Sehemu ya Tatu)

Mungu anaweka Uwiano Kati ya Vitu Vyote ili Kumpatia Binadamu Mazingira Imara kwa ajili ya Kuendelea Kuishi

Mungu anadhihirisha matendo Yake miongoni mwa vitu vyote na miongoni mwa vitu vyote Anavyovitawala na Anashikilia sheria za vitu vyote. Tumemaliza kusema juu ya jinsi ambavyo Mungu anatawala sheria za vitu vyote vilevile jinsi ambavyo Anawakimu na kuwalea binadamu wote ndani ya sheria hizo. Hiki ni kipengele kimoja. Kinachofuata, tutazungumza juu ya kipengele kingine, ambacho ni njia moja ambayo Mungu ana udhibiti wa kila kitu. Hivi ndivyo, baada ya kuumba vitu vyote, Akaweka uwiano wa uhusiano kati yao. Hii pia ni mada kubwa sana kwenu. Kuweka uwiano wa uhusiano kati ya vitu vyote—je, hiki ni kitu ambacho watu wanaweza kufanya? Binadamu wenyewe hawawezi. Watu wanaweza tu kuharibu. Hawawezi kuweka uwiano wa uhusiano kati ya vitu vyote; hawawezi kuvisimamia, wala hawana mamlaka makubwa hayo au nguvu. Ni Mungu Mwenyewe ndiye ana aina ya nguvu kuweza kufanya kitu cha aina hii. Kusudi la Mungu la kufanya kitu cha aina hii—kinamsaidia nini? Ni vilevile, inafanana kwa ukaribu na kuendelea kuishi kwa binadamu. Kila kitu ambacho Mungu anataka kufanya ni cha lazima—hakuna kitu ambacho Anaweza au asiweze kufanya. Ili Yeye alinde kuendelea kuishi kwa binadamu na kuwapatia watu mazingira faafu kwa ajili ya kuendelea kuishi, kuna vitu fulani vya lazima, vitu fulani vya muhimu sana ambavyo ni lazima Afanye kulinda kuendelea kuishi kwao.

Kutokana na maana ya moja kwa moja ya kirai “Mungu anaweka uwiano kwa vitu vyote,” ni mada pana sana; kwanza inakupatia dhana ili uweze kujua kwamba kuweka uwiano kwa vitu vyote ni utawala wa Mungu kwa vitu vyote. Neno “uwiano” linamaanisha nini? Kwanza, “uwiano” unamaanisha kutoruhusu kitu fulani kuwa nje ya uwiano. Kila mtu anajua kuhusu mizani. Unapotumia mizani kupima kitu fulani, unakiweka katika upande mmoja wa kipimo na kuweka uzito katika upande mwingine. Kiasi cha mwisho cha uzito kinaamua uzito wa kitu hicho—huo ndio unaitwa uwiano. Ili kuweka uwiano, uzito wa pande mbili lazima uwe sawa. Mungu aliumba vitu vingi miongoni mwa vitu vyote—Aliumba vitu ambavyo havibadiliki, vitu ambavyo vinajongea, vitu ambavyo vinaishi, na vitu ambavyo vinapumua, vilevile vile ambavyo havipumui. Je, ni rahisi kwa vitu hivi vyote kupata uhusiano wa kutegemeana, wa kusaidiana na kuzuiana, wa kuingiliana? Kwa hakika kuna kanuni fulani ndani ya jambo hili. Ingawa inatatiza sana, sio ngumu kwa Mungu. Hata hivyo, kwa watu, ni vigumu sana kufanya utafiti. Ni neno rahisi sana—uwiano. Hata hivyo, ikiwa watu wangelitafiti, ikiwa watu wangehitaji kutengeneza uwiano, basi hata kama wanataaluma wangekuwa wanalifanyia kazi—wanabiolojia wa kibinadamu, mamajusi, wanafizikia, wakemia na hata wanahistoria—matokeo ya mwisho ya utafiti huo yangekuwa ni yapi? Matokeo yake yasingekuwa chochote. Hii ni kwa sababu uumbaji wa Mungu wa vitu vyote ni wa ajabu sana na binadamu kamwe hataweza kufungua siri zake. Mungu alipoviumba vitu vyote, Alianzisha kanuni kati yao, Alianzisha njia tofautitofauti za kuendelea kuishi kwa ajili ya kuzuiana, kukamilishana, kuheshimiana, na riziki. Mbinu hizi mbalimbali zinatatiza sana; si rahisi au za kuelekea upande mmoja. Watu wanapotumia akili zao, maarifa yao, na tukio ambalo wamewahi kuona kuthibitisha au kutafiti kanuni zinazoongoza udhibiti wa Mungu wa vitu vyote, vitu hivi ni vigumu sana kuvigundua. Pia ni vigumu sana kugundua au kupata matokeo yoyote. Inaweza ikasemwa kwamba ni vigumu sana watu kupata matokeo. Ni vigumu sana kwa watu kupata matokeo, ni vigumu sana kwao kudumisha uwiano kwa kutegemea akili na maarifa yao kuongoza viumbe vyote vilivyoumbwa na Mungu. Hii ni kwa sababu kama watu hawajui kanuni za kuendelea kuishi kwa viumbe vyote, hawajui jinsi ya kulinda aina hii ya uwiano. Kwa hiyo, ikiwa watu wangeweza kusimamia na kuongoza viumbe vyote vya Mungu, kungekuwa na uwezekano mkubwa wa kuharibu uwiano. Mara tu utakapoharibiwa, mazingira yao kwa ajili ya kuendelea kuishi yangeweza kuharibiwa, na hiyo inapotokea, ingeweza kufuatiwa na mgogoro kwa ajili ya kuendelea kuishi kwao. Ingesababisha janga. Binadamu anapoishi katikati ya janga, nini kingeweza kutokea mbele yao? Yangekuwa ni matokeo ambayo ni vigumu kuyakisia, vigumu kuyabashiri.

Basi ni jinsi gani Mungu anaweka uwiano kwenye uhusiano kati ya vitu vyote? Kwanza, kuna baadhi ya maeneo duniani ambayo yamefunikwa na barafu na theluji kwa mwaka mzima, wakati katika baadhi ya maeneo, misimu yote minne ni kama msimu wa machipuo. Hutoweza kabisa kuona kipande cha barafu au chembe ya theluji—hakuna msimu wa baridi. Hii ni njia moja—ni kutokana na mtazamo mkubwa wa hali ya hewa. Aina ya pili ni pale watu wanapoona milima ikiwa na uoto uliostawi sana, ambapo aina zote za mimea inafunika ardhi; kuna malundo ya msitu na unapotembea katikati yao huwezi hata kuona jua. Katika milima mingine nyasi hata hazioti—kuna safu na safu za milima yenye ukame, isiyokaliwa. Ukiangalia kwa nje, yote ni milima yenye mchanga uliorundikana. Kundi moja la milima limejaa uoto uliositawi, na kundi jingine halina hata nyasi. Hii ni aina ya pili. Katika aina ya tatu, unaweza kuona tabaka la mbuga lisilokuwa na kikomo, uwanda wa kijani unaopunga. Au unaweza kuona jangwa kadri jicho linavyoweza kuona; huoni kiumbe hai yeyote, wala chanzo chochote cha maji, ni sauti tu ya upepo pamoja na mchanga. Katika aina ya nne, sehemu moja imefunikwa na bahari, ambayo imeundwa na eneo kubwa la maji, wakati katika sehemu nyingine unahangaika sana kutafuta chemchemi ya maji. Katika aina ya tano, katika nchi moja mvua ya manyunyu inanyesha mfululizo na ina ukungu na unyevunyevu, wakati kwenye nchi nyingine siku za jua kali ni za kawaida sana na hutaona hata tone moja la mvua. Katika aina ya sita, aina moja ya sehemu ni nchi tambarare ambapo hewa ni finyu sana na ni vigumu kupumua, na katika aina nyingine ya eneo kuna kinamasi na nyanda za chini, ambayo yanatumika kama makazi ya aina mbalimbali ya ndege wahamao. Hizi ni aina tofautitofauti za tabia ya nchi, au tabia za nchi au mazingira ambayo yanaitikia mazingira tofautitofauti ya kijiografia. Hiyo ni sawa na kusema, Mungu anaweka uwiano kwenye mazingira ya msingi ya binadamu kwa ajili ya kuendelea kuishi kutoka katika mtazamo wa mazingira makubwa, kutoka katika tabia ya nchi kwenda katika mazingira ya kijiografia, kutoka katika vijenzi tofauti vya udongo kwenye kiwango cha vyanzo vya maji ili kupata uwiano kwenye hewa, halijoto na unyevunyevu wa mazingira ambamo watu wanaendelea kuishi. Kwa tofauti hizi za mazingira tofauti ya kijiografia, watu watakuwa na hewa imara na halijoto na unyevunyevu katika misimu tofautitofauti vitakuwa imara. Hii inawaruhusu watu kuendelea kuishi katika aina hiyo ya mazingira kwa ajili ya kuendelea kuishi siku zote. Kwanza, mazingira makubwa yanapaswa kuwekewa uwiano. Hii inafanyika kupitia kutumia kikamilifu maeneo mbalimbali ya kijiografia na muundo na vilevile muachano kati ya hali za nchi tofautitofauti kwa ajili ya kuzuiana ili kupata uwiano ambao Mungu anataka na ambao binadamu anahitaji. Hii ni kutokana na mtazamo wa mazingira makubwa.

Ukiangalia kwenye maelezo, kama vile uoto, inawezekanaje kuifanya hiyo ipate uwiano? Yaani, ni jinsi gani uoto unaweza kuruhusiwa kuendelea kuishi ndani ya mazingira yenye uwiano kwa ajili ya kuendelea kuishi? Ni kwa kusimamia urefu wa maisha, viwango vya ukuaji, na viwango vya kuzaliana vya aina mbalimbali za mimea ili kulinda mazingira yao kwa ajili ya kuendelea kuishi. Chukulia nyasi dogo kama mfano—wakati wa machipuo linachipua, wakati wa kiangazi linatoa maua, na wakati wa majira ya kupukutika majani linatoa matunda. Tunda linaanguka kwenye ardhi na nyasi hii inakufa. Mwaka ujao, mbegu kutoka kwenye tunda inachipua na kukua kulingana na sheria zile zile. Urefu wa maisha ya nyasi ni mafupi sana. Kila mbegu inaanguka ardhini, inakuza mizizi na kuchipuka, inaweka maua na kuzaa matunda—hatua hii inatokea tu wakati wa machipuo, kiangazi na kupukutika, Aina zote za miti pia zina urefu wao wa maisha na vipindi tofauti kwa ajili ya kuchipua na kuzaa matunda. Baadhi ya miti hufa baada tu ya miaka 30 hadi 50—ina urefu wa maisha ya kuanzia miaka 30 hadi 50, lakini matunda yao huanguka ardhini, ambayo kisha hukuza mizizi na machipuko, maua na kuzaa tunda, na kuishi kwa miaka mingine 30 hadi 50. Hiki ndicho kiwango cha kujirudia kwake. Mti mzee unakufa na mti mdogo unakua—hii ndio maana siku zote unaona miti inaendelea kukua msituni. Lakini pia ina mzunguko wao mzuri na mchakato ama kuzaliwa na kufa. Baadhi ya miti inaweza kuishi kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu moja, na baadhi inaweza kuishi kwa hata miaka elfu tatu. Haijalishi ni aina gani ya mmea au urefu wao wa maisha ni mrefu kiasi gani, nikizungumza kwa ujumla, Mungu anasimamia uwiano wake kulingana na kipindi unachoishi, uwezo wake wa kuzaliana, kasi yake ya kuzaliana vilevile kiasi na kiwango chake cha kuzaliana. Hii inawaruhusu, kuanzia majani hadi miti, kuweza kuendelea kusitawi, kukua ndani ya mazingira ya kiikolojia yenye uwiano. Kwa hiyo unapoangalia msitu duniani, haijalishi kama ni miti au majani, unaendelea kujizalisha na kukua kulingana na sheria zake. Haihitaji msaada wa binadamu; haihitaji kazi yoyote ya ziada kutoka kwa binadamu. Ni kwa sababu tu wana aina hii ya uwiano ndipo wana uwezo wa kudumisha mazingira yao kwa ajili ya kuendelea kuishi. Ni kwa sababu tu wana mazingira faafu kwa ajili ya kuendelea kuishi ndipo misitu hii, kanda hizi za mbuga zinaweza kuendelea kuishi duniani. Uwepo wao unalea kizazi baada ya kizazi cha watu vilevile kizazi baada ya kizazi cha aina zote za viumbe hai vyenye makazi misituni na kwenye kanda za mbuga—ndege na wanyama, wadudu, na aina zote za vijiumbe.

Mungu pia anadhibiti uwiano wa aina zote za wanyama. Uwiano huu unadhibitiwaje? Ni sawa na kwenye mimea—anasimamia uwiano wao na anaamua idadi yao kulingana na uwezo wao wa kuzaliana, ukubwa na kiwango cha kuzaliana kwao na wajibu wanaoufanya miongoni mwa wanyama. Kwa mfano, simba hula pundamilia, kwa hiyo ikiwa idadi ya simba ingezidi idadi ya pundamilia, hatima ya pundamilia ingekuwaje? Wangepotea kabisa. Na ikiwa kuzaliana kwa pundamilia kungekuwa kwa idadi ndogo kuliko idadi ya simba, hatima yao ingekuwaje? Vilevile wangepotea kabisa. Kwa hiyo, idadi ya pundamilia inapaswa kuwa kubwa kuliko idadi ya simba. Hii ni kwa sababu pundamilia hawaishi tu kwa ajili yao; wanaishi pia kwa ajili ya simba. Unaweza pia kusema kwamba kila pundamilia ni sehemu moja ya pundamilia, lakini pia ni chakula katika kinywa cha simba. Kasi ya simba ya kuzaliana haiwezi kamwe kuiacha ile ya pundamilia, kwa hiyo idadi yao haiwezi kuwa kubwa kuliko idadi ya pundamilia. Ni kwa njia hii tu ndipo chanzo cha chakula cha simba kinaweza kuhakikishwa. Na kwa hivyo, ingawa simba ni maadui wa asili wa pundamilia, watu mara kwa mara huwaona wakiwa wamepumzika kwa kustarehe katika eneo moja. Pundamilia hawatapungua idadi au kupotea kabisa kwa sababu simba wanawawinda na kuwala, na simba hawataongezeka idadi yao kwa sababu ya hadhi yao kama “mfalme.” Uwiano huu ni kitu ambacho Mungu alikianzisha zamani sana. Yaani, Mungu alianzisha sheria za uwiano kati ya wanyama wote ili kwamba waweze kupata uwiano, na hiki ni kitu ambacho watu mara nyingi huona. Je, simba ni adui pekee wa asili wa pundamilia? La, mamba pia hula pundamilia. Kumshuhudia mamba akimla pundamilia pia ni kitendo cha ukatili. Pundamilia anaonekana kuwa mnyama asiyekuwa na msaada kabisa. Hawana ukali kama wa simba, na wanapomkabili adui huyu wa kutisha, wanaweza kukimbia tu. Hawawezi hata kutoa upinzani. Wakati ambapo hawawezi kumshinda mbio simba, wanaweza kujiruhusu tu waliwe naye. Hii inaweza kuonekana mara kwa mara katika ulimwengu wa wanyama. Mnapata wazo gani mnapoona kitu cha namna hii? Je, unamhurumia pundamilia? Je, unamchukia simba? Pundamilia wanaonekana wazuri sana. Lakini simba, siku zote wanawaangalia kwa tamaa. Na kwa upumbavu, pundamilia hawakimbii mbali sana. Wanawaangalia simba pale wakiwasubiri, kwa kawaida wakiwasubiri chini ya kivuli cha mti. Nani anajua ni wakati gani atawala. Wanajua hili mioyoni mwao, lakini hawatalihama eneo hilo. Hili ni jambo la ajabu. Jambo hili la ajabu linajumuisha majaliwa ya Mungu, kanuni Yake. Unamhurumia pundamilia lakini huna uwezo wa kumsaidia, na unahisi kwamba simba ni wa kuchukiwa lakini huwezi ukamwepuka. Pundamilia ni chakula ambacho Mungu amekiandaa kwa ajili ya simba, lakini haijalishi ni kwa namna gani simba wanawala, pundamilia hawatamalizwa. Idadi ya watoto ambao simba wanazaa ni ndogo sana, na wanazaa polepole sana, kwa hiyo haijalishi ni pundamilia ngapi wanakula, idadi zao haziwezi kuzidi za pundamilia. Hii ni aina ya uwiano.

Lengo la Mungu ni lipi katika kudumisha aina hii ya uwiano? Hii inahusiana na mazingira ya watu kwa ajili ya kuendelea kuishi vilevile kuendelea kuishi kwa binadamu. Ikiwa pundamilia au mawindo mengine ya simba—paa au wanyama wengineo—watazaliana taratibu sana na idadi ya simba ikaongezeka haraka, ni aina gani ya hatari ambayo binadamu wangepata? Simba kuwala pundamilia ni tukio la kawaida, lakini ikiwa simba angewala watu, lingekuwa ni janga. Janga hili sio kitu ambacho kilipangwa kabla na Mungu, halipo ndani ya sheria Yake, wala kile ambacho amekileta kwa ajili ya binadamu. Badala yake, ni kile ambacho watu wamejiletea wenyewe. Kwa hiyo kama Mungu aonavyo, uwiano kati ya vitu vyote ni muhimu kwa ajili ya binadamu kuendelea kuishi. Iwe ni mimea au wanyama hawawezi kupoteza uwiano wao sahihi. Mimea, wanyama, milima, na maziwa—Mungu amewaandalia binadamu mazingira ya kawaida ya kiikolojia. Hadi pale tu ambapo watu watakuwa na aina hii ya mazingira ya kiikolojia—yenye uwiano—ndipo kuendelea kuishi kwao kutakuwa salama. Ikiwa miti au nyasi ingekuwa na uwezo mdogo wa kuzalisha au kasi yake ya uzalishaji ingekuwa ya taratibu sana, je, udongo ungepoteza unyevunyevu wake? Ikiwa udongo ungepoteza unyevunyevu wake, je, bado ungekuwa na afya? Ikiwa udongo ungepoteza uoto wake na unyevunyevu wake, ungemomonyoka haraka sana, na mchanga ungetokea badala yake. Wakati udongo ulipoharibika, mazingira ya watu kwa ajili ya kuendelea kuishi pia yangeharibika. Pamoja na uharibifu huu majanga yangeweza kutokea. Bila aina hii ya uwiano wa kiikolojia, bila aina hii ya mazingira ya kiikolojia, watu wangeendelea kuathirika na majanga kwa sababu ya kukosa uwiano baina ya vitu hivi vyote. Kwa mfano, wakati kunapokuwa na kukosekana kwa uwiano wa kimazingira hadi kusababisha uharibifu wa mazingira ya ikolojia ya vyura, wote wanakusanyika pamoja, idadi yao inaongezeka haraka sana na watu hata wanaona idadi kubwa ya vyura wanapita mtaani mijini, na idadi kubwa ya vyura barabarani. Ikiwa idadi kubwa ya vyura ingechukua sehemu kubwa ya mazingira ya watu kwa ajili ya kuendelea kuishi, hiyo ingeitwaje? Janga. Kwa nini liitwe janga? Wanyama hawa wadogo ambao wana manufaa kwa binadamu wana faida kwa watu wanapobaki katika eneo ambalo ni faafu kwao; wanadumisha uwiano wa mazingira ya watu kwa ajili ya kuendelea kuishi. Mara tu wanapokuwa janga, wataathiri mpangilio wa maisha ya watu. Vitu vyote na vipengele vyote ambavyo chura wanavileta vinaweza kuathiri ubora wa maisha ya watu. Hata ogani zao za kimwili zinaweza kushambuliwa—hii ni moja ya aina ya majanga. Aina nyingine ya janga, ambalo ni kitu ambacho binadamu wamepitia mara kwa mara—ni kutokea kwa idadi kubwa ya nzige. Hili si janga? Hili ni janga la kutisha. Haijalishi binadamu wana uwezo kiasi gani—watu wanaweza kutengeneza ndege, mizinga, na mabomu ya atomiki—lakini pale ambapo nzige wanawavamia binadamu, wanakuwa na suluhisho gani? Je, wanaweza kuwashambulia kwa mizinga? Je, wanaweza kuwafyatulia risasi kwa bunduki? Hawawezi. Basi wanaweza kuwanyunyizia dawa ya kuua wadudu ili kuwafukuza? Hiyo si rahisi pia. Hao nzige wadogo wanakuja kufanya nini? Wao haswa hula mimea na nafaka. Popote pale nzige watakapokwenda, mazao na nafaka yanafutiliwa mbali kabisa. Kwa hivyo, chini ya uvamizi wa nzige, kufumba na kufumbua, chakula ambacho wakulima wanakitegemea—nafaka za mwaka mzima—zingeweza kuliwa kabisa na nzige. Kwa binadamu, ujio wa nzige sio tu kero—ni janga. Nzige ni aina ya janga, sasa vipi kuhusu panya? Ikiwa hakuna ndege wowote mbua wa kula panya, watazaliana haraka sana, haraka kuliko unavyoweza kufikiri. Na ikiwa kuenea kwa panya hakutadhibitiwa, je, binadamu wanaweza kuishi maisha mazuri? Kwa hivyo ni kitu gani ambacho binadamu wangekabiliana nacho? (Tauni.) Tauni tu? Panya watatafuna kila kitu. Watatafuna hata mbao. Ikiwa kuna panya wawili tu katika nyumba, kila mtu kwenye nyumba yote atachukizwa. Wakati mwingine wanaiba mafuta na kula, wakati mwingine wanakula nafaka. Na vitu ambavyo hawali wanavitafuna tu na kuvivuruga kabisa. Wanatafuna nguo, viatu, fanicha—wanatafuna kila kitu. Wakati mwingine watapanda kwenye uchaga wa vyombo—je, vyombo hivyo bado vinaweza kutumiwa? Hata kama utavisafisha hutahisi una amani, kwa hiyo unavitupa tu nje. Hii ndiyo shida ambayo panya wanawapatia watu. Ni panya wadogo tu, lakini watu hawana namna ya kushughulika nao. Wamefanyiwa hata udhalimu na hao panya. Hakuna haja ya kuzungumzia kundi lote la panya—panya wawili tu wanatosha kufanya uharibifu. Kama wangekuwa janga, madhara yake hayawezi kufikirika. Na ikiwa mchwa wadogo wangekuwa janga, yale madhara ambayo wangefanya kwa binadamu pia yasingeweza kupuuzwa. Mchwa kula mbao kwa kiwango ambacho hadi nyumba inaanguka ni tukio la kawaida. Uwezo wao hauwezi kupuuzwa. Lingekuwa jambo la kuogofya ikiwa aina tofauti za ndege wangesababisha janga? (Ndiyo.) Kusema vingine, haijalishi wao ni aina gani ya wanyama au viumbe hai, mara tu watakapopoteza uwiano wao, watakua, kuzaliana, na kuishi ndani ya mawanda yasiyokuwa ya kawaida, mawanda yasiyofuata kanuni. Hiyo ingeweza kuleta madhara yasiyoweza kufikirika kwa binadamu. Hiyo isingeweza kuathiri kuendelea kuishi na maisha ya watu tu, bali pia ingeleta janga kwa binadamu, hata kufikia hatua ambapo watu watapatwa na maangamizo, watapatwa na hatma ya kufa.

Mungu alipoumba vitu vyote, alitumia aina zote za mbinu na njia za kuziwekea uwiano, kuweka uwiano katika mazingira ya kuishi kwa ajili ya milima na maziwa, kuweka uwiano katika mazingira ya kuishi kwa ajili ya mimea na aina zote za wanyama, ndege, wadudu—lengo Lake lilikuwa ni kuruhusu aina zote za viumbe hai kuishi na kuongezeka ndani ya sheria ambazo alikuwa Amezianzisha. Viumbe vyote haviwezi kwenda nje ya sheria hizi na haziwezi kuvunjwa. Ni ndani ya aina hii tu ya mazingira ya msingi ndipo binadamu wanaweza kuendelea kuishi kwa usalama na kuongezeka, kizazi baada ya kizazi. Ikiwa kiumbe yeyote anakwenda zaidi ya ukubwa au mawanda yaliyoanzishwa na Mungu, au ikiwa anazidi kiwango cha ukuaji, marudio, au idadi chini ya utawala Wake, mazingira ya binadamu kwa ajili ya kuendelea kuishi yangepata uharibifu wa viwango vinavyotofautiana. Na wakati uo huo, kuendelea kuishi kwa binadamu kungetishiwa. Ikiwa aina moja ya kiumbe hai ni kubwa sana kwa idadi, itawanyang’anya watu chakula chao, kuharibu vyanzo vya maji ya watu, na kuharibu makazi yao. Kwa njia hiyo, kuzaliana kwa binadamu au hali ya kuendelea kuishi ingeathiriwa mara moja. Kwa mfano, maji ni muhimu sana kwa vitu vyote. Ikiwa kuna idadi kubwa sana ya panya, siafu, nzige, na vyura, au wanyama wengine wa kila aina, watakunywa maji zaidi. Kadri kiwango cha maji wanachokunywa kinaongezeka, ndani ya mawanda haya yasiyobadilika ya vyanzo vya maji ya kunywa na maeneo ya majimaji, maji ya kunywa ya watu na vyanzo vya maji vitapungua, na watapungukiwa maji. Ikiwa maji ya kunywa ya watu yataharibiwa, kuchafuliwa au kuangamizwa kwa sababu aina zote za wanyama zimeongezeka kwa idadi, chini ya aina hiyo ya mazingira katili kwa ajili ya kuendelea kuishi, kuendelea kuishi kwa binadamu hakika kutakuwa kumetishiwa vikali. Ikiwa kuna aina moja au aina kadhaa za viumbe hai ambavyo vinazidi idadi yao inayofaa, hewa, halijoto, unyevunyevu, na hata vijenzi vya hewa ndani ya eneo la binadamu kwa ajili ya kuendelea kuishi litakuwa na sumu na kuharibiwa kwa viwango vinavyotofautiana. Hali kadhalika, chini ya mazingira haya, kuendelea kuishi kwa binadamu na hatma bado vitakuwa chini ya tishio la aina hiyo ya mazingira. Kwa hiyo, ikiwa watu watapoteza uwiano huu, hewa wanayovuta itaharibiwa, maji wanayokunywa yatachafuliwa, na halijoto ambayo wanahitaji pia itabadilika, itaathiriwa kwa viwango tofautitofauti. Ikiwa hiyo itatokea, mazingira asilia ya binadamu kwa ajili ya kuendelea kuishi yataandamwa na madhara na changamoto kubwa. Chini ya aina hii ya mazingira ambapo mazingira ya msingi ya binadamu kwa ajili ya kuendelea kuishi yameharibiwa, hatma na matarajio ya binadamu yatakuwa ni nini? Ni tatizo kubwa sana! Kwa sababu Mungu anajua vitu vyote ni nini kwa binadamu, wajibu wa kila aina ya kitu Alichokiumba, aina gani ya athari kinacho kwa watu, na faida kubwa kiasi gani kinaleta kwa binadamu—katika moyo wa Mungu kuna mpango kwa ajili ya haya yote na Anasimamia kila kipengele cha vitu vyote alivyoviumba, kwa hiyo kwa binadamu, kila kitu Anachofanya ni muhimu sana—vyote ni lazima. Kwa hiyo wakati unaona baadhi ya matukio ya kiikolojia miongoni mwa vitu vyote, au baadhi ya sheria za asili miongoni mwa vitu vyote, hutashuku tena ulazima wa kila kitu ambacho kiliumbwa na Mungu. Hutatumia tena maneno ya kijinga kufanya hukumu zisizokuwa na msingi juu ya mipangilio ya Mungu juu ya vitu vyote na njia zake mbalimbali za kuwakimu binadamu. Pia hutafanya mahitimisho yasiyokuwa na msingi juu ya sheria za Mungu kwa ajili ya vitu vyote ambavyo Aliviumba. Je, hii haiko hivyo?

Je, haya yote tuliyoyazungumza ni nini? Yafikirie. Mungu ana nia Yake katika kila kitu anachofanya. Ingawa binadamu hawawezi kuona nia hiyo, siku zote inahusiana na kuendelea kuishi kwa binadamu. Inahusiana bila kutenganishwa nayo—ni ya lazima. Hii ni kwa sababu Mungu hajawahi kufanya kitu ambacho hakina manufaa. Kwa kila kitu ambacho Anafanya, mpango Wake upo ndani ya nadharia na kanuni zake, ambazo zinajumuisha hekima Yake. Lengo la mpango na nia hiyo ni kwa ajili ya ulinzi wa binadamu, kumsaidia binadamu kuzuia janga, uvamizi wa kiumbe chochote hai, na aina yoyote ya madhara kwa binadamu yasababishwayo na vitu vyote. Kwa hiyo kutokana na matendo ya Mungu ambayo tumeyaona kutoka katika mada hii ambayo tunaijadili, tungeweza kusema kwamba Mungu anawakimu binadamu kwa njia nyingine? Je, tungeweza kusema kwamba Mungu anawalisha na kuwachunga binadamu kwa njia hii? (Ndiyo.) Je, kuna uhusiano mkubwa kati ya mada hii na anwani ya ushirika wetu, “Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote”? (Ndiyo.) Kuna uhusiano mkubwa, na mada hii ni kipengele kimoja chake. Kabla ya kuzungumza kuhusu mada hizi, watu walikuwa tu na fikra zisizo dhahiri juu ya Mungu, Mungu Mwenyewe na matendo Yake—hawakuwa na uelewa wa kweli juu ya vitu hivi. Hata hivyo, watu wanapoambiwa kuhusu matendo Yake na vitu ambavyo Amefanya, wanaweza kuelewa na kufahamu kanuni za kile ambacho Mungu anafanya na wanaweza kupata uelewa juu yake, sio? (Ndiyo.) Ingawa katika moyo wa Mungu, nadharia Zake, kanuni Zake, na Sheria Zake zinatatiza sana Anapokuwa anafanya kitu chochote, Alipotengeneza vitu vyote, na Anapotawala vitu vyote, ikiwa kitu kimoja kimechukuliwa kushiriki na nyinyi katika ushirika, je, hamtaweza kuelewa mioyoni mwenu kwamba haya ni matendo ya Mungu, na yapo thabiti sana? (Ndiyo.) Basi ni kwa jinsi gani uelewa wenu wa sasa juu ya Mungu ni tofauti na ulivyokuwa kabla? Ni tofauti kwa asili yake. Mlichokielewa kabla kilikuwa tupu, kisicho dhahiri sana, na kila mnachokielewa sasa kinajumuisha kiasi kikubwa cha ushahidi thabiti kushikilia matendo ya Mungu, kulinganisha na kile Mungu anacho na alicho. Kwa hiyo, yote ambayo nimeyasema ni nyenzo nzuri sana kwa ajili ya uelewa wa Mungu.

Hayo ndiyo kwa ajili ya kusanyiko la leo. Kwaheri! Kuwa na jioni njema! (Kwa heri, Mwenyezi Mungu.)

Februari 9, 2014

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp