109. Upendo wa Mungu kwa Binadamu
Uliyezaliwa katika nchi hii ya uchafu,
Unastahimili aibu na mateso makubwa.
Unaonyesha ukweli na kuwahukumu binadamu.
Maneno Yako yanawashinda maadui wote.
Uliyezaliwa katika nchi hii ya uchafu,
Unastahimili aibu na mateso makubwa.
Unaonyesha ukweli na kuwahukumu binadamu.
Maneno Yako yanawashinda maadui wote.
Hujawahi kufurahia mapenzi ya ujana.
Hushiriki katika furaha ya familia.
Unavumilia aibu na kuhisi huzuni, ni nani anayeweza kuelewa uchungu Wako?
Umetoa kila kitu kuwaokoa binadamu.
Unajinyenyekeza Mwenyewe kuwa mwanadamu na kukumbana na shida pamoja na mwanadamu.
Una wasiwasi kwa mwanadamu usiku na mchana,
Umesema yote yaliyopo ya kusemwa na moyo Wako unahuzunika kwa ajili ya mwanadamu.
Upendo Wako ni wa kweli na mzuri, unaomba moyo Wangu uamke.
Maneno Yako yanaonyesha uweza Wako, moyo Wangu umeshindwa.
Tabia Yako ni ya haki sana, inavutia uchaji moyoni mwangu.
Unahukumu kwa maneno Yako na Ninapata utakaso na wokovu.
Upendo wako ni vigumu kuupima, moyo wangu hautaki chochote zaidi.
Kwa uaminifu, najigharimu kwa ajili Yako kulipiza neema Yako kwa maisha yangu yote.